< Mathayo 6 >

1 “Angalieni msitende wema wenu mbele ya watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni.
Uyenyaje ungandi abhombe imbo inyinza hubhantu ili huyilolesye, subhapate ifaida hwa Dada uwahumwanya.
2 “Hivyo mnapowapa wahitaji, msipige panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na watu. Amin nawaambia wao wamekwisha kupokea thawabu yao.
Ishi nufumya isadaka usahayitufye sana usahabhe ndeshe abhanafiki shebhabhomba mumasinagogi na mumitaa, nkaabhantu bhabhatime semubhapae ifaida nkiimo.
3 Lakini ninyi mtoapo sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa kushoto usijue mkono wako wa kuume unachofanya,
Lelo awe lufumya ukhona gwaho ugwa humongo gusahamanye sheshibhombeha hundilo,
4 ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo Baba yako wa mbinguni, yeye aonaye sirini atakupa thawabu kwa wazi.
ili huje isadaka yaho ufumye hu siri. Nkhu Udada waho yalola muhati abhalupele ithawabu yaho.
5 “Nanyi msalipo, msiwe kama wanafiki, maana wao hupenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kando ya barabara ili waonekane na watu. Amin nawaambia, wao wamekwisha kupata thawabu yao.
Na luputa usahabhe, udeshe anafiki, pipo abhene bhasungwa ahwimilile na pute, mumasinagogi na mukona izya mukhaya zyabho nka abhantu bha bhenye. Lelo ihumbabhuzya bhapite ithawabu yabho.
6 Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye sirini atakupa thawabu yako.
Awe luputa injila hu hati ufunje ulwiji upuute hwa Daada uwamumwoyo udaada ya lola muhati asipele ithawabu yaho.
7 Nanyi mnaposali msiseme maneno kama wafanyavyo watu wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa maneno yao.
Nu puta ungandi pyanile inongwa zyesezili ni maana, ndeshe abhamunsi shebhabhomba pipo bhasibha abhantu bhabhahubhiuvwe pipo bhayanga inongwa inyinji.
8 Msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla hamjamwomba.
Ishi usahabhe ndeshe abhene pipo uDada aminye uhwanza henu shusile alabhe hukwakwe.
9 “Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba: “‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe.
Uputaje ishi: Dada witu uwahumwanya itawa lyaho lyimishilwaje.
10 Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
Ubhumwini waho winze, ulugano lwaho lubhombeshe pansi na humwanya.
11 Utupatie riziki yetu ya kila siku.
Utipele ishalye shitu insiku zyonti.
12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyokwisha kuwasamehe wadeni wetu.
Utukhobhoshele amalando gitu, ndeati shetihubhakhobhoshela abhimalando bhitu.
13 Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu [kwa kuwa Ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amen].’
Usahatipe injelo, utidime nu setano.
14 Kwa kuwa kama mkiwasamehe watu wengine wanapowakosea, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
Nkemwabhakhobhoshela abhantu amalando gabho, Udada winyu uwahumwanya abhahubhakhobhoshele namwi.
15 Lakini msipowasamehe watu wengine makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
Nkushe mubhabhakhobhoshele abhantu Udada abhabhakhobhoshele makosa ginyu.
16 “Mnapofunga, msiwe wenye huzuni kama wafanyavyo wanafiki. Maana wao hukunja nyuso zao ili kuwaonyesha wengine kwamba wamefunga. Amin, amin nawaambia wao wamekwisha kupata thawabu yao kamilifu.
Hu gonti, lufunga usahalolesye uzugunizu humaso ndeshe abhanafiki shebhabhomba bhazugumila humiso nke abhantu bhamanye aje bhafunjile. Lyooli ihubhuzya bhapite ithawabu yabho.
17 Lakini mnapofunga, jipakeni mafuta kichwani na kunawa nyuso zenu
Lelo, lufunga pahala amafuta hwitwe lyaho uyoje hunaso.
18 ili kufunga kwenu kusionekane na watu wengine ila Baba yenu aketiye mahali pa siri; naye Baba yenu aonaye sirini atawapa thawabu yenu kwa wazi.
