< Mathayo 8 >
1 Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makutano makubwa ya watu yakamfuata.
Kad je Isus sišao s gore, pohrli za njim silan svijet.
2 Mtu mmoja mwenye ukoma akaja na kupiga magoti mbele yake, akasema, “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”
I gle, pristupi neki gubavac, pokloni mu se do zemlje i reče: “Gospodine, ako hoćeš, možeš me očistiti.”
3 Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Mara yule mtu akatakasika ukoma wake.
Isus pruži ruku i dotakne ga se govoreći: “Hoću, očisti se!” I odmah se očisti od gube.
4 Kisha Yesu akamwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote. Lakini nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na utoe sadaka aliyoamuru Mose, ili kuwa ushuhuda kwao.”
Kaže mu Isus: “Pazi, nikomu ne kazuj, nego idi, pokaži se svećeniku i prinesi dar što ga propisa Mojsije, njima za svjedočanstvo.”
5 Yesu alipoingia Kapernaumu, jemadari mmoja alimjia, kumwomba msaada,
Kad uđe u Kafarnaum, pristupi mu satnik pa ga zamoli:
6 akisema, “Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani na amepooza, tena ana maumivu makali ya kutisha.”
“Gospodine, sluga mi leži kod kuće uzet, u strašnim mukama.”
7 Yesu akamwambia, “Nitakuja na kumponya.”
Kaže mu: “Ja ću doći izliječiti ga.”
8 Lakini yule jemadari akamwambia, “Bwana, mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
Odgovori satnik: “Gospodine, nisam dostojan da uđeš pod krov moj, nego samo reci riječ i izliječen će biti sluga moj.
9 Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
Ta i ja, premda sam čovjek pod vlašću, imam pod sobom vojnike pa reknem jednomu: 'Idi!' - i ode, drugomu: 'Dođi!' - i dođe, a sluzi svomu: 'Učini to' - i učini.”
10 Yesu aliposikia maneno haya, alishangaa, akawaambia wale waliomfuata, “Amin, nawaambia, hata katika Israeli sijapata kuona yeyote mwenye imani kubwa namna hii.
Čuvši to, zadivi se Isus i reče onima koji su išli za njim: “Zaista, kažem vam, ni u koga u Izraelu ne nađoh tolike vjere.
11 Ninawaambia kwamba wengi watatoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaki na Yakobo katika Ufalme wa Mbinguni.
A kažem vam: Mnogi će s istoka i zapada doći i sjesti za stol s Abrahamom, Izakom i Jakovom u kraljevstvu nebeskom,
12 Lakini warithi wa Ufalme watatupwa katika giza la nje, ambako kutakuwako kilio na kusaga meno.”
a sinovi će kraljevstva biti izbačeni van u tamu. Ondje će biti plač i škrgut zubi.”
13 Kisha Yesu akamwambia yule jemadari, “Nenda na iwe kwako sawasawa na imani yako.” Naye yule mtumishi akapona saa ile ile.
I reče Isus satniku: “Idi, neka ti bude kako si vjerovao!” I ozdravi sluga u taj čas.
14 Yesu alipoingia nyumbani kwa Petro, alimkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, akiwa ana homa.
Ušavši u kuću Petrovu, Isus ugleda njegovu punicu koja ležaše u ognjici.
15 Akamgusa mkono wake na homa ikamwacha, naye akainuka na kuanza kumhudumia.
Dotače joj se ruke i pusti je ognjica. Ona ustade i posluživaše mu.
16 Jioni ile, wakamletea watu wengi waliopagawa na pepo wachafu, naye akawatoa wale pepo wachafu kwa neno lake, na kuwaponya wagonjwa wote.
A uvečer mu doniješe mnoge opsjednute. On izagna duhove riječju i sve bolesnike ozdravi -
17 Haya yalifanyika ili litimie lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba: “Mwenyewe alitwaa udhaifu wetu na alichukua magonjwa yetu.”
da se ispuni što je rečeno po Izaiji proroku: On slabosti naše uze i boli ponese.
