< Mika 5 >

1 Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi, kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu. Watampiga mtawala wa Israeli shavuni kwa fimbo.
Now shalt thou gather thyself in troops, O daughter of troops; they have laid siege against us; they smite the judge of Israel with a rod upon the cheek.
2 “Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi, ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda, kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli, ambaye asili yake ni kutoka zamani, kutoka milele.”
But thou, Beth-lehem Ephrathah, which art little to be among the thousands of Judah, out of thee shall one come forth unto Me that is to be ruler in Israel; whose goings forth are from of old, from ancient days.
3 Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati mwanamke aliye na utungu atakapozaa na ndugu zake wengine warudi kujiunga na Waisraeli.
Therefore will He give them up, until the time that she who travaileth hath brought forth; then the residue of his brethren shall return with the children of Israel.
4 Atasimama na kulichunga kundi lake katika nguvu ya Bwana, katika utukufu wa jina la Bwana Mungu wake. Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.
And he shall stand, and shall feed his flock in the strength of the LORD, in the majesty of the name of the LORD his God; and they shall abide, for then shall he be great unto the ends of the earth.
5 Naye atakuwa amani yao. Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu na kupita katika ngome zetu, tutawainua wachungaji saba dhidi yake, hata viongozi wanane wa watu.
And this shall be peace: when the Assyrian shall come into our land, and when he shall tread in our palaces, then shall we raise against him seven shepherds, and eight princes among men.
6 Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga, nchi ya Nimrodi kwa upanga. Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru atakapoivamia nchi yetu na kuingia katika mipaka yetu.
And they shall waste the land of Assyria with the sword, and the land of Nimrod with the keen-edged sword; and he shall deliver us from the Assyrian, when he cometh into our land, and when he treadeth within our border.
7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa katikati ya mataifa mengi kama umande kutoka kwa Bwana, kama manyunyu juu ya majani, ambayo hayamngoji mtu wala kukawia kwa mwanadamu.
And the remnant of Jacob shall be in the midst of many peoples, as dew from the LORD, as showers upon the grass, that are not looked for from man, nor awaited at the hands of the sons of men.
8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa, katikati ya mataifa mengi, kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni, kama mwana simba miongoni mwa makundi ya kondoo, ambaye anaumiza vibaya na kuwararua kila anapopita katikati yao, wala hakuna awezaye kuokoa.
And the remnant of Jacob shall be among the nations, in the midst of many peoples, as a lion among the beasts of the forest, as a young lion among the flocks of sheep, who, if he go through, treadeth down and teareth in pieces, and there is none to deliver.
9 Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako, nao adui zako wote wataangamizwa.
Let Thy hand be lifted up above Thine adversaries, and let all Thine enemies be cut off.
10 “Katika siku ile,” asema Bwana, “nitaangamiza farasi zenu katikati yenu na kubomoa magari yenu ya vita.
And it shall come to pass in that day, saith the LORD, that I will cut off thy horses out of the midst of thee, and will destroy thy chariots;
11 Nitaiangamiza miji ya nchi yenu na kuziangusha chini ngome zenu zote.
And I will cut off the cities of thy land, and will throw down all thy strongholds;
12 Nitaangamiza uchawi wenu na hamtapiga tena ramli.
And I will cut off witchcrafts out of thy hand; and thou shalt have no more soothsayers;
13 Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu; hamtasujudia tena kazi ya mikono yenu.
And I will cut off thy graven images and thy pillars out of the midst of thee; and thou shalt no more worship the work of thy hands.
14 Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu na kubomoa miji yenu.
And I will pluck up thy Asherim out of the midst of thee; and I will destroy thine enemies.
15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”
And I will execute vengeance in anger and fury upon the nations, because they hearkened not.

< Mika 5 >