< Mika 1 >

1 Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
Parole de Yahweh qui fut adressée à Michée de Moréseth, dans les jours de Joathan, d’Achaz et d’Ézéchias, rois de Juda, dont il eut la vision touchant Samarie et Jérusalem.
2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
Écoutez, vous tous, peuples! Sois attentive, terre, avec ce qui te remplit! Le Seigneur Yahweh va témoigner contre vous, le Seigneur, du palais de sa sainteté!
3 Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
Car voici que Yahweh va sortir de sa demeure; il descendra, il marchera sur les hauteurs de la terre.
4 Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
Les montagnes se fondront sous ses pas, les vallées se fendront, comme la cire devant le feu, comme l’eau versée sur une pente.
5 Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
Tout cela, à cause du crime de Jacob, et à cause des péchés de la maison d’Israël. Quel est le crime de Jacob? n’est-ce pas Samarie? Et quels sont les hauts lieux de Juda? n’est-ce pas Jérusalem?
6 “Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
Je ferai de Samarie un tas de pierres dans un champ, un lieu à planter la vigne; je ferai rouler ses pierres dans la vallée, et je mettrai à nu ses fondements.
7 Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
Toutes ses statues seront brisées; et tous ses salaires consumés par le feu; de toutes ses idoles je ferai une ruine, car elle les a amassées avec le salaire de la prostitution, et elles redeviendront un salaire de prostitution.
8 Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
À cause de cela, je me lamenterai et je hurlerai, je marcherai dépouillé et nu; je répandrai une lamentation comme le chacal, et une plainte comme l’autruche.
9 Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
Car sa plaie est mortelle; car elle vient jusqu’à Juda, elle arrive jusqu’à la porte de mon peuple, jusqu’à Jérusalem.
10 Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
Ne l’annoncez pas dans Geth; ne pleurez pas dans Acco! À Beth-Aphra je me roule dans la poussière.
11 Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
Passe, habitante de Saphir, dans une honteuse nudité! L’habitante de Tsoanan n’est point sortie; le deuil de Beth-Haetsel vous prive de son abri.
12 Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
L’habitante de Maroth est en détresse à cause de ses biens; car le malheur est descendu d’auprès de Yahweh, sur la porte de Jérusalem.
13 Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
Attelle le char au coursier, habitante de Lachis; ce fut le commencement du péché pour la fille de Sion, qu’on ait trouvé chez toi les crimes d’Israël.
14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
C’est pourquoi tu renonceras à posséder Moréseth de Geth; les maisons d’Aczib seront une déception pour les rois d’Israël.
15 Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
Je t’amènerai un conquérant, habitante de Marésa; la noblesse d’Israël s’en ira jusqu’à Odollam.
16 Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.
Arrache tes cheveux, rase-les, à cause de tes enfants bien-aimés; fais-toi chauve comme le vautour, car ils s’en vont en captivité loin de toi!

< Mika 1 >