< Mika 3 >

1 Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
Zato rekoh: èujte, poglavice Jakovljeve i knezovi doma Izrailjeva, ne treba li vam znati šta je pravo?
2 ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
Koji mrzite na dobro a ljubite zlo, sadirete kožu s njih i meso s kosti njihovijeh;
3 ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
I jedete meso naroda mojega i sadirete kožu s njih i kosti im prebijate, i sasijecate kao u lonac i kao meso u kotao.
4 Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
Tada æe vikati ka Gospodu, ali ih neæe uslišiti, nego æe sakriti lice svoje od njih u ono vrijeme, kako oni zlo radiše.
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
Ovako veli Gospod za proroke koji zavode moj narod, koji grizu zubima svojim i vièu: mir; i ako im ko ne da ništa u usta, dižu rat na nj.
6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
Zato æe vam utvara biti noæ i proricanje vaše tama; i sunce æe zaæi tijem prorocima i dan æe im se smraèiti.
7 Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
Tada æe se postidjeti vidioci, i vraèari æe se posramiti, i svi æe zastrijeti usne svoje, jer neæe biti odgovora Božijega.
8 Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
Ali ja sam pun sile od duha Gospodnjega, i suda i hrabrosti da kažem Jakovu zloèinstvo njegovo i Izrailju grijeh njegov.
9 Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
Èujte ovo, poglavice doma Jakovljeva i knezovi doma Izrailjeva, koji se gadite na pravdu, i sve što je pravo izvræete;
10 mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
Koji gradite Sion krvlju i Jerusalim bezakonjem.
11 Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
Poglavari njegovi sude po mitu, i sveštenici njegovi uèe za platu, i proroci njegovi gataju za novce, a na Gospoda se oslanjaju govoreæi: nije li Gospod usred nas? neæe doæi zlo na nas.
12 Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.
Zato æe se s vas Sion preorati kao njiva, i Jerusalim æe postati gomila, i gora od doma visoka šuma.

< Mika 3 >