< Mika 2 >
1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Ai daqueles que inventam a iniqüidade e trabalhar o mal em suas camas! Quando a manhã é leve, eles a praticam, porque está no poder de suas mãos.
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
Eles cobiçam os campos e os apreendem, e casas, e depois levá-los embora. Eles oprimem um homem e sua casa, mesmo um homem e sua herança.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
Portanto, diz Yahweh: “Eis que estou planejando contra estas pessoas um desastre, do qual você não removerá seus pescoços, nem você andará altivo, pois é um momento maligno.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
Naquele dia, eles vão fazer uma parábola contra você, e lamentar com uma lamentação triste, dizendo, “Estamos totalmente arruinados! A posse de meu povo está dividida. De fato, ele me tira isso e atribui nossos campos a traidores””.
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
Portanto, você não terá ninguém que divida a terra por lotes na assembléia de Yahweh.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
“Não profetizem!”-eles profetizam- “Não profetize sobre estas coisas”. A vergonha não nos ultrapassará”.
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
Diz-se, ó casa de Jacob, “O Espírito de Yahweh está com raiva? São estes os seus feitos? Minhas palavras não fazem bem àquele que caminha sem culpa”?
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
Mas ultimamente meu povo tem se erguido como inimigo. Você tira o manto e a roupa daqueles que passam sem cuidado, voltando da batalha.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
Você expulsa as mulheres do meu povo de suas agradáveis casas; de seus filhos pequenos você tira a minha bênção para sempre.
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Levante-se, e parta! Pois este não é o seu lugar de descanso, por causa da impureza que destrói, mesmo com uma dolorosa destruição.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
Se um homem que caminha com espírito de falsidade mente, dizendo, “Eu vos profetizarei de vinho e de bebida forte”. ele seria o profeta deste povo.
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
Certamente vou reunir todos vocês, Jacob. Certamente vou recolher o restante de Israel. Vou colocá-los juntos como ovelhas de Bozrah, como um rebanho no meio do seu pasto. Eles irão se aglomerar com pessoas.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
Aquele que quebra o caminho sobe diante deles. Eles rompem o portão, e saem. O rei deles passa diante deles, com Yahweh à sua frente.