< Mathayo 4 >

1 Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
Then Jesus was led up into the wilderness by the Spirit to be tempted by the devil.
2 Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
And, after he had fasted for forty days and forty nights, he became hungry.
3 Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
The Tempter came to him, and said: “If you are God’s Son, tell these stones to become loaves of bread.”
4 Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
But Jesus answered, “Scripture says – ‘It is not on bread alone that a person is to live, but on every word that comes from the mouth of God.’”
5 Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
Then the devil took him to the Holy City, and, placing him on the parapet of the temple, said to him,
6 akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
“If you are God’s Son, throw yourself down, for scripture says – ‘He will give his angels commands about you, and on their hands they will lift you up, so you do not even strike your foot against a stone.’”
7 Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
“Scripture also says,” answered Jesus, “‘You must not tempt the Lord your God.’”
8 Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
The third time, the devil took Jesus to a very high mountain, and, showing him all the kingdoms of the world and their splendor, said to him:
9 kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
“All these I will give you, if you will fall at my feet and worship me.”
10 Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
Then Jesus said to him, “Go away, Satan! For scripture says – ‘You must worship the Lord your God, and worship him only.’”
11 Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
Then the devil left him alone, and angels came and helped him.
12 Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
When Jesus heard that John had been arrested, he returned to Galilee.
13 Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
Afterward, leaving Nazareth, he went and settled at Capernaum, which is by the side of the sea, within the borders of Zebulun and Naphtali;
14 ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
in fulfillment of these words in the prophet Isaiah –
15 “Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
‘The land of Zebulun and the land of Naphtali, the land of the Road by the sea, and beyond the Jordan, with Galilee of the Gentiles –
16 watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
The people who were living in darkness have seen a great light, and, for those who were living in the shadow-land of death, a light has dawned!’
17 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
At that time Jesus began to proclaim – “Repent, for the kingdom of heaven is at hand.”
18 Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
As Jesus was walking along the shore of the Sea of Galilee, he saw two brothers – Simon, also known as Peter, and his brother Andrew – casting a net into the sea; for they were fishermen.
19 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
“Come and follow me,” Jesus said, “and I will teach you to fish for people.”
20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
The two men left their nets at once and followed him.
21 Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
Going further on, he saw two other men who were also brothers, James, Zebedee’s son, and his brother John, in their boat with their father, mending their nets. Jesus called them,
22 Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
and they at once left their boat and their father, and followed him.
23 Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
Jesus went all through Galilee, teaching in their synagogues, proclaiming the good news of the kingdom, and curing every kind of disease and every kind of sickness among the people;
24 Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
and his fame spread all through Syria. They brought to him all who were ill with any form of disease, or who were suffering pain – any who were either possessed by demons, or were lunatic, or paralyzed; and he cured them.
25 Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.
He was followed by large crowds from Galilee, the district of the Ten Towns, Jerusalem, Judea, and from beyond the Jordan.

< Mathayo 4 >