< Mika 2 >

1 Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
Woe to those who devise iniquity and work evil upon their beds! When the morning is light they practice it, because it is in the power of their hand.
2 Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
And they covet fields, and seize them, and houses, and take them away. And they oppress a man and his house, even a man and his heritage.
3 Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
Therefore thus says Jehovah: Behold, I devise an evil against this family, from which ye shall not remove your necks, nor shall ye walk haughtily, for it is an evil time.
4 Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
In that day they shall take up a taunt against you, and lament with a doleful lamentation. And say, We are utterly ruined. He changes the portion of my people. How he removes it from me! He divides our fields to the rebellious.
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
Therefore thou shall have nobody to cast the line by lot in the assembly of Jehovah.
6 Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
Prophesy ye not, they prophesy. They shall not prophesy to these, so reproaches shall not depart.
7 Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
Shall it be said, O house of Jacob, Is the Spirit of Jehovah restricted? Are these his doings? Do not my words do good to him who walks uprightly?
8 Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
But of late my people have risen up as an enemy. Ye strip off the robe with the garment from those who pass by securely as men turning back from war.
9 Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
Ye cast out the women of my people from their pleasant houses. Ye take away my glory from their young sons forever.
10 Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
Arise ye, and depart, for this is not your resting-place, because of uncleanness that destroys, even with a grievous destruction.
11 Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
If a man walking in a spirit of falsehood lies, saying, I will prophesy to thee of wine and of strong drink, he shall even be the prophet of this people.
12 “Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
I will surely assemble, O Jacob, all of thee. I will surely gather the remnant of Israel. I will put them together as the sheep of Bozrah, as a flock in the midst of their pasture. They shall make great noise because of the multitude of men.
13 Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”
The breaker has gone up before them. They have broken forth and passed on to the gate, and have gone out there. And their king has passed on before them, and Jehovah at the head of them.

< Mika 2 >