< Mika 5 >

1 Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi, kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu. Watampiga mtawala wa Israeli shavuni kwa fimbo.
Yet now gather yourselves in troops, O people of troops! They lay siege against us; With a rod they smite the cheek of the judge of Israel.
2 “Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi, ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli, ambaye asili yake ni kutoka zamani, kutoka milele.”
But thou, Bethlehem Ephratah, Who art small to be among the thousands of Judah, Out of thee shall he come forth for me to be ruler in Israel, Whose origin is from the ancient age, from the days of old!
3 Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati mwanamke aliye na utungu atakapozaa na ndugu zake wengine warudi kujiunga na Waisraeli.
But He [[Jehovah]] shall deliver them up, Until she that bringeth forth hath brought forth; Then shall the residue of his brethren return to the children of Israel.
4 Atasimama na kulichunga kundi lake katika nguvu ya Bwana, katika utukufu wa jina la Bwana Mungu wake. Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.
He shall stand and rule in the strength of Jehovah, In the majesty of Jehovah, his God; And they shall dwell in security, For he shall be great even to the ends of the earth.
5 Naye atakuwa amani yao. Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu na kupita katika ngome zetu, tutawainua wachungaji saba dhidi yake, hata viongozi wanane wa watu.
And he shall be peace. When the Assyrian shall come into our land, To trample upon our palaces, Then shall we raise against him seven shepherds, And eight leaders of the people,
6 Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga, nchi ya Nimrodi kwa upanga. Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru atakapoivamia nchi yetu na kuingia katika mipaka yetu.
And they shall devour the land of Assyria with the sword, The land of Nimrod within her gates. Thus shall he deliver us from the Assyrian, when he cometh into our land, And treadeth in our borders.
7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa katikati ya mataifa mengi kama umande kutoka kwa Bwana, kama manyunyu juu ya majani, ambayo hayamngoji mtu wala kukawia kwa mwanadamu.
The residue of Jacob shall be in the midst of many nations As the dew which cometh from Jehovah, As drops of rain upon the grass, Which tarrieth not for man, Nor waiteth for the sons of men.
8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, katikati ya mataifa mengi, kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni, kama mwana simba miongoni mwa makundi ya kondoo, ambaye anaumiza vibaya na kuwararua kila anapopita katikati yao, wala hakuna awezaye kuokoa.
The residue of Jacob shall be among the nations, In the midst of many kingdoms, As a lion among the beasts of the forest, As a young lion among flocks of sheep, Who, when he assaulteth, treadeth down and teareth, and none can deliver.
9 Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako, nao adui zako wote wataangamizwa.
Thy hand shall be lifted up over thine adversaries, And all thine enemies shall be destroyed!
10 “Katika siku ile,” asema Bwana, “nitaangamiza farasi zenu katikati yenu na kubomoa magari yenu ya vita.
It shall come to pass in that day, saith Jehovah, That I will destroy thy horses from the midst of thee, And I will consume thy chariots;
11 Nitaiangamiza miji ya nchi yenu na kuziangusha chini ngome zenu zote.
I will destroy the fortified cities of thy land, And throw down all thy strongholds;
12 Nitaangamiza uchawi wenu na hamtapiga tena ramli.
I will destroy sorceries from thy borders, And soothsayers shall not be with thee.
13 Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu; hamtasujudia tena kazi ya mikono yenu.
I will destroy thy graven images and thy statues from the midst of thee, And thou shalt no more bow down to the work of thine hands;
14 Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu na kubomoa miji yenu.
I will root out thy Astartes from the midst of thee, And I will destroy thy fortified cities;
15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”
And I will execute vengeance in anger and in fury Upon the nations which have not hearkened to me.

< Mika 5 >