< Mathayo 26 >

1 Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
And it came to pass, when Jesus had finished all these sayings, he said to his disciples,
2 “Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
Ye know that after two days is the passover, and the Son of man is betrayed to be crucified.
3 Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
Then assembled the chief priests, and the scribes, and the elders of the people, in the palace of the high priest, who was called Caiaphas,
4 Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
And consulted that they might take Jesus by subtilty, and kill [him].
5 Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
But they said, Not on the feast -[day], lest there be an uproar among the people.
6 Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
Now when Jesus was in Bethany, in the house of Simon the leper,
7 naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
There came to him a woman having an alabaster-box of very precious ointment, and poured it on his head as he sat [at table].
8 Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
But when his disciples saw [it], they had indignation, saying, To what purpose [is] this waste?
9 Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
For this ointment might have been sold for much, and given to the poor.
10 Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
When Jesus understood [it], he said to them, Why trouble ye the woman? for she hath wrought a good work upon me.
11 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
For ye have the poor always with you; but me ye have not always.
12 Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
For in that she hath poured this ointment on my body, she did [it] for my burial.
13 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Verily I say to you, Wherever this gospel shall be preached in the whole world, [there] shall also this, which this woman hath done, be told for a memorial of her.
14 Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
Then one of the twelve, called Judas Iscariot, went to the chief priests,
15 na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
And said, What will ye give me, and I will deliver him to you? And they covenanted with him for thirty pieces of silver.
16 Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
And from that time he sought opportunity to betray him.
17 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
Now the first [day] of the [feast of] unleavened bread, the disciples came to Jesus, saying to him, Where wilt thou that we prepare for thee to eat the passover?
18 Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
And he said, Go into the city to such a man, and say to him, The Master saith, My time is at hand; I will keep the passover at thy house with my disciples.
19 Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
And the disciples did as Jesus had appointed them; and they made ready the passover.
20 Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
Now when the evening was come, he sat down with the twelve.
21 Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
And as they were eating, he said, Verily I say to you, that one of you will betray me.
22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
And they were exceeding sorrowful, and began every one of them to say to him, Lord, is it I?
23 Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
And he answered and said, He that dippeth [his] hand with me in the dish, the same will betray me.
24 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
The Son of man goeth, as it is written concerning him: but woe to that man by whom the Son of man is betrayed! it had been good for that man, if he had not been born.
25 Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
Then Judas, who betrayed him, answered and said, Master, is it I? He said to him, Thou hast said.
26 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
And as they were eating, Jesus took bread, and blessed [it], and broke [it], and gave [it] to the disciples, and said, Take, eat; this is my body.
27 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
And he took the cup, and gave thanks, and gave [it] to them, saying, Drink ye all of it;
28 Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
For this is my blood of the new testament, which is shed for many for the remission of sin.
29 Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
But I say to you, I will not drink henceforth of this fruit of the vine, until that day when I drink it new with you in my Father's kingdom.
30 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
And when they had sung a hymn, they went out to the mount of Olives.
31 Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
Then saith Jesus to them, All ye shall be offended because of me this night: for it is written, I will smite the shepherd, and the sheep of the flock shall be scattered abroad.
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
But after I am risen again, I will go before you into Galilee.
33 Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
Peter answered and said to him, Though all [men] shall be offended because of thee, [yet] will I never be offended.
34 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jesus said to him, Verily I say to thee, that this night, before the cock shall crow, thou wilt deny me thrice.
35 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Peter said to him, Though I should die with thee, yet will I not deny thee. Likewise also said all the disciples.
36 Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
Then cometh Jesus with them to a place called Gethsemane, and saith to the disciples, Sit ye here, while I go yonder and pray.
37 Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
And he took with him Peter, and the two sons of Zebedee, and began to be sorrowful and very heavy.
38 Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
Then saith he to them, My soul is exceeding sorrowful, even to death: tarry ye here, and watch with me.
39 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
And he went a little further, and fell on his face, and prayed, saying, O my Father, if it is possible, let this cup pass from me: nevertheless, not as I will, but as thou [wilt].
