< Mika 2 >

1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Malheur à vous, qui songez à l’inutile, et qui inventez le mal sur vos lits; à la lumière du matin ils l’accomplissent, parce que c’est contre Dieu qu’est élevée leur main.
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
Et ils ont convoité des champs, et ils les ont pris violemment; et ils ont usurpé des maisons; et ils opprimaient un homme et sa maison; un autre homme et son héritage.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
C’est pour cela, voici ce que dit le Seigneur: Voici que moi je prépare pour cette famille un malheur dont vous ne retirerez pas vos cous, et vous ne marcherez pas en superbes, parce que c’est un temps très mauvais.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
En ce jour-là, vous serez pris pour un sujet de parabole, et avec un doux plaisir sera chantée la chanson de ceux qui diront: Par la désolation nous avons été ravagés; la portion de mon peuple a été changée; comment se retirera-t-il de moi, puisqu’il reviendra pour partager nos contrées?
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
À cause de cela, il n’y aura personne qui mette le cordeau de partage dans l’assemblée du Seigneur.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
Ne dites point sans cesse: Il ne répandra pas ses oracles sur eux, la confusion ne les couvrira pas.
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
La maison de Jacob dit: Est-ce que l’esprit du Seigneur a été raccourci, ou est-ce que telles sont ses pensées? Mes paroles ne sont-elles pas favorables à celui qui marche dans la droiture?
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
Mais, au contraire, mon peuple s’est levé en adversaire; de dessus la tunique, vous avez enlevé le manteau; et ceux qui passaient de bonne foi, vous les avez tournés à la guerre.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
Vous avez chassé les femmes de mon peuple de la maison de leurs délices; vous avez enlevé ma louange à leurs petits enfants pour jamais.
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Levez-vous, et allez, parce qu’il n’y a point de repos ici pour vous; à cause de son impureté, cette terre sera corrompue d’une putréfaction horrible.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
Plût à Dieu que je fusse un homme n’ayant pas l’esprit prophétique, et que je parlasse plutôt mensonge! je le verserai le vin de la colère de Dieu, et je t’enivrerai; et celui pour qui il sera versé, sera ce peuple.
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
Je te rassemblerai certainement tout entier, ô Jacob; je réunirai les restes d’Israël; je les mettrai tous ensemble comme dans une bergerie, comme un troupeau au milieu de son parc; une multitude d’hommes y causera du tumulte.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
Car celui qui ouvrira le chemin, montera devant eux: ils se partageront, et passeront à la porte et entreront par elle; et leur roi passera en leur présence, et le Seigneur sera à leur tête.

< Mika 2 >