< Mathayo 1 >

1 Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu:
Généalogie de Jésus-Christ, fils de David, fils d'Abraham.
2 Abrahamu akamzaa Isaki, Isaki akamzaa Yakobo, Yakobo akawazaa Yuda na ndugu zake,
Abraham engendra Isaac; Isaac, Jacob; Jacob, Juda et ses frères;
3 Yuda akawazaa Peresi na Zera, ambao mama yao alikuwa Tamari, Peresi akamzaa Hesroni, Hesroni akamzaa Aramu,
Juda, Phares et Zara, qu'il eut de Thamar; Phares, Esrom; Esrom, Aram;
4 Aramu akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
Aram, Aminabad; Aminabad, Naasson; Naasson, Salmon;
5 Salmoni akamzaa Boazi, na mama yake Boazi alikuwa Rahabu, Boazi akamzaa Obedi, ambaye mama yake alikuwa Ruthu, Obedi akamzaa Yese,
Salmon, Booz, qu'il eut de Rahab; Booz, Jobed, qu'il eut de Ruth;
6 Yese akamzaa Daudi ambaye alikuwa mfalme. Daudi akamzaa Solomoni, ambaye mama yake ni yule aliyekuwa mke wa Uria.
Jobed, Issaï; Issaï, le roi David. David engendra Salomon qu'il eut de la femme d'Urie;
7 Solomoni akamzaa Rehoboamu, Rehoboamu akamzaa Abiya, Abiya akamzaa Asa,
Salomon, Roboam; Roboam, Abia; Abia, Asa;
8 Asa akamzaa Yehoshafati, Yehoshafati akamzaa Yoramu, Yoramu akamzaa Uzia,
Asa, Josaphat; - Josaphat, Joram; Joram, Ozias;
9 Uzia akamzaa Yothamu, Yothamu akamzaa Ahazi, Ahazi akamzaa Hezekia,
Ozias, Joatham; Joatham, Achez; Achez, Ezéchias;
10 Hezekia akamzaa Manase, Manase akamzaa Amoni, Amoni akamzaa Yosia,
Ezéchias, Manassé; Manassé, Amos; Amos, Josias;
11 wakati wa uhamisho wa Babeli, Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake.
Josias, Jéchonias et ses frères, lors de l'émigration à Babylone.
12 Baada ya uhamisho wa Babeli: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli akamzaa Zerubabeli,
Après l'émigration à Babylone, Jéchonias engendra Salathiel; Salathiél, Zorobabel;
13 Zerubabeli akamzaa Abiudi, Abiudi akamzaa Eliakimu, Eliakimu akamzaa Azori,
Zorobabel, Abioud; Abioud, Eliacim; Eliacim, Azor;
14 Azori akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Akimu, Akimu akamzaa Eliudi,
Azor, Sadoc; Sadoc, Achim; Achim, Elioud;
15 Eliudi akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Matani, Matani akamzaa Yakobo,
Elioud, Eléazar; Eléazar, Matthan; Matthan, Jacob;
16 naye Yakobo akamzaa Yosefu ambaye alikuwa mumewe Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
Jacob, Joseph, le mari de Marie, de laquelle naquit Jésus, qu'on appelle Christ.
17 Hivyo, kulikuwepo na jumla ya vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi hadi wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli, na vizazi kumi na vinne tangu wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli hadi Kristo.
Il y a donc, en tout, quatorze générations d'Abraham à David; quatorze, de David à l'émigration à Babylone, et quatorze, de l'émigration jusqu’à Christ.
18 Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria alionekana kuwa na mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Or, voici de quelle manière Jésus-Christ vint au monde. Marie, sa mère, ayant été fiancée à Joseph, se trouva enceinte par l'effet du Saint-Esprit, avant qu'ils eussent habité ensemble.
19 Kwa kuwa Yosefu, mwanaume aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani, aliazimu kumwacha kwa siri.
Joseph, son mari, étant un homme de bien, et ne voulant pas l'exposer à la honte, résolut de la répudier secrètement.
20 Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na kusema, “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Il y pensait, lorsqu'un ange du Seigneur lui apparut en songe, et lui dit: «Joseph, fils de David, ne crains point de prendre chez toi Marie, ta femme; car l'enfant qu'elle a conçu est du Saint-Esprit.
21 Naye atamzaa mwana, nawe utamwita Jina lake Yesu, kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka dhambi zao.”
Elle mettra au monde un fils, et tu lui donneras le nom de Jésus, parce que c'est lui qui sauvera son peuple de ses péchés.»
22 Haya yote yalitukia ili litimie lile Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii, akisema:
Tout cela arriva, afin que s'accomplît ce qu'avait dit le Seigneur par le prophète:
23 “Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli”: maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
«Voici, la vierge sera enceinte; elle mettra au monde un fils à qui l’on donnera le nom d'Emmanuel, » ce qui signifie «Dieu avec nous.»
24 Yosefu alipoamka kutoka usingizini, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake.
A son réveil, Joseph fit comme l'ange du Seigneur le lui avait commandé: il prit sa femme chez lui.
25 Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria alipojifungua mwanawe kifungua mimba akamwita Jina lake Yesu.
Et il ne la connut point, jusqu’à ce qu'elle eût mis au monde un fils, et il lui donna le nom de Jésus.

< Mathayo 1 >