40 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
And he cometh to the disciples, and findeth them asleep, and saith to Peter, What, could ye not watch with me one hour?
41 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Watch and pray, that ye enter not into temptation: the spirit indeed [is] willing, but the flesh [is] weak.
42 Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
He went away again the second time, and prayed, saying, O my Father, if this cup may not pass away from me, except I drink it, thy will be done.
43 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
And he came and found them asleep again: for their eyes were heavy.
44 Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
And he left them, and went away again, and prayed the third time, saying the same words.
45 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Then he cometh to his disciples, and saith to them, Sleep on now, and take [your] rest: behold, the hour is at hand, and the Son of man is betrayed into the hands of sinners.
46 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Rise, let us be going: behold, he is at hand that doth betray me.
47 Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
And while he was yet speaking, lo, Judas, one of the twelve, came, and with him a great multitude with swords and staffs, from the chief priests and elders of the people.
48 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
Now he that betrayed him, gave them a sign, saying, Whomsoever I shall kiss, that same is he; hold him fast.
49 Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
And forthwith he came to Jesus, and said, Hail Master; and kissed him.
50 Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
And Jesus said to him, Friend, Why art thou come? Then they came, and laid hands on Jesus, and took him.
51 Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
And behold, one of them, who were with Jesus, stretched out [his] hand, and drew his sword, and struck a servant of the high priest, and smote off his ear.
52 Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
Then said Jesus to him, Put up again thy sword into its place: for all they that take the sword, shall perish by the sword.
53 Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
Thinkest thou that I cannot now pray to my Father, and he will presently give me more than twelve legions of angels?
54 Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
But how then shall the scriptures be fulfilled, that thus it must be?
55 Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
In that same hour said Jesus to the multitudes, Are ye come out as against a thief with swords and staffs to take me? I sat daily with you teaching in the temple, and ye laid no hold on me.
56 Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
But all this was done, that the scriptures of the prophets might be fulfilled. Then all the disciples forsook him, and fled.
57 Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
And they that had laid hold on Jesus, led [him] away to Caiaphas the high priest, where the scribes and the elders were assembled.
58 Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
But Peter followed him at a distance, to the high priest's palace, and went in, and sat with the servants to see the end.
59 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
Now the chief priests and elders, and all the council, sought false testimony against Jesus, to put him to death;
60 Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
But found none: and, though many false witnesses came, [yet] found they none. At the last came two false witnesses,
61 na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
And said, This [man] said, I am able to destroy the temple of God, and to build it in three days.
62 Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
And the high priest arose, and said to him, Answerest thou nothing, what [is it which] these testify against thee?
63 Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
But Jesus held his peace. And the high priest answered and said to him, I adjure thee by the living God, that thou tell us whether thou art the Christ the Son of God.
64 Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
Jesus saith to him, Thou hast said: nevertheless I say to you, Hereafter shall ye see the Son of man sitting on the right hand of power, and coming in the clouds of heaven.
65 Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
Then the high priest rent his clothes, saying, He hath spoken blasphemy; what further need have we of witnesses? behold, now ye have heard his blasphemy.
66 Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
What think ye? They answered and said, He is guilty of death.
67 Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
Then they spit in his face, and buffetted him; and others smote [him] with the palms of their hands,
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
Saying, Prophesy to us, thou Christ, Who is he that smote thee?
69 Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
Now Peter sat without in the palace: and a damsel came to him, saying, Thou also wast with Jesus of Galilee.
70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
But he denied before [them] all, saying, I know not what thou sayest.
71 Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
And when he had gone out into the porch, another [maid] saw him, and said to them that were there, This [man] was also with Jesus of Nazareth.
72 Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
And again he denied with an oath, I do not know the man.
73 Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
And after a while came to [him] they that stood by, and said to Peter, Surely thou also art [one] of them; for thy speech betrayeth thee.
74 Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
Then began he to curse and to swear, [saying], I know not the man. And immediately the cock crowed.
75 Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
And Peter remembered the word of Jesus, who said to him, Before the cock shall crow, thou wilt deny me thrice. And he went out, and wept bitterly.

< Mathayo 26 >