18 Yesu alipoona makutano mengi wamemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake wavuke mpaka ngʼambo ya ziwa.
Kad Isus vidje mnoštvo oko sebe, zapovjedi da se prijeđe prijeko.
19 Kisha mwalimu mmoja wa sheria akamjia Yesu na kumwambia, “Mwalimu, nitakufuata kokote uendako.”
I pristupi jedan pismoznanac te mu reče: “Učitelju, za tobom ću kamo god ti pošao.”
20 Naye Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
Kaže mu Isus: “Lisice imaju jazbine i ptice nebeske gnijezda, a Sin Čovječji nema gdje bi glavu naslonio.”
21 Mwanafunzi mwingine akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
Drugi mu od učenika reče: “Gospodine, dopusti mi da prije odem i pokopam svoga oca.”
22 Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate, uwaache wafu wawazike wafu wao.”
Isus mu kaže: “Hajde za mnom i pusti neka mrtvi pokapaju svoje mrtve.”
23 Naye alipoingia kwenye mashua, wanafunzi wake wakamfuata.
Kad uđe u lađu, pođoše za njim njegovi učenici.
24 Ghafula, kukainuka dhoruba kali baharini hata mashua ikaanza kufunikwa na mawimbi, lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.
I gle, žestok vihor nasta na moru tako da lađu prekrivahu valovi. A on je spavao.
25 Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, tuokoe! Tunazama!”
Oni pristupiše i probudiše ga govoreći: “Gospodine, spasi, pogibosmo!”
26 Naye Yesu akawaambia, “Kwa nini mnaogopa, enyi wa imani haba?” Kisha akaamka na kukemea dhoruba na mawimbi, nako kukawa shwari kabisa.
Kaže im: “Što ste plašljivi, malovjerni?” Tada ustade i zaprijeti vjetrovima i moru te nasta velika utiha.
27 Wale watu wakashangaa, wakisema, “Ni mtu wa namna gani huyu? Hata upepo na mawimbi vinamtii!”
A ljudi su u čudu pitali: “Tko je taj da mu se i vjetrovi i more pokoravaju?”
28 Walipofika ngʼambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili waliopagawa na pepo wachafu walitoka makaburini nao wakakutana naye. Watu hawa walikuwa wakali mno kiasi kwamba hakuna mtu aliyeweza kupita njia ile.
I kada dođe prijeko, u gadarski kraj, eto mu u susret dvaju opsjednutih: izlazili su iz grobnica, silno goropadni, te nitko nije mogao proći onim putem.
29 Wakapiga kelele, “Una nini nasi, Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kututesa kabla ya wakati ulioamriwa?”
I gle, povikaše: “Što ti imaš s nama, Sine Božji? Došao si ovamo prije vremena mučiti nas?”
30 Mbali kidogo kutoka pale walipokuwa, kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha.
A podalje od njih paslo je veliko krdo svinja.
31 Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu, “Ukitutoa humu, turuhusu twende kwenye lile kundi la nguruwe.”
Zlodusi ga zaklinjahu: “Ako nas istjeraš, pošalji nas u ovo krdo svinja.”
32 Akawaambia, “Nendeni!” Hivyo wakatoka na kuwaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremka gengeni kwa kasi, likaingia katika ziwa na kufa ndani ya maji.
On im reče: “Idite!” Oni iziđoše i uđoše u svinje. I gle, sve krdo jurnu niz obronak u more i podavi se u vodama.
33 Wale watu waliokuwa wakiwachunga hao nguruwe wakakimbia wakaingia mjini, wakaeleza yote kuhusu yale yaliyowatokea wale waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu.
A svinjari pobjegoše, odoše u grad te razglasiše sve, napose o opsjednutima.
34 Kisha watu wote wa mji huo wakatoka kwenda kukutana na Yesu. Nao walipomwona wakamsihi aondoke kwenye nchi yao.
I gle, sav grad iziđe u susret Isusu. Kad ga ugledaše, zamole ga da ode iz njihova kraja.