< Mathayo 3 >
1 Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Uyahudi, akisema,
Or, en ces jours-là, vint Jean-Baptiste prêchant dans le désert de Judée,
2 “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
Et disant: Faites pénitence, car le royaume des cieux approche.
3 Huyu ndiye yule aliyenenwa habari zake na nabii Isaya aliposema: “Sauti ya mtu aliaye huko nyikani, ‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
C’est lui dont a parlé le prophète Isaïe, disant: Voix de quelqu’un qui crie dans le désert: Préparez la voie du Seigneur faites droits ses sentiers.
4 Basi Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia, akiwa na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
Or Jean avait un vêtement de poils de chameau et une ceinture de cuir autour de ses reins; et sa nourriture était des sauterelles et du miel sauvage.
5 Watu walikuwa wakimwendea kutoka Yerusalemu, Uyahudi yote na nchi zote za kandokando ya Mto Yordani.
Alors accourait à lui Jérusalem, toute la Judée et tout le pays autour du Jourdain;
6 Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
Et ils étaient baptisés par lui dans le Jourdain, confessant leurs péchés.
7 Lakini alipowaona Mafarisayo na Masadukayo wengi wakija ili kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Or voyant beaucoup de Pharisiens et de Saducéens venant à son baptême, il leur dit: Race de vipères, qui vous a montré à fuir devant la colère qui va venir?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba.
Faites donc de dignes fruits de pénitence.
9 Wala msidhani mnaweza kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwa mawe haya.
Et ne songez pas à dire en vous-mêmes: Nous avons Abraham pour père; car je vous le dis, Dieu peut, de ces pierres mêmes, susciter des enfants à Abraham.
10 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti, basi kila mti usiozaa matunda mazuri, hukatwa na kutupwa motoni.
Déjà la cognée a été mise à la racine des arbres. Tout arbre donc qui ne produit pas de bon fruit sera coupé et jeté au feu.
11 “Mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba. Lakini nyuma yangu anakuja yeye aliye na uwezo kuliko mimi, ambaye sistahili hata kuvichukua viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Moi, à la vérité, je vous baptise dans l’eau pour la pénitence; mais celui qui doit venir après moi est plus puissant que moi; et je ne suis pas digne de porter sa chaussure: lui-même vous baptisera dans l’Esprit saint et dans le feu.
12 Pepeto lake liko mkononi mwake, naye atasafisha sakafu yake ya kupuria, na kuikusanya ngano ghalani na kuyateketeza makapi kwa moto usiozimika.”
Son van est dans sa main, et il nettoyera entièrement son aire: il amassera son blé dans le grenier; mais il brûlera la paille dans un feu qui ne peut s’éteindre.
13 Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Mto Yordani ili Yohana ambatize.
Alors Jésus vint de la Galilée au Jourdain vers Jean pour être baptisé par lui.
14 Lakini Yohana akajitahidi kumzuia, akimwambia, “Mimi ninahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu nikubatize?”
Or Jean le détournait, disant: C’est moi qui dois être baptisé par vous, et vous venez à moi!
15 Lakini Yesu akamjibu, “Kubali hivi sasa, kwa maana ndivyo itupasavyo kwa njia hii kuitimiza haki yote.” Hivyo Yohana akakubali.
Mais, répondant, Jésus lui dit: Laisse maintenant, car c’est ainsi qu’il convient que nous accomplissions toute justice. Alors Jean le laissa.
16 Naye Yesu alipokwisha kubatizwa, mara alipotoka ndani ya maji, ghafula mbingu zikafunguka, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua na kutulia juu yake.
Or ayant été baptisé, Jésus sortit aussitôt de l’eau; et voici que les cieux lui furent ouverts: il vit l’Esprit de Dieu descendant en forme de colombe et venant sur lui.
17 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ambaye ninapendezwa sana naye.”
Et voici une voix du ciel disant: Celui-ci est mon fils bien-aimé en qui j’ai mis mes complaisances.