< Mathayo 9 >

1 Yesu akaingia kwenye chombo, akavuka na kufika katika mji wa kwao.
Jeesus astus paati, sõitis teisele poole järve ja läks oma kodulinna.
2 Wakati huo huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelazwa kwenye mkeka. Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, jipe moyo mkuu. Dhambi zako zimesamehewa.”
Seal toodi tema juurde halvatu, kes lamas oma magamisasemel. Nähes nende usku, ütles Jeesus halvatule: „Ole julge, poeg! Sinu patud on sulle andeks antud!“
3 Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa sheria wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”
Siis mõned kirjatundjad mõtlesid endamisi: „See mees teotab Jumalat!“
4 Lakini Yesu akiyafahamu mawazo yao, akawaambia, “Kwa nini mnawaza maovu mioyoni mwenu?
Jeesus aga, teades nende mõtteid, küsis neilt: „Miks te mõtlete kurja oma südames?
5 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
Kumb on kergem, kas öelda „Sinu patud on andeks antud“või „Tõuse üles ja kõnni“?
6 Lakini, ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Ndipo akamwambia yule aliyepooza, “Inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
Aga teadke, et Inimese Pojal on meelevald patte andeks anda maa peal.“Ja ta ütles halvatule: „Tõuse üles, võta oma ase ja mine koju!“
7 Yule mtu akasimama, akaenda nyumbani kwake.
Ning mees tõusis ja läks koju.
8 Makutano walipoyaona haya, wakajawa na hofu ya Mungu, wakamtukuza Mungu ambaye alikuwa ametoa mamlaka kama haya kwa wanadamu.
Seda nähes oli rahvas hämmastuses ja nad ülistasid Jumalat, kes on andnud inimestele sellise meelevalla.
9 Yesu alipokuwa akienda kutoka huko, alimwona mtu mmoja jina lake Mathayo akiwa ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru. Yesu akamwambia, “Nifuate.” Mathayo akaondoka, akamfuata.
Sealt edasi minnes nägi Jeesus meest nimega Matteus maksukoguja pingil istumas ning ütles talle: „Järgne mulle!“Ja ta tõusis ja järgnes talle.
10 Yesu alipokuwa akila chakula ndani ya nyumba ya Mathayo, watoza ushuru wengi na “wenye dhambi” wakaja kula pamoja naye na wanafunzi wake.
Kui siis Jeesus istus lauas tema kodus, tuli sinna palju maksukogujaid ja patuseid ning sõid koos Jeesuse ja tema jüngritega.
11 Mafarisayo walipoona mambo haya, wakawauliza wanafunzi wake, “Kwa nini Mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
Seda nähes küsisid variserid tema jüngritelt: „Miks teie õpetaja sööb koos maksukogujate ja patustega?“
12 Lakini Yesu aliposikia hayo, akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, lakini wale walio wagonjwa ndio wanaohitaji tabibu.
Seda kuuldes ütles Jeesus: „Arsti ei vaja terved, vaid haiged.
13 Nendeni mkajifunze maana ya maneno haya: ‘Nataka rehema, wala si dhabihu.’ Kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
Minge ja õppige, mida tähendab „Ma soovin halastust, mitte ohvrit“. Mina ei ole tulnud kutsuma õigeid, vaid patuseid.“
14 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakaja na kumuuliza Yesu, “Imekuwaje kwamba sisi na Mafarisayo tunafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”
Siis tulid Johannese jüngrid Jeesuse juurde ja küsisid: „Miks meie ja variserid paastume, aga sinu jüngrid ei paastu?“
15 Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kuomboleza wakati angali pamoja nao? Wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.
Jeesus vastas neile: „Ei sobi pulmalistel leinata ajal, kui peigmees on nendega. Ent tuleb aeg, mil peigmees neilt ära võetakse, küll nad siis paastuvad.
16 “Hakuna mtu anayeshonea kiraka kipya kwenye nguo iliyochakaa, kwa maana kile kiraka kitachanika kutoka kwenye hiyo nguo, nayo hiyo nguo itachanika zaidi.
Keegi ei paika vanutamata riidetükiga vana kuube. Säärane paik rebeneks küljest ja käristaks augu veel suuremaks.
17 Wala watu hawaweki divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama wakifanya hivyo, viriba vitapasuka nayo divai itamwagika, navyo viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya, na hivyo divai na viriba huwa salama.”
Samuti ei valata värsket veini vanadesse nahklähkritesse, muidu lähkrid lõhkevad, vein voolab maha ja lähkreid ei saa enam kasutada. Värske vein valatakse uutesse lähkritesse, siis säilivad mõlemad.“
18 Yesu alipokuwa akiwaambia mambo haya, mara akaingia kiongozi wa sinagogi akapiga magoti mbele yake, akamwambia, “Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini njoo uweke mkono wako juu yake, naye atakuwa hai.”
Kui ta seda neile rääkis, tuli tema juurde sünagoogi ülem, põlvitas ta ette ja ütles: „Just praegu suri mu tütar, aga tule, pane oma käsi ta peale, siis ta ärkab ellu!“
19 Yesu akaondoka akafuatana naye, nao wanafunzi wake pia wakaandamana naye.
Jeesus tõusis ja järgnes talle koos oma jüngritega.
