< Mika 3 >
1 Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
Then said I, Hear, I pray you, ye heads of Jacob, and ye judges of the house of Israel, —Is it not yours to know justice?
2 ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
Ye haters of right, and lovers of wrong, —tearing away their skin from off them, and their flesh from off their bones;
3 ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
Who indeed have eaten the flesh of my people, and, their skin from off them, have stript, and, their bones, have they broken in pieces, —and will spread them out, as flesh with a fork, and as flesh, in the midst of a pot.
4 Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
Then, shall they make outcry unto Yahweh, but he will not answer them, —that he may hide his face from them, at that time, even as they have made wicked their doings.
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
Thus, saith Yahweh, concerning the prophets who are leading astray my people, —who bite with their teeth, and then cry—Prosper! and whoso holdeth not to their mouth, they hallow against him a war!
6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
Therefore, shall it be night to you, for lack of vision, and darkness to you, for lack of divination, —and the sun, shall go in, over the prophets, and the day, shall be overcast because of them;
7 Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
And the men of vision, shall turn pale, and the diviners, shall blush, and shall put a covering upon their lip, all of them, —because there is no answer of God.
8 Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
But, in very deed, I, am full of vigour, with the spirit of Yahweh, and of justice and of valour, —to declare to Jacob, his transgression, and to Israel, his sin.
9 Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
Hear this, I pray you, ye heads of the house of Jacob, and ye judges of the house of Israel, —who abhor justice, and, all right, do pervert:
10 mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
Building Zion, with deeds of blood, —and Jerusalem, with perversity.
11 Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
Her heads, for a bribe, pronounce sentence, and, her priests, for a price, give direction, and, her prophets, for silver, divine, —yet, on Yahweh, they lean, saying, Is not, Yahweh, in our midst? there shall not come upon us, calamity.
12 Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.
Wherefore, for your sake, Zion, as a field, shall be ploughed, and, Jerusalem, unto heaps of ruins, shall be turned, —and, the mountain of the house, shall [be] like mounds in a jungle.