< Mathayo 7 >

1 “Usihukumu ili usije ukahukumiwa.
« Ne jugez pas, afin que vous ne soyez pas jugés.
2 Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.
Car, de quelque jugement que vous jugiez, on vous jugera, et de quelque mesure que vous mesuriez, on vous mesurera.
3 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
Pourquoi vois-tu la tache qui est dans l'œil de ton frère, et ne considères-tu pas la poutre qui est dans ton propre œil?
4 Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe?
Ou comment diras-tu à ton frère: « Laisse-moi enlever la paille de ton œil », et voici que la poutre est dans ton propre œil?
5 Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
Hypocrite! Enlève d'abord la poutre de ton œil, et tu verras ensuite clairement pour enlever la paille de l'œil de ton frère.
6 “Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
« Ne donnez pas aux chiens ce qui est sacré, et ne jetez pas vos perles devant les cochons, de peur qu'ils ne les foulent aux pieds, ne se retournent et ne vous mettent en pièces.
7 “Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
« Demandez, et l'on vous donnera. Cherchez, et vous trouverez. Frappez, et l'on vous ouvrira.
8 Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.
Car quiconque demande reçoit. Celui qui cherche trouve. A celui qui frappe, on ouvrira.
9 “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
Ou bien, qui est parmi vous qui, si son fils lui demande du pain, lui donnera une pierre?
10 Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka?
Ou, s'il demande un poisson, qui lui donnera un serpent?
11 Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
Si donc, méchants comme vous l'êtes, vous savez donner de bonnes choses à vos enfants, à combien plus forte raison votre Père qui est dans les cieux donnera-t-il de bonnes choses à ceux qui les lui demandent.
12 Kwa hiyo chochote mnachotaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii ndiyo Sheria na Manabii.
C'est pourquoi, tout ce que vous voulez que les hommes vous fassent, vous le leur ferez aussi; car c'est là la loi et les prophètes.
13 “Ingieni kupitia mlango mwembamba, kwa maana lango ni pana na njia ni pana ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa kupitia lango hilo.
« Entrez par la porte étroite; car la porte est large, et le chemin est spacieux, qui mène à la perdition, et il y a beaucoup de gens qui entrent par là.
14 Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.
Que la porte est étroite et le chemin resserré qui mène à la vie! Il y en a peu qui la trouvent.
15 “Jihadharini na manabii wa uongo, wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini ndani ni mbwa mwitu wakali.
« Gardez-vous des faux prophètes, qui viennent à vous en habits de brebis, mais qui sont en réalité des loups ravisseurs.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je, watu huchuma zabibu kwenye miiba, au tini kwenye michongoma?
C'est à leurs fruits que vous les reconnaîtrez. Cueillez-vous des raisins sur des épines ou des figues sur des chardons?
17 Vivyo hivyo, mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
De même, tout bon arbre produit de bons fruits, mais l'arbre corrompu produit de mauvais fruits.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
Un bon arbre ne peut pas produire de mauvais fruits, et un arbre corrompu ne peut pas non plus produire de bons fruits.
19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Tout arbre qui ne produit pas de bons fruits est coupé et jeté au feu.
20 Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.
C'est donc à leurs fruits que vous les reconnaîtrez.
21 “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
« Tous ceux qui me disent: « Seigneur, Seigneur » n'entreront pas dans le Royaume des cieux, mais celui qui fait la volonté de mon Père qui est dans les cieux.
22 Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’
En ce jour-là, plusieurs me diront: « Seigneur, Seigneur, n'avons-nous pas prophétisé en ton nom, chassé des démons en ton nom, et fait beaucoup de miracles en ton nom?
23 Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
Alors je leur dirai: « Je ne vous ai jamais connus. Retirez-vous de moi, vous qui commettez l'iniquité ».
24 “Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.
« Quiconque entend ces paroles que je dis et les met en pratique, je le comparerai à un homme sage qui a bâti sa maison sur le roc.
25 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba.
La pluie est tombée, les inondations sont survenues, les vents ont soufflé et ont battu cette maison, mais elle n'est pas tombée, car elle était fondée sur le roc.
26 Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga.
Quiconque entend ces paroles que je dis et ne les met pas en pratique est semblable à un homme insensé qui a bâti sa maison sur le sable.
27 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”
La pluie est tombée, les inondations sont arrivées, les vents ont soufflé et frappé cette maison, et elle est tombée, et sa chute a été grande. »
28 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,
Lorsque Jésus eut achevé de dire ces choses, la foule fut frappée de son enseignement,
29 kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.
car il les enseignait avec autorité, et non comme les scribes.

< Mathayo 7 >