< Mathayo 1 >

1 Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu:
Dawitnat Abrahamn naar wottso Iyesus Krstos shuweyi s'ap'o haniye.
2 Abrahamu akamzaa Isaki, Isaki akamzaa Yakobo, Yakobo akawazaa Yuda na ndugu zake,
Abraham Yisak'i b́shuwi, Yisak' Yak'obi b́shuwi, Yak'ob Yihudnat bí'eshwotsi b́shuwi,
3 Yuda akawazaa Peresi na Zera, ambao mama yao alikuwa Tamari, Peresi akamzaa Hesroni, Hesroni akamzaa Aramu,
Yihudwere Faresnat Zaran Timari eteef máátswatse b́shuwi, Fares Hesroni b́shwi, Hesronwere Arami b́shuwi,
4 Aramu akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
Aramu Aminadabi b́shuwi, Aminadabu Ne'asoni b́shuwi, Ne'asonu Selmoni b́shuwi,
5 Salmoni akamzaa Boazi, na mama yake Boazi alikuwa Rahabu, Boazi akamzaa Obedi, ambaye mama yake alikuwa Ruthu, Obedi akamzaa Yese,
Selmon Boezn Reaabi eteets máátswatse b́shuwi, Boez Iyobedn Ruuti eteef máátswatse b́shuwi, Iyobed Iseyi b́shuwi,
6 Yese akamzaa Daudi ambaye alikuwa mfalme. Daudi akamzaa Solomoni, ambaye mama yake ni yule aliyekuwa mke wa Uria.
Isey Nugúso Dawiti b́shuwi. Nugúso Dawit Oriyo mááts teshtswatse Selemoni b́shuwi,
7 Solomoni akamzaa Rehoboamu, Rehoboamu akamzaa Abiya, Abiya akamzaa Asa,
Selemon Rob'ami b́shuwi, Rob'am Abiyayi b́shuwi, Abiyawere Asafi b́shuwi,
8 Asa akamzaa Yehoshafati, Yehoshafati akamzaa Yoramu, Yoramu akamzaa Uzia,
Asaf Iyosaft'i b́shuwi, Iyosaft' Iyorami b́shuwi, Iyoram Oziyani b́shuwi,
9 Uzia akamzaa Yothamu, Yothamu akamzaa Ahazi, Ahazi akamzaa Hezekia,
Oziyanwere Iyo'atami b́shuwi, Iyo'atam Akazi b́shuwi, Akaz Hzk'iyasi b́shuwi,
10 Hezekia akamzaa Manase, Manase akamzaa Amoni, Amoni akamzaa Yosia,
Hzk'iyas Mnaseyi b́ shuwi, Mnaase Amos'i b́shuwi, Amos' Iyosyasi b́shuwi,
11 wakati wa uhamisho wa Babeli, Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake.
Iyosyas Israe'el ashaasho Babilon maants bo kishodek't damets dúr Ikoniyannat bí'eshwotsi b́shuwi.
12 Baada ya uhamisho wa Babeli: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli akamzaa Zerubabeli,
Bokisho dek't Babiloni dameyakon Ikoniyan Salatiyal b́ shuwi Selatyal Zerubabeli b́ shuwi,
13 Zerubabeli akamzaa Abiudi, Abiudi akamzaa Eliakimu, Eliakimu akamzaa Azori,
Zerubabel Abiyodi b́shuwi, Abiyodu Eelyak'emi b́shwi, Eelyak'em Azori b́ shuwi,
14 Azori akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Akimu, Akimu akamzaa Eliudi,
Azor Sadok'i b́shuwi, Sadok' Akimi b́shuwi, Akim Eelyudi b́shuwi,
15 Eliudi akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Matani, Matani akamzaa Yakobo,
Eeliyud Alazari b́shuwi, Alazar Matani b́shuwi, Matan Yak'obi b́shuwi,
16 naye Yakobo akamzaa Yosefu ambaye alikuwa mumewe Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
Yak'ob Krstosi eteefo Iyesusi shuwtsu Mariyami wid'tso Yosefi b́shuwi.
17 Hivyo, kulikuwepo na jumla ya vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi hadi wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli, na vizazi kumi na vinne tangu wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli hadi Kristo.
Eshe Abrahamatse tuut Dawitats b́borfetso tatse awd gubra, Dawitatse tuut kisho dek't Babilonits dameetsok b́borfetso tatse awd gubra, kisho dek't Babiloni dametsatse tuut waa Krstosok b́borfetso tatse awd gubree.
18 Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria alionekana kuwa na mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Iyesus Krstos b́shwetsok'o hank'oyi b́tesh, b́ índ Mariyam Yosefsh wid'eyat bbefere, bogonkerawon bi S'ayin shayiron maac'at' bdatseyi.
19 Kwa kuwa Yosefu, mwanaume aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani, aliazimu kumwacha kwa siri.
Bin wid'tso Yosef ash kááw b́teshtsotse Maryami ash shinatse kish kitso geeratse, mansh áátson k'azk'ro b́gaw.
20 Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na kusema, “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Ernmó keewan jango shiyanoke b́befere doonzo melakiyo gúmon bí'ats be'eyat hank'o bíet, «Dawit naaro Yosefo! Nwid'tsu Mariyam bmaac'tso S'ayin shayiron b́wottsotse bin nmoo maants dek'osh shatk'aye.
21 Naye atamzaa mwana, nawe utamwita Jina lake Yesu, kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka dhambi zao.”
Biye nungush na'o shwitwaniye, bí ashuwotsi morrotse b́kashitwotse b́shútso Iyesusi etetune.»
22 Haya yote yalitukia ili litimie lile Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii, akisema:
Jaman b́wottsonwere doonzo nebiyiyo weeron b́keewtso b́s'eenetwok'owe,
23 “Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli”: maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
«Hambe, baar na'a s'eenu mac'itwanee, nungush na'onowere shuwitwane, b́ shútsonwere ‹Amanu'eli› err s'eegetwe.» Amanu'eli etonwere «Ik'o nontoniye» etee.
24 Yosefu alipoamka kutoka usingizini, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake.
Yosef tokrotse b́ tuwor, doonzo melakiyo bísh b́keewtsok'on b́ wid'tsu Mariyami b́moomants dek'tbíami.
25 Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria alipojifungua mwanawe kifungua mimba akamwita Jina lake Yesu.
Wotowa eree bna'o bshuufetsosh bin danatse. B́shútsonowere Iyesusi et b́s'eeg.

< Mathayo 1 >