< Mika 4 >

1 Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote; utainuliwa juu ya vilima, na watu wa mataifa watamiminika humo.
And in the laste of daies the hil of the hous of the Lord schal be maad redi in the cop of hillis, and hiy ouer smale hillis. And puplis schulen flete to him, and many puplis schulen haaste,
2 Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
and shulen seie, Come ye, stie we til to the hil of the Lord, and to the hous of God of Jacob; and he schal teche vs of hise weies, and we schulen go in hise pathis. For lawe schal go out fro Syon, and the word of the Lord fro Jerusalem;
3 Atahukumu kati ya mataifa mengi, na ataamua migogoro ya mataifa yenye nguvu na yaliyo mbali. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
and he schal deme bitwixe many puplis, and schal chastise stronge folkis til in to fer. And thei schulen bete togidere her swerdis in to scharis, and her speris in to picoisis; a folc schal not take swerd ayens folc, and thei schulen no more lerne for to fiyte.
4 Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakuna mtu atakayewaogopesha, kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.
And a man schal sitte vndur his vyneyerd, and vndur his fige tree; and ther schal not be that schal make aferd, for the mouth of the Lord of oostis spak.
5 Mataifa yote yanaweza kutembea katika jina la miungu yao; sisi tutatembea katika jina la Bwana Mungu wetu milele na milele.
For alle puplis schulen go, ech man in the name of his Lord God; but we schulen walke in the name of oure Lord God in to the world, and ouer.
6 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “nitawakusanya walemavu; nitawakusanya walio uhamishoni na wale niliowahuzunisha.
In that dai, seith the Lord, Y schal gadere the haltynge, and Y schal gadere hir that Y castide awei, and whom Y turmentide Y schal coumforte.
7 Nitawafanya walemavu kuwa mabaki, wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu. Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni kuanzia siku hiyo na hata milele.
And Y schal putte the haltynge in to relifs, ether remenauntis, and hir that trauelide, in a strong folc. And the Lord schal regne on hem in the hil of Sion, fro this now and til in to with outen ende.
8 Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi, ee ngome ya Binti Sayuni, milki ya awali itarudishwa kwako, ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”
And thou, `derk tour of the floc of the douyter of Sion, `til to thee he schal come, and the first power schal come, the rewme of the douytir of Jerusalem.
9 Kwa nini sasa unalia kwa nguvu: kwani huna mfalme? Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate kama ya mwanamke aliye na utungu wa kuzaa?
Now whi art thou drawun togidere with mournyng? whether a kyng is not to thee, ether thi counselour perischide? for sorowe hath take thee, as a womman trauelinge of child.
10 Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa, kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji ukapige kambi uwanjani. Utakwenda Babeli; huko utaokolewa. Huko Bwana atakukomboa kutoka mikononi mwa adui zako.
Thou douyter of Sion, make sorewe, and haaste, as a womman trauelynge of child; for now thou schalt go out of the citee, and schalt dwelle in cuntree, and schalt come `til to Babiloyne; there thou schalt be delyuered, there the Lord schal ayen bie thee, fro the hond of thin enemyes.
11 Lakini sasa mataifa mengi yamekusanyika dhidi yako. Wanasema, “Mwache anajisiwe, macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”
And now many folkis ben gaderid on thee, whiche seien, Be it stonyd, and oure iye biholde in to Sion.
12 Lakini hawayajui mawazo ya Bwana; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.
Forsothe thei knewen not the thouytis of the Lord, and vndurstoden not the councel of hym, for he gaderide hem as the hei of feeld.
13 “Inuka upure, ee Binti Sayuni, kwa kuwa nitakupa pembe za chuma; nitakupa kwato za shaba na utavunja vipande vipande mataifa mengi.” Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana, utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.
Rise thou, douyter of Sion, and threische, for Y schal putte thin horn of irun, and Y schal putte thi nailis brasun; and thou schalt make lesse, ether waste, many puplis, and schalt sle to the Lord the raueyns of hem, and the strengthe of hem to the Lord of al erthe.

< Mika 4 >