20 Wakati huo huo, mwanamke mmoja, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, akaja nyuma ya Yesu, akagusa upindo wa vazi lake,
Ja näe, üks naine, kes oli kannatanud verejooksu juba kaksteist aastat, lähenes Jeesusele selja tagant ja puudutas ta kuue serva,
21 kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikigusa tu vazi lake, nitaponywa.”
öeldes endamisi: „Kui ma võiksin puudutada kasvõi tema kuube, siis ma saaksin terveks!“
22 Yesu akageuka, naye alipomwona akamwambia, “Binti, jipe moyo mkuu, imani yako imekuponya.” Naye yule mwanamke akapona kuanzia saa ile ile.
Jeesus aga pöördus ümber, nägi teda ja ütles: „Ole julge, tütar! Sinu usk on sind terveks teinud!“Ja sellest tunnist alates oli naine terve.
23 Yesu alipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi na kuwaona waombolezaji wakipiga filimbi za maombolezo na watu wengi wakipiga kelele,
Kui nüüd Jeesus jõudis sünagoogi ülema majja ning nägi flöödimängijaid ja häälekat rahvahulka,
24 akawaambia, “Ondokeni! Kwa maana binti huyu hakufa, bali amelala.” Wakamcheka kwa dhihaka.
ütles ta: „Minge ära! Tüdruk ei ole surnud, vaid magab!“Aga nad naersid tema üle.
25 Lakini watu walipokwisha kutolewa nje, akaingia mle ndani na kumshika yule binti mkono, naye akaamka.
Ent kui rahvahulk oli välja aetud, astus Jeesus tuppa, võttis tüdruku käest kinni ja ta ärkas üles.
26 Habari hizi zikaenea katika maeneo yale yote.
Ja kuuldus sellest levis kogu ümbruskonnas.
27 Yesu alipokuwa akiondoka mahali pale, vipofu wawili wakamfuata wakipiga kelele kwa nguvu na kusema, “Mwana wa Daudi, tuhurumie!”
Kui Jeesus läks sealt edasi, järgnesid talle kaks pimedat, kes hüüdsid: „Taaveti Poeg, halasta meie peale!“
28 Alipoingia mle nyumbani wale vipofu wakamjia. Naye Yesu akawauliza, “Mnaamini kwamba ninaweza kufanya jambo hili?” Wakamjibu, “Ndiyo, Bwana.”
Kui Jeesus oli majja astunud, tulid pimedad tema juurde ja ta küsis neilt: „Kas te usute, et ma suudan seda teha?“„Jah, Issand, “vastasid nad talle.
29 Ndipo Yesu akagusa macho yao na kusema, “Iwe kwenu sawasawa na imani yenu.”
Siis Jeesus puudutas nende silmi ja ütles: „Teile sündigu teie usku mööda!“
30 Macho yao yakafunguka. Yesu akawaonya vikali, akisema, “Angalieni mtu yeyote asijue kuhusu jambo hili.”
Ja nende silmad avanesid. Nüüd Jeesus hoiatas neid karmilt: „Vaadake, et keegi sellest teada ei saa!“
31 Lakini wao wakaenda na kueneza habari zake katika eneo lile lote.
Nemad aga läksid ja rääkisid sellest terves ümbruskonnas.
32 Walipokuwa wanatoka, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu na ambaye hakuweza kuongea aliletwa kwa Yesu.
Kui nad olid lahkunud, siis toodi tema juurde tumm mees, kes oli kurjast vaimust vaevatud.
33 Yule pepo mchafu alipotolewa, yule mtu aliyekuwa bubu akaongea. Ule umati wa watu ukastaajabu na kusema, “Jambo kama hili kamwe halijapata kuonekana katika Israeli.”
Jeesus ajas kurja vaimu välja ja tumm hakkas rääkima. „Sellist asja pole Iisraelis veel nähtud!“imestas rahvas.
34 Lakini Mafarisayo wakasema, “Huyo anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa mkuu wa pepo wachafu.”
Variserid aga ütlesid: „Ta ajab kurje vaime välja kurjade vaimude valitseja abil!“
35 Yesu akazunguka katika miji yote na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi.
Ja Jeesus käis läbi kõik linnad ja külad, õpetades sünagoogides, kuulutas evangeeliumi Kuningriigist ning tervendas igasugustest haigustest ja hädadest.
36 Alipoona makutano, aliwahurumia kwa sababu walikuwa wanasumbuka bila msaada, kama kondoo wasiokuwa na mchungaji.
Rahvahulki nähes tundis ta neile kaasa, sest nad olid rõhutud ja räsitud nagu lambad, kellel pole karjast.
37 Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Mavuno ni mengi lakini watendakazi ni wachache.
Siis ta ütles oma jüngritele: „Lõikus on suur, aga töötegijaid on vähe.
38 Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.”
Seepärast paluge lõikuse Issandat, et ta saadaks töötegijaid välja oma lõikusele!“

< Mathayo 9 >