< Mika 3 >

1 Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
And I sayd, Heare, I pray you, O heads of Iaakob, and yee princes of the house of Israel: should not ye knowe iudgement?
2 ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
But they hate the good, and loue the euill: they plucke off their skinnes from them, and their flesh from their bones.
3 ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
And they eate also the flesh of my people, and flay off their skinne from them, and they breake their bones, and chop them in pieces, as for the pot, and as flesh within the caldron.
4 Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
Then shall they crye vnto the Lord, but he will not heare them: he wil euen hide his face from them at that time, because they haue done wickedly in their workes.
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
Thus saith the Lord, Concerning the prophets that deceiue my people, and bite them with their teeth, and cry peace, but if a man put not into their mouthes, they prepare warre against him,
6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
Therefore night shalbe vnto you for a vision, and darkenesse shalbe vnto you for a diuination, and the sunne shall goe downe ouer the prophets, and the day shalbe darke ouer them.
7 Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
Then shall the Seers bee ashamed, and the southsayers confounded: yea, they shall all couer their lippes, for they haue none answere of God.
8 Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
Yet notwithstanding I am full of power by the Spirite of the Lord, and of iudgement, and of strength to declare vnto Iaakob his transgression, and to Israel his sinne.
9 Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
Heare this, I pray you, ye heades of the house of Iaakob, and princes of the house of Israel: they abhorre iudgement, and peruert all equitie.
10 mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
They build vp Zion with blood, and Ierusalem with iniquitie.
11 Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
The heads thereof iudge for rewardes, and the Priestes thereof teache for hyre, and the prophets thereof prophecie for money: yet wil they leane vpon the Lord, and say, Is not the Lord among vs? no euill can come vpon vs.
12 Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.
Therefore shall Zion for your sake bee plowed as a field, and Ierusalem shalbe an heape, and the mountaine of the house, as the hye places of the forest.

< Mika 3 >