< Mathayo 3 >

1 Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Uyahudi, akisema,
那時,洗者若翰出現在猶太曠野宣講說:
2 “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
「你們悔改吧!因為天國臨近了。」
3 Huyu ndiye yule aliyenenwa habari zake na nabii Isaya aliposema: “Sauti ya mtu aliaye huko nyikani, ‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
這人便是那藉先知依撒依亞所預言的:「在曠野有呼號者的聲音:你們該當預備上主的道路,修直衪的途徑。」
4 Basi Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia, akiwa na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
這若翰穿著駱駝毛做的衣服,腰間束著皮帶,他的食物是蝗蟲和野蜜。
5 Watu walikuwa wakimwendea kutoka Yerusalemu, Uyahudi yote na nchi zote za kandokando ya Mto Yordani.
那時,耶路撒冷、全猶太以及全約但河一帶的人;都出來到衪那裏去,
6 Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
承認自己的罪過,並在約但河裏受衪的洗。
7 Lakini alipowaona Mafarisayo na Masadukayo wengi wakija ili kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
衪見到許多法利賽人和賽杜色人來受他的洗,就對他們說:「毒蛇的種類!誰指教你們逃避那即將來臨的忿怒﹖
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba.
那麼,就結出與悔改相稱的果實吧!
9 Wala msidhani mnaweza kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwa mawe haya.
你們自己不要思念說:我們亞巴郎為父。我給你們說:天主能從這些石頭給亞巴郎興起子孫來。
10 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti, basi kila mti usiozaa matunda mazuri, hukatwa na kutupwa motoni.
斧子已放在樹根上了,凡不結好果子的樹,必被砍倒,投入火中。
11 “Mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba. Lakini nyuma yangu anakuja yeye aliye na uwezo kuliko mimi, ambaye sistahili hata kuvichukua viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
我固然用水洗你們,為使你們悔改;但在我以後要來的那一位,比我更強,我連提衪的鞋也不配,衪要以聖神及火洗你們。
12 Pepeto lake liko mkononi mwake, naye atasafisha sakafu yake ya kupuria, na kuikusanya ngano ghalani na kuyateketeza makapi kwa moto usiozimika.”
衪的簸箕已在衪手中,衪要揚敬盡自己的禾場,將衪的麥粒收入倉內,至於糠秕,卻要用不滅的火焚燒。
13 Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Mto Yordani ili Yohana ambatize.
那時,耶穌由加里肋亞來到約但河若翰那裏,為受衪的洗;
14 Lakini Yohana akajitahidi kumzuia, akimwambia, “Mimi ninahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu nikubatize?”
但若翰想要阻止衪說:「我本來需要受你的洗,而你卻來就我嗎﹖
15 Lakini Yesu akamjibu, “Kubali hivi sasa, kwa maana ndivyo itupasavyo kwa njia hii kuitimiza haki yote.” Hivyo Yohana akakubali.
耶穌回答衪說:「你暫且容許吧!因為我們應當這樣,以完成全義。」於是若翰就容許了衪。
16 Naye Yesu alipokwisha kubatizwa, mara alipotoka ndani ya maji, ghafula mbingu zikafunguka, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua na kutulia juu yake.
耶穌受洗後,立時從水裏上來,忽然天為他開了。他看見天主聖神有如鴿子降下,來到他上面;
17 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ambaye ninapendezwa sana naye.”
又有聲音由天上說:「這是我的愛子,我所喜悅的」

< Mathayo 3 >