< Mathayo 4 >
1 Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
Then Yeshua was led up by the Spirit into the wilderness to be tempted by the devil.
2 Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
When he had fasted forty days and forty nights, he was hungry afterward.
3 Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
The tempter came and said to him, “If you are the Son of God, command that these stones become bread.”
4 Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
But he answered, “It is written, ‘Man shall not live by bread alone, but by every word that proceeds out of God’s mouth.’”
5 Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
Then the devil took him into the holy city. He set him on the pinnacle of the temple,
6 akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
and said to him, “If you are the Son of God, throw yourself down, for it is written, ‘He will command his angels concerning you,’ and, ‘On their hands they will bear you up, so that you don’t dash your foot against a stone.’”
7 Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
Yeshua said to him, “Again, it is written, ‘You shall not test the Lord, your God.’”
8 Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
Again, the devil took him to an exceedingly high mountain, and showed him all the kingdoms of the world and their glory.
9 kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
He said to him, “I will give you all of these things, if you will fall down and worship me.”
10 Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
Then Yeshua said to him, “Get behind me, Satan! For it is written, ‘You shall worship the Lord your God, and you shall serve him only.’”
11 Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
Then the devil left him, and behold, angels came and served him.
12 Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
Now when Yeshua heard that Yochanan was delivered up, he withdrew into Galilee.
13 Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
Leaving Nazareth, he came and lived in Capernaum, which is by the sea, in the region of Zebulun and Naphtali,
14 ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
that it might be fulfilled which was spoken through Isaiah the prophet, saying,
15 “Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
“The land of Zebulun and the land of Naphtali, toward the sea, beyond the Jordan, Galilee of the Gentiles,
16 watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
the people who sat in darkness saw a great light; to those who sat in the region and shadow of death, to them light has dawned.”
17 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
From that time, Yeshua began to proclaim, and to say, “Repent! For the Kingdom of Heaven is at hand.”
18 Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
Walking by the sea of Galilee, he saw two brothers: Simon, who is called Peter, and Andrew, his brother, casting a net into the sea; for they were fishermen.
19 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
He said to them, “Come after me, and I will make you fishers for men.”
20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
They immediately left their nets and followed him.
21 Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
Going on from there, he saw two other brothers, Jacob the son of Zebedee, and Yochanan his brother, in the boat with Zebedee their father, mending their nets. He called them.
22 Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
They immediately left the boat and their father, and followed him.
23 Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
Yeshua went about in all Galilee, teaching in their synagogues, proclaiming the Good News of the Kingdom, and healing every disease and every sickness among the people.
24 Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
The report about him went out into all Syria. They brought to him all who were sick, afflicted with various diseases and torments, possessed with demons, epileptics, and paralytics; and he healed them.
25 Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.
Great multitudes from Galilee, Decapolis, Jerusalem, Judea, and from beyond the Jordan followed him.