< Mathayo 7 >
1 “Usihukumu ili usije ukahukumiwa.
"Judge not, that you may be judged, yourselves;
2 Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.
"for with what judgment you judge, you will be judged, and in what measure you measure, others will measure to you.
3 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
"And why do you look at the mote in your brother’s eye, and fail to notice the beam which is in your own eye?
4 Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe?
"Or how will you say to your brother, ‘Permit me to remove the mote from your eye,’ when, behold, the beam is in your own eye?
5 Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
"Hypocrite! First cast out the beam from your own eye, and then you will see clearly how to cast the mote out of your brother’s eye.
6 “Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
"Do not give what is holy to the dogs, nor cast your pearls before swine; lest in turn they trample them under their feet, and then turn and attack you.
7 “Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
"Ask, and it will be given you; seek, and you will find; knock, and the door will be opened to you.
8 Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.
"For every one who asks receives, and he who seeks finds, and to him who knocks the door is opened.
9 “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
"What man of you is there who, when his son asks a loaf, will give him a stone?
10 Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka?
"or if his son asks for a fish, will offer him a snake?
11 Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
"If you then, evil as you are, know how to give good gifts to your children, how much more will your heavenly Father give good gifts to those who ask him?
12 Kwa hiyo chochote mnachotaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii ndiyo Sheria na Manabii.
"Therefore everything that you would have men do to you, do you also the same to them; for this is the Law and the Prophets.
13 “Ingieni kupitia mlango mwembamba, kwa maana lango ni pana na njia ni pana ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa kupitia lango hilo.
"Enter by the narrow gate; for broad is the gate and wide the road that leads to destruction, and many are they who go in by it;
14 Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.
"but the gate is narrow and the road is steep, which leads to life, and they are few who find it.
15 “Jihadharini na manabii wa uongo, wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini ndani ni mbwa mwitu wakali.
"Beware of the false prophets who come to you in sheep’s clothing, but within they are ravening wolves.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je, watu huchuma zabibu kwenye miiba, au tini kwenye michongoma?
"By their fruits you will know them. Are grapes gathered of thorns, or figs of thistles?
17 Vivyo hivyo, mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
"No, every good tree bears good fruit, but a worthless tree bears bad fruit.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
"A good tree cannot bear bad fruit; neither can a worthless tree bear good fruit.
19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
"Every tree which does not bear good fruit is cut down and cast into the fire.
20 Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.
"Hence it is by their fruit you will know them.
21 “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
"Not everyone who says to me, ‘Lord, Lord,’ will enter into the kingdom of heaven, but he who does the will of my Father who is in heaven.
22 Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’
"Many in that day will say to me, "‘Lord, Lord, have we not prophesied in your name, and in your name cast out demons, and in your name done many mighty works?’
23 Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
"Then I will tell them plainly, "‘I never knew you; depart from me, you workers of iniquity.’
24 “Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.
"Every one who hears my words and does them I will liken to a wise man who built his house upon the rock.
25 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba.
"And the rain descended, and the floods came, and the winds blew, and beat upon the house, but it fell not, for it was founded upon the rock.
26 Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga.
"And every one who hears these words of mine and does them not, I will liken to a foolish man, who built his house upon the sand.
27 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”
"And the rain descended, and the floods came, and the winds blew, and beat upon that house, and it fell, and great was the fall of it."
28 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,
Now when Jesus had finished his discourse, the crowds were astounded at his teaching,
29 kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.
for he was teaching them as one having authority, and not as their scribes taught them.