< Mathayo 4 >
1 Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
Male Jisua hah Diabol methêma a om rangin Ratha'n ramchâra a tuong zoi.
2 Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
Sûn sômminli jân sômminli sâk sâkloiin a om suolechu Jisua hah a vonchâm zoia.
3 Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
Hanchu Diabol a honga, a kôm, “Pathien Nâipasal ni nîn chu, hi lungngei hih vâipôl chang rangin chongpêk roh,” a tia.
4 Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
Hannirese, Jisua'n a kôm han, “Pathien Lekhabu'n Miriem hi vâipôl korongin ring no nia, Pathien bâia chong hongsuokin kêng an a ring rang ani,” tiin a thuona.
5 Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
Hanchu Diabol'n Jisua hah, Khopuilien Inthieng Jerusalema a tuonga, Biekin sîpinsângtaka a mindinga,
6 akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
male a kôm, “Pathien Nâipasal ni nîn chu nangma nethenin inchôm inla, Pathien Lekhabu'n ati anghan: ‘Nu chungroia chu Pathien'n a vântîrtonngei chongpêk ngei a ta; an kutngei leh nang lei modong an tih, masikin ne kengei luo khom lunga nên sûi loina rangin,’” a tia.
7 Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
Jisua'n a kôm, “Aniatachu Pathien Lekhabu'n, Pumapa na Pathien minsin no roh, ti khom ânziek sa,” tiin a thuona.
8 Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
Male, Diabol hah muol insângtaka a tuonga rammuola rêngramngei murdi le an roiinpuinangei a min mua.
9 kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
A kôm, “khûkinbilin chubai mi ni mûkin chu hi ngei murdi hih nang pêk let ki tih,” a ti pea.
10 Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
Male Jisua'n a kôm, “Soitan, rotpai roh! Pathien Lekhabu'n, ‘Pumapa na Pathien vai chubaimûk inla, ama sin vai tho roh a ti!’” tiin a thuona.
11 Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
Masuole chu Diabol'n Jisua a mâka; male vântîrtonngei an juonga, ama an juong san zoi.
12 Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
Jisua'n, John an sûr ti a riet lechu, Galilee rama a thengpata.
13 Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
Nazareth a mâka, Capernaum khopuia ava om zoia, mahah Galilee Dîl pang Zebulun le Naphtali ramhuola om ani.
14 ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
Mahi dêipu Isaiah lei ti hah ahongtung adikna ranga ani:
15 “Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
“Zebulun ram le Naphtali ram, tuipui panna lampuia, Jordan râl kângkhat tieng, Galilee, Jentailngei ram!
16 watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
Ijîng nuoia om mingei han vâr roiinpuitak mûng an ta. Thina ram ijîng nuoia omngei chunga han vâr hah hong êl atih.”
17 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
Ma zora renga hah Jisua'n, “Nin nunsienangei renga inhei ta roi, Invân Rêngram hih anâi zoi sikin!” tiin thurchi misîr a phut kelen zoi.
18 Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
Jisua'n Galilee dîl pang rûla a chai anghan ngasûrpungei lâibungsa inik a mu ngeia, Simon (Peter an ti) le anâipa Andrew, dîla lên leh nga an sûra.
19 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
Jisua'n an kôm, “Ko kôm hong ungla, miriem sûrna chang nangni minchu ki tih,” a tipe ngeia.
20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
Voikhat rengin an lênngei an mâkraka, an jûi kelen zoi.
21 Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
Ava se nôk uol vietin chu lâibungsa adang, Zebedee nâipasalngei Jacob le John ava mu ngei nôka. Anni ngei hah an pa Zebedee leh an rukuong sûnga an lei oma, an lênngei an lei sina. Jisua'n a koi ngeia,
22 Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
male voikhat rengin rukuong le an pa mâkrakin, an jûi kelen zoi.
23 Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
Jisua'n Galilee ram pumpuia a sea, synagog in sûng ngeia a minchua, Rêngram Thurchi Sa a misira, mingei lâia natna le damloina jât tamtak a mindama.
24 Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
Ama chungroi hah Syria ram pumpuia ânthang zoia, masikin mingei han damloi murdi, natna jât tamtak le intaknangei renga an hong tuong ngeia: ramkhori sûrngei, risangol inveingei, phalkhatthi ngei, hah Jisua'n a lei mindam ngei pak ani.
25 Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.
Galilee ram le Khopui Sôm ngei renga, Jerusalem renga, Judea ram renga le Jordan râla ramngei renga mipui tamtak ama an jûi zoi ani.