< Mika 2 >

1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Woe [to] those devising iniquity, And working evil on their beds, In the morning light they do it, For their hand is—to God.
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
And they have desired fields, And they have taken violently, And houses, and they have taken away, And have oppressed a man and his house, Even a man and his inheritance.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
Therefore, thus said YHWH: “Behold, I am devising against this family calamity, From which you do not remove your necks, Nor walk loftily, for it [is] a time of evil.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
In that day [one] takes up for you an allegory, And he has wailed a wailing of woe, He has said, We have been utterly spoiled, The portion of my people He changes, How He moves toward me! To the backslider our fields He apportions.
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
Therefore, you have no caster of a line by lot In the assembly of YHWH.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
You do not prophesy—they prophesy, They do not prophesy to these, It does not remove shame.
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
[Those] named the house of Jacob: Has the Spirit of YHWH been shortened? Are these His doings? Do My words not benefit the people that are walking uprightly?
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
And recently My people raise up as an enemy, You strip off the honorable ornament from the outer garment, From the confident passers by, You who are turning back from war.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
The women of My people you cast out from its delightful house, From its sucklings you take away My honor for all time.
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Rise and go, for this [is] not the rest, Because of uncleanness it corrupts, And corruption is powerful.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
If one is going [with] the wind, And [with] falsehood has lied: I prophesy to you of wine, and of strong drink, He has been the prophet of this people!
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
I surely gather you, O Jacob, all of you, I surely bring together the remnant of Israel, Together I set it as the flock of Bozrah, As a drove in the midst of its pasture, It makes a noise because of man.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
The breaker has gone up before them, They have broken through, Indeed, they pass through the gate, Indeed, they go out through it, And their king passes on before them, And YHWH at their head!”

< Mika 2 >