< Mika 2 >

1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Malheur à ceux qui méditent l'iniquité et qui préparent le mal sur leurs couches! au point du jour ils l'exécutent, quand c'est au pouvoir de leurs mains.
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
Ils convoitent les champs et les ravissent, les maisons, et ils s'en emparent; ils font violence à l'homme et à sa maison, au maître et à son héritage.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
C'est pourquoi ainsi parle Yahweh: Voici que je médite contre cette race un mal, dont vous ne pourrez dégager votre cou; et vous ne marcherez plus la tête haute, car ce sera un temps mauvais.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
En ce jour-là on prononcera sur vous un proverbe, et on chantera une complainte: " C'en est fait, dira-t-on, nous sommes entièrement dévastés: il aliène la part de mon peuple! Comment me l'enlève-t-il? Il distribue nos champs aux infidèles? "
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
C'est pourquoi tu n'auras personne qui étende chez toi le cordeau, pour une part d'héritage, dans l'assemblée de Yahweh.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
— Ne prophétisez plus, prophétisent-ils. Si on ne prophétise pas à ceux-ci, l'opprobre ne s'éloignera pas.
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
Toi qu'on nomme maison de Jacob, est-ce que Yahweh est dépourvu de patience? Sont-ce là ses œuvres? — Mes paroles ne sont-elles pas bienveillantes pour celui qui marche avec droiture?
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
Hier mon peuple s'est levé en adversaire: de dessus la robe vous arrachez le manteau; ceux qui passent sans défiance, vous les traitez en ennemis.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
Vous chassez les femmes de mon peuple, de leurs maisons chéries; à leurs petits enfants vous ôtez pour jamais ma gloire!
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Levez-vous! Partez..., car ce pays n'est pas un lieu de repos, à cause de la souillure qui vous tourmentera, et d'un cruel tourment.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
S'il y avait un homme courant après le vent et débitant des mensonges, en disant: " Je vais te prophétiser vin et cervoise! " ce serait le prophète de ce peuple.
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
Je te rassemblerai tout entier, ô Jacob, je recueillerai les restes d'Israël; je les grouperai ensemble comme des brebis dans un bercail; comme un troupeau au milieu de son enclos, ainsi bruira la multitude des hommes.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
Celui qui fait la brèche monte devant eux; ils font la brèche, ils franchissent la porte, et par elle ils sortent; leur roi passe devant eux, et Yahweh est à leur tête.

< Mika 2 >