< Mathayo 3 >

1 Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Uyahudi, akisema,
之后,施洗者约翰出现,在犹太的荒野中传道。
2 “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
他说:“悔改吧,因为天国已降临。”
3 Huyu ndiye yule aliyenenwa habari zake na nabii Isaya aliposema: “Sauti ya mtu aliaye huko nyikani, ‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
约翰便是以赛亚先知曾预言的那个人。预言曾说:在荒野一个声音在呼喊:“预备主的道,修直他的路!”
4 Basi Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia, akiwa na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
约翰身穿驼毛衣服,腰束皮带,以蝗虫和野蜜为食。
5 Watu walikuwa wakimwendea kutoka Yerusalemu, Uyahudi yote na nchi zote za kandokando ya Mto Yordani.
人们从耶路撒冷、犹太全地和约旦河一带赶来,来到他的身边,
6 Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
向他忏悔自己的罪,在约旦河中接受他的施洗。
7 Lakini alipowaona Mafarisayo na Masadukayo wengi wakija ili kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
但约翰看见很多法利赛人和撒都该人也来此受洗,便对他们说:“你们乃毒蛇之子,谁告诉你们可以逃离那即将到来的审判?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba.
你们要拿出行动,证明真心悔改。
9 Wala msidhani mnaweza kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwa mawe haya.
不要心中暗自产生傲慢的想法:‘亚伯拉罕就是我们的祖先。’我告诉你们,上帝可以用这些石头创造亚伯拉罕的后裔。
10 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti, basi kila mti usiozaa matunda mazuri, hukatwa na kutupwa motoni.
事实上,砍树的斧子已经准备好,所有结不出好果子的树,都会被砍倒丢入火中。
11 “Mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba. Lakini nyuma yangu anakuja yeye aliye na uwezo kuliko mimi, ambaye sistahili hata kuvichukua viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
是的,我是用水为你们施洗,显示你们的悔改。但在我之后,还会出现一位比我更伟大之人,我甚至连替他提鞋的资格都没有,他将用圣灵和火为你们施洗。
12 Pepeto lake liko mkononi mwake, naye atasafisha sakafu yake ya kupuria, na kuikusanya ngano ghalani na kuyateketeza makapi kwa moto usiozimika.”
他手里拿着簸谷工具,他将清理打谷场,把麦子收进谷仓,然后用不灭之火把谷壳烧尽。”
13 Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Mto Yordani ili Yohana ambatize.
这时,耶稣从加利利来到约旦河,走到约翰处准备接受他的施洗。
14 Lakini Yohana akajitahidi kumzuia, akimwambia, “Mimi ninahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu nikubatize?”
约翰想要阻止他,说:“我本应由受你施洗,你却要让我来为你施洗吗?”
15 Lakini Yesu akamjibu, “Kubali hivi sasa, kwa maana ndivyo itupasavyo kwa njia hii kuitimiza haki yote.” Hivyo Yohana akakubali.
耶稣答道:“请这样做吧。我们应遵循上帝说是正确之事。”于是约翰便答应下来。
16 Naye Yesu alipokwisha kubatizwa, mara alipotoka ndani ya maji, ghafula mbingu zikafunguka, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua na kutulia juu yake.
当耶稣受洗后从水中立起;忽然天空敞开,他看见上帝之灵降落,如鸽子般落在他身上。
17 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ambaye ninapendezwa sana naye.”
天空传来一个声音,说:“这是吾子,他让我欢喜。”

< Mathayo 3 >