< Mathayo 7 >
1 “Usihukumu ili usije ukahukumiwa.
"Do not judge, so that you won't be judged.
2 Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.
For with whatever judgment you judge, you will be judged; and with whatever measure you measure, it will be measured to you.
3 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
And why do you see the speck that is in your brother's eye, but do not notice the log that is in your own eye?
4 Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe?
Or how will you tell your brother, 'Let me remove the speck from your eye;' and look, the log is in your own eye?
5 Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
You hypocrite. First remove the log out of your own eye, and then you can see clearly to remove the speck out of your brother's eye.
6 “Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
"Do not give that which is holy to the dogs, neither throw your pearls before the pigs, or they will trample them under their feet and turn and tear you to pieces.
7 “Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
"Ask, and it will be given to you. Seek, and you will find. Knock, and it will be opened for you.
8 Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.
For everyone who asks receives. He who seeks finds. To him who knocks it will be opened.
9 “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
Or who is there among you, who, if his son will ask him for bread, will give him a stone?
10 Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka?
Or if he will ask for a fish, who will give him a serpent?
11 Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
If you then, being evil, know how to give good gifts to your children, how much more will your Father who is in heaven give good things to those who ask him.
12 Kwa hiyo chochote mnachotaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii ndiyo Sheria na Manabii.
Therefore whatever you desire for people to do to you, so also you should do to them; for this is the Law and the Prophets.
13 “Ingieni kupitia mlango mwembamba, kwa maana lango ni pana na njia ni pana ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa kupitia lango hilo.
"Enter in by the narrow gate; for wide is the gate and broad is the way that leads to destruction, and many are those who enter in by it.
14 Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.
How narrow is the gate, and difficult is the way that leads to life. Few are those who find it.
15 “Jihadharini na manabii wa uongo, wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini ndani ni mbwa mwitu wakali.
"Beware of false prophets, who come to you in sheep's clothing, but inwardly are ravening wolves.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je, watu huchuma zabibu kwenye miiba, au tini kwenye michongoma?
By their fruits you will know them. Do you gather grapes from thorns, or figs from thistles?
17 Vivyo hivyo, mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
Even so, every good tree produces good fruit; but the corrupt tree produces evil fruit.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
A good tree cannot produce evil fruit, neither can a corrupt tree produce good fruit.
19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Every tree that does not grow good fruit is cut down, and thrown into the fire.
20 Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.
Therefore, by their fruits you will know them.
21 “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Not everyone who says to me, 'Lord, Lord,' will enter into the kingdom of heaven; but he who does the will of my Father who is in heaven.
22 Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’
Many will tell me in that day, 'Lord, Lord, did not we prophesy in your name, in your name cast out demons, and in your name do many mighty works?'
23 Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
And then I will tell them, 'I never knew you. Depart from me, you who practice lawlessness.'
24 “Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.
"Everyone therefore who hears these words of mine, and does them, will be compared to a wise man, who built his house on a rock.
25 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba.
And the rain came down, the floods came, and the winds blew, and beat on that house; and it did not fall, for it was founded on the rock.
26 Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga.
And everyone who hears these words of mine, and does not do them will be like a foolish man, who built his house on the sand.
27 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”
And the rain came down, the floods came, and the winds blew, and beat on that house; and it fell—and great was its fall."
28 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,
And it happened, when Jesus had finished saying these things, that the crowds were astonished at his teaching,
29 kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.
for he taught them with authority, and not like their scribes.