< Mika 3 >
1 Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
And he shall say, Hear now these words, you heads of the house of Jacob, and you remnant of the house of Israel; is it not for you to know judgement?
2 ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
[who] hate good, and seek evil; [who] tear their skins off them, and their flesh off their bones:
3 ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
even as they devoured the flesh of my people, and stripped their skins off them, and broke their bones, and divided [them] as flesh for the cauldron, and as meat for the pot,
4 Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
thus they shall cry to the Lord, but he shall not listen to them; and he shall turn away his face from them at that time, because they have done wickedly in their practices against themselves.
5 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
Thus says the Lord concerning the prophets that lead my people astray, that bit with their teeth, and proclaim peace to them; and [when] nothing was put into their mouth, they raised up war against them:
6 Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
therefore there shall be night to you instead of a vision, and there shall be to you darkness instead of prophecy; and the sun shall go down upon the prophets, and the day shall be dark upon them.
7 Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
And the seers of night-visions shall be ashamed, and the prophets shall be laughed to scorn: and all the people shall speak against them, because there shall be none to listen to them.
8 Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
Surely I will strengthen myself with the Spirit of the Lord, and of judgement, and of power, to declare to Jacob his transgressions, and to Israel his sins.
9 Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
Hear now these words, you chiefs of the house of Jacob, and the remnant of the house of Israel, who hate judgement, and pervert all righteousness;
10 mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
who build up Sion with blood, and Jerusalem with iniquity.
11 Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
The heads thereof have judged for gifts, and the priests thereof have answered for hire, and her prophets have divined for silver: and [yet] they have rested on the Lord, saying, Is not the Lord amongst us? no evil shall come upon us.
12 Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.
Therefore on your account Sion shall be ploughed as a field, and Jerusalem shall be as a storehouse of fruits, and the mountain of the house as a grove of the forest.