< Mathayo 7 >

1 “Usihukumu ili usije ukahukumiwa.
Judge not, that ye be not iudged.
2 Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.
Eor with what iudgement ye iudge, ye shall be iudged, and with what measure ye mete, it shall be measured to you againe.
3 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
And why seest thou the mote, that is in thy brothers eye, and perceiuest not the beame that is in thine owne eye?
4 Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe?
Or howe sayest thou to thy brother, Suffer me to cast out the mote out of thine eye, and beholde, a beame is in thine owne eye?
5 Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
Hypocrite, first cast out that beame out of thine owne eye, and then shalt thou see clearely to cast out the mote out of thy brothers eye.
6 “Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
Giue ye not that which is holy, to dogges, neither cast ye your pearles before swine, lest they treade them vnder their feete, and turning againe, all to rent you.
7 “Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
Aske, and it shall be giuen you: seeke, and ye shall finde: knocke, and it shall be opened vnto you.
8 Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.
For whosoeuer asketh, receiueth: and he, that seeketh, findeth: and to him that knocketh, it shall be opened.
9 “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
For what man is there among you, which if his sonne aske him bread, woulde giue him a stone?
10 Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka?
Or if he aske fish, wil he giue him a serpent?
11 Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
If ye then, which are euill, can giue to your children good giftes, howe much more shall your Father which is in heauen, giue good thinges to them that aske him?
12 Kwa hiyo chochote mnachotaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii ndiyo Sheria na Manabii.
Therefore whatsoeuer ye woulde that men should doe to you, euen so doe ye to them: for this is the Lawe and the Prophets.
13 “Ingieni kupitia mlango mwembamba, kwa maana lango ni pana na njia ni pana ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa kupitia lango hilo.
Enter in at the streight gate: for it is the wide gate, and broade way that leadeth to destruction: and many there be which goe in thereat,
14 Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.
Because the gate is streight, and the way narowe that leadeth vnto life, and fewe there be that finde it.
15 “Jihadharini na manabii wa uongo, wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini ndani ni mbwa mwitu wakali.
Beware of false prophets, which come to you, in sheepes clothing, but inwardly they are rauening wolues.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je, watu huchuma zabibu kwenye miiba, au tini kwenye michongoma?
Ye shall know them by their fruites. Doe men gather grapes of thornes? or figges of thistles?
17 Vivyo hivyo, mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
So euery good tree bringeth foorth good fruite, and a corrupt tree bringeth forth euill fruite.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
A good tree can not bring forth euil fruite: neither can a corrupt tree bring forth good fruite.
19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Euery tree that bringeth not forth good fruite, is hewen downe, and cast into the fire.
20 Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.
Therefore by their fruites ye shall knowe them.
21 “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Not euery one that sayeth vnto me, Lord, Lord, shall enter into the kingdome of heauen, but he that doeth my Fathers will which is in heauen.
22 Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’
Many will say to me in that day, Lord, Lord, haue we not by thy Name prophecied? and by thy name cast out deuils? and by thy name done many great workes?
23 Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
And then will I professe to them, I neuer knewe you: depart from me, ye that worke iniquitie.
24 “Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.
Whosoeuer then heareth of mee these words, and doeth the same, I will liken him to a wise man, which hath builded his house on a rock:
25 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba.
And the raine fell, and the floods came, and the windes blewe, and beat vpon that house, and it fell not: for it was grounded on a rocke.
26 Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga.
But whosoeuer heareth these my wordes, and doeth them not, shall be likened vnto a foolish man, which hath builded his house vpon the sand:
27 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”
And the raine fell, and the floods came, and the windes blewe, and beat vpon that house, and it fell, and the fall thereof was great.
28 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,
And it came to passe, when Iesus had ended these wordes, the people were astonied at his doctrine.
29 kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.
For he taught them as one hauing authoritie, and not as the Scribes.

< Mathayo 7 >