< Mika 4 >
1 Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote; utainuliwa juu ya vilima, na watu wa mataifa watamiminika humo.
Mais il arrivera, aux derniers jours, que la montagne de la maison de l'Éternel sera établie au-dessus des montagnes, et elle s'élèvera par-dessus les collines, et les peuples y afflueront.
2 Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
Et des nations nombreuses iront, et diront: Venez et montons à la montagne de l'Éternel, à la maison du Dieu de Jacob; il nous instruira de ses voies, et nous marcherons dans ses sentiers! Car la loi sortira de Sion, et la parole de l'Éternel, de Jérusalem.
3 Atahukumu kati ya mataifa mengi, na ataamua migogoro ya mataifa yenye nguvu na yaliyo mbali. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
Il jugera entre des peuples nombreux, et sera l'arbitre de nations puissantes, jusqu'aux pays lointains; ils forgeront de leurs épées des hoyaux, et de leurs lances, des serpes; une nation ne lèvera plus l'épée contre l'autre, et on n'apprendra plus la guerre.
4 Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakuna mtu atakayewaogopesha, kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.
Mais chacun habitera sous sa vigne et sous son figuier, sans que personne les épouvante; car la bouche de l'Éternel des armées a parlé.
5 Mataifa yote yanaweza kutembea katika jina la miungu yao; sisi tutatembea katika jina la Bwana Mungu wetu milele na milele.
Quand tous les peuples marchent chacun au nom de son dieu, nous, nous marcherons au nom de l'Éternel notre Dieu, à toujours et à perpétuité!
6 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “nitawakusanya walemavu; nitawakusanya walio uhamishoni na wale niliowahuzunisha.
En ce jour-là, dit l'Éternel, je rassemblerai les boiteux, je recueillerai ceux qui étaient chassés, ceux que j'avais maltraités;
7 Nitawafanya walemavu kuwa mabaki, wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu. Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni kuanzia siku hiyo na hata milele.
Et je ferai de ceux qui boitent un reste, et de ceux qui ont été éloignés une nation puissante; et l'Éternel régnera sur eux, à la montagne de Sion, dès lors et à toujours.
8 Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi, ee ngome ya Binti Sayuni, milki ya awali itarudishwa kwako, ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”
Et toi, tour du troupeau, colline de la fille de Sion, jusqu'à toi viendra, à toi arrivera l'ancienne domination; la royauté sera à la fille de Jérusalem.
9 Kwa nini sasa unalia kwa nguvu: kwani huna mfalme? Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate kama ya mwanamke aliye na utungu wa kuzaa?
Pourquoi maintenant pousses-tu des cris? N'y a-t-il pas de roi au milieu de toi, ou ton conseiller a-t-il péri, pour que la douleur t'ait saisie comme celle qui enfante?
10 Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa, kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji ukapige kambi uwanjani. Utakwenda Babeli; huko utaokolewa. Huko Bwana atakukomboa kutoka mikononi mwa adui zako.
Sois en travail et crie, fille de Sion, comme celle qui enfante! Car maintenant tu sortiras de la ville, et tu demeureras aux champs, et tu iras jusqu'à Babylone. Là tu seras délivrée; là, l'Éternel te rachètera de la main de tes ennemis.
11 Lakini sasa mataifa mengi yamekusanyika dhidi yako. Wanasema, “Mwache anajisiwe, macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”
Et maintenant plusieurs nations se rassemblent contre toi, qui disent: “Qu'elle soit profanée, et que notre œil voie en Sion ce qu'il désire! “
12 Lakini hawayajui mawazo ya Bwana; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.
Mais elles ne connaissent pas les pensées de l'Éternel, et elles ne comprennent pas son dessein; car il les a rassemblées comme des gerbes dans l'aire.
13 “Inuka upure, ee Binti Sayuni, kwa kuwa nitakupa pembe za chuma; nitakupa kwato za shaba na utavunja vipande vipande mataifa mengi.” Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana, utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.
Lève-toi et foule, fille de Sion! Car je te ferai une corne de fer et des ongles d'airain, et tu broieras des peuples nombreux, et je vouerai comme un interdit leur butin à l'Éternel, et leurs richesses au Seigneur de toute la terre.