< Mika 1 >
1 Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
Parole de Dieu qui fut adressée, du temps de Jotham, Achaz, Ezéchias, rois de Juda, à Michée de Moréchet, lequel prophétisa au sujet de Samarie et de Jérusalem:
2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
"Ecoutez, peuples, écoutez tous! Prête ton attention, ô terre, toi et ce que tu renfermes! Que le Seigneur Dieu serve de témoin contre vous, le Seigneur du fond de sa sainte résidence!
3 Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
Oui, voici l’Eternel qui sort de sa demeure, qui descend et foule les hauteurs de la terre.
4 Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
Sous ses pas, les montagnes se liquéfient, lés vallées se crevassent: ainsi la cire fond sous l’action du feu et les eaux se précipitent sur une pente.
5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
Tout cela à cause de l’infidélité de Jacob et des prévarications de la maison d’Israël. A qui imputer l’infidélité de Jacob? N’Est-ce point à Samarie? A qui les hauts-lieux de Juda? N’Est-ce point à Jérusalem?
6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
Aussi ferai-je de Samarie un champ de décombres, un terrain de plantation pour des vignes. Je lancerai ses pierres dans la vallée et mettrai à nu ses fondations.
7 Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
Toutes ses images sculptées seront fracassées, ses présents d’amour consumés par le feu; toutes ses statues, je les réduirai en ruines; car les ayant amassées avec le salaire de la prostitution, elle les verra s’en aller en salaire de prostitution.
8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
C’Est pour cela que je veux donner cours à mes plaintes, à mes lamentations, circuler pieds-nus et sans vêtements, poussant des hurlements lugubres comme les chacals et des cris plaintifs comme les autruches.
9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
Car cuisants sont les maux qui l’ont frappée, ils atteignent même Juda, s’étendent jusqu’à la porte de mon peuple, jusqu’à Jérusalem.
10 Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
Ne le racontez pas à Gath! Evitez de pousser des sanglots! Dans les maisons de Afra, roulez-vous dans la poussière!
11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
Suivez votre chemin, habitants de Chafir, dans une nudité honteuse! Les habitants de Caanân, eux, n’osent pas sortir; le deuil de Bethaêcel vous ôte l’envie d’y séjourner.
12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
Les habitants de Maroth tremblent pour leur bien-être, puisque déjà, de par l’Eternel, le malheur a fondu sur les portes de Jérusalem.
13 Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
Attachez les chars aux coursiers, habitants de Lakhich! Tu fus une source de péché pour la fille de Sion, car c’est bien chez toi que se trouvent les crimes d’Israël.
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
C’Est pourquoi tu diras adieu à Moréchet-Gath; les maisons d’Akhzib sont une déception pour les rois d’Israël.
15 Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
Une fois de plus, habitants de Marêcha, j’amènerai un conquérant contre toi; jusqu’à Adoullam parvient l’élite d’Israël.
16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.
Coupe-toi les cheveux, rase-toi à cause des enfants qui sont tes délices. Rends ta calvitie large comme les ailes de l’aigle, puisqu’ils te quittent pour aller en exil.