< Mika 2 >

1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
woe! to devise: devise evil: wickedness and to work bad: evil upon bed their in/on/with light [the] morning to make: do her for there to/for god: power hand their
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
and to desire land: country and to plunder and house: home and to lift: raise and to oppress great man and house: home his and man and inheritance his
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
to/for so thus to say LORD look! I to devise: devise upon [the] family [the] this distress: harm which not to remove from there neck your and not to go: walk haughtily for time distress: harm he/she/it
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
in/on/with day [the] he/she/it to lift: loud upon you proverb and to wail wailing to be to say to ruin to ruin portion people my to change how? to remove to/for me to/for backsliding land: country our to divide
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
to/for so not to be to/for you to throw cord in/on/with allotted in/on/with assembly LORD
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
not to drip/prophesy to drip/prophesy [emph?] not to drip/prophesy to/for these not to remove shame
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
to say house: household Jacob be short spirit: temper LORD if: surely yes these deed his not word my be good with [the] upright to go: walk
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
and previously people my to/for enemy to arise: rise from opposite garment robe to strip [emph?] from to pass security to return: return battle
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
woman people my to drive out: divorce [emph?] from house: home luxury her from upon infant her to take: take glory my to/for forever: enduring
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
to arise: rise and to go: went for not this [the] resting in/on/with for the sake of to defile to destroy and destruction be sick
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
if man: anyone to go: went spirit: breath and deception to lie to drip/prophesy to/for you to/for wine and to/for strong drink and to be to drip/prophesy [the] people [the] this
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
to gather to gather Jacob all you to gather to gather remnant Israel unitedness to set: make him like/as flock enclosure like/as flock in/on/with midst [the] pasture his to make noise from man
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
to ascend: rise [the] to break through to/for face: before their to break through and to pass gate and to come out: come in/on/with him and to pass king their to/for face: before their and LORD in/on/with head: top their

< Mika 2 >