Subhaloleshe humaso gabhantu aje ufunjile, u Ngulubhi mweene yabhamanye Udada yamanya muhati abhahupele ithawabu yaho.
19 “Msijiwekee hazina duniani, mahali ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi huvunja na kuiba.
Usahabhishe amali gaho munsi umu zinanjiha na bhole na bhibha bhahwibha.
20 Lakini jiwekeeni hazina mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba.
Badala yakwe, abhishe amali gaho hwa Ngulubhi, sibhahwibha, sigabhola wa segananjiha.
21 Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo pia moyo wako utakapokuwa.
Pipo amali gaho pegali umwoyo waho pebhubhabhe.
22 “Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni nyofu, mwili wako wote utajaa nuru.
Ilinso lukhozyo lwi bili. Nkushele, ilyinso lyaho lyumi ubili wonti, bhubhabhe nulukhozyo.
23 Lakini kama jicho lako ni ovu, mwili wako wote utajawa na giza. Kwa hiyo basi, kama nuru iliyomo ndani yako ni giza, hilo ni giza kuu namna gani!
Nkushele ilyinso lyaho lifwiye, ubili waho wonti bhuli hisi haani. Ishi nkulukhozyo lweluli muhati muliwe hisi ahagosi ndeshe bhuli!
24 “Hakuna mtu awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.
Numo nka weka yangabha na lume bha bhili, pipo abhahunvitwe unu na hugane uwinji lumo abhahwepe hwunu abhahu sufye uwinji. Hamuwezi kumtumikia Mungu na mali.
25 “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini au mtakunywa nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini. Je, maisha si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
Ishi ihuhabhe nu sanje ahusu amaisha gaho aje ubhalyeshi, ubhamweleshi, ahusu ubili waho ubhakwate shi! Amaisha se haani yi shalye ubili haani yi meenda?
26 Waangalieni ndege wa angani; wao hawapandi wala hawavuni au kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani zaidi kuliko hao ndege?
Enya inyonyi zyezipuluha humwanya. Saazitota sazivunza sazibhunganya na bhishe mushanka, lelo Udada uwahumwanya ahuzilisya. Je amwisemulibhi maana hani kuliko inyonyi?
27 Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
Weemu hulimwe uwahuyitamye ankayonjezya idhiraa yeka huwomi wimaisha gakwe?
28 “Nanyi kwa nini mnajitaabisha kwa ajili ya mavazi? Fikirini maua ya shambani yameavyo. Hayafanyi kazi wala hayafumi.
Ye enu mubha musaga aje yibhakwate nshi? Msubhilile amaua mmashamba shegabha segabhomba imbombo segahuyikwatizya.
29 Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
Bado ihumbabhuzya hata yu Sulemani nu tuntumu wakwe saga ahakwatiziwilwe mojawapo yiga.
30 Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo na kesho yanatupwa motoni, je, hatawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba?
Nkushele Ungulubhi ahugakwatizya amasole agamumagunda, gegakhala isiku lyeka ni ndabhi gatagwa mumwoto je bhulibhuli angabhakwatizya amwi mwemuli nulwitiho uludodo?
31 Kwa hiyo msiwe na wasiwasi, mkisema, ‘Tutakula nini?’ au ‘Tutakunywa nini?’ au ‘Tutavaa nini?’
Eshi musahasaje aje, 'Je tibhalyeshi?' au “Je tibhamweleshi?” au “Je tibhakhwate menda bhuli?”
32 Watu wasiomjua Mungu ndio wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa mbinguni anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
Pipo abhinsi bhahuganza amambo iga, nu Dada winyu uwahumwanya aminye aje muhuganza igo.
33 Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, na haya yote atawapa pia.
Ishi nasuti mwanze ubhumwini wakwe ni lyoli yakwe nigo gonta gabhahwonjeleshe huliwe.
34 Kwa hiyo msiwe na wasiwasi kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.
Ishi usahalole usahasaje kwa ajili yi ndabhi, pipo indabhi zibhamanyishe hunuhwo. Isiku lyolyonti likwiliye hwi tatizizo lyakwe.

< Mathayo 6 >