< Mathayo 26 >

1 Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
And it came to pass, when Jesus had finished all these sayings, that he said to his disciples,
2 “Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
Ye know that after two days cometh the passover; and the Son of man is delivered up to be crucified.
3 Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
Then the chief priests and the elders of the people assembled in the court of the palace of the high-priest, named Caiaphas;
4 Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
and took counsel together that they might seize Jesus by craft, and put him to death.
5 Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
But they said, Not at the feast, lest there be an uproar among the people.
6 Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
Now when Jesus was at Bethany, in the house of Simon the leper,
7 naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
there came to him a woman having an alabaster bottle of very costly ointment, and poured it on his head while he was reclining at table.
8 Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
But the disciples seeing it, were much displeased, saying, To what purpose is this waste?
9 Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
For this might have been sold for much, and given to the poor.
10 Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
And Jesus, perceiving it, said to them, Why do ye trouble the woman? For she hath done a good deed to me.
11 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
For the poor ye have always with you; but me ye have not always.
12 Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
For she, in pouring this ointment on my body, hath done it to prepare me for burial.
13 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Truly do I say to you, Wherever these glad tidings shall be published in the whole world, this too which she hath done will be told for a memorial of her.
14 Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
Then one of the twelve, called Judas Iscariot, went to the chief priests,
15 na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
and said, What will ye give me, and I will deliver him up to you? And they paid him thirty pieces of silver.
16 Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
And from that time he sought an opportunity to deliver him up.
17 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
And on the first of the days of unleavened bread the disciples came to Jesus, saying, Where wilt thou that we make ready for thee to eat the passover?
18 Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
And he said, Go into the city to such a man, and say to him, The Teacher saith, My time is at hand; I keep the passover at thy house with my disciples.
19 Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
And the disciples did as Jesus directed them, and made ready the passover.
20 Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
And when evening came, he took his place at table with the twelve disciples.
21 Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
And as they were eating, he said, Truly do I say to you, that one of you will betray me.
22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
And they were exceedingly sorrowful, and began every one to say to him, Is it I, Lord?
23 Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
And he answering said, He that hath dipped his hand with me in the dish, he will betray me.
24 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
The Son of man indeed goeth away, as it hath been written concerning him; but woe to that man by whom the Son of man is betrayed! Well were it for that man if he had not been born.
25 Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
Then Judas, his betrayer, answering said, Is it I, Rabbi? He saith to him, It is.
26 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
And, as they were eating, Jesus took a loaf, and having blessed, broke it, and gave it to the disciples, and said, Take, eat; this is my body.
27 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
And he took a cup, and gave thanks, and gave it to them, saying, Drink ye all of it;
28 Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
for this is my blood of the covenant, which is shed for many for remission of sins.
29 Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
And I say to you, I shall not drink henceforth of this fruit of the vine, until that day when I drink it new with you in the kingdom of my Father.
30 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
And having sung a hymn, they went out to the Mount of Olives.
31 Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
Then Jesus saith to them, This night will all of you fall away from me; for it is written, “I will smite the shepherd, and the sheep of the flock will be scattered.”
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
But after I have risen, I will go before you into Galilee.
33 Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
Peter answering said to him, Though all should fall away from thee, yet will I never fall away.
34 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jesus said to him, Truly do I say to thee, that this night, before a cock crows, thou wilt thrice deny me.
35 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Peter saith to him, Even if I must die with thee, I will not deny thee. And so said all the disciples.
36 Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
Then Jesus cometh with them to a place called Gethsemane, and saith to the disciples, Sit here, while I go yonder and pray.
37 Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
And taking with him Peter and the two sons of Zebedee, he began to he sorrowful and full of anguish.
38 Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
Then he saith to them, My soul is exceedingly sorrowful, even to death; remain here, and watch with me.
39 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
And he came a little nearer, and fell on his face, praying and saying, Father, if it be possible, let this cup pass from me! nevertheless, not as I will, but as Thou wilt.
40 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
And he cometh to the disciples, and findeth them sleeping, and saith to Peter, Is it so that ye could not watch with me one hour?
41 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Watch, and pray that ye enter not into temptation; the spirit indeed is willing, but the flesh is weak.
42 Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
Again he went away a second time, and prayed, saying, My Father, if this [[cup]] cannot pass away from me, but I must drink it, thy will be done!
43 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
And coming again he found them sleeping; for their eyes were heavy.
44 Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
And leaving them, he went away again, and prayed the third time, saying again the same words.
45 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Then he cometh to the disciples, and saith to them, Sleep on, and take your rest! Lo! the hour is at hand, and the Son of man is delivered up into the hands of sinners.
46 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Rise, let us be going; lo! he is at hand that delivereth me up.
47 Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
And while he was yet speaking, lo! Judas, one of the twelve, came, and with him a great multitude with swords and clubs, from the chief priests and elders of the people.
48 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
And his betrayer had given them a sign, saying, Whomever I shall kiss, he is the man; seize him.
49 Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
And immediately going up to Jesus, he said, Hail, Rabbi! and kissed him.
50 Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
And Jesus said to him, Friend, for what hast thou come! Then they came and laid hands on Jesus, and seized him.
51 Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
And, lo! one of those who were with Jesus stretched out his hand, and drew his sword, and struck the servant of the high-priest, and cut off his ear.
52 Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
Then Jesus saith to him, Put back thy sword into its place; for all they that take the sword will perish by the sword.
53 Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
Dost thou think that I cannot pray to my Father, and he will now give me more than twelve legions of angels?
54 Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
But how then shall the Scriptures be fulfilled, that thus it must be?
55 Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
In that hour Jesus said to the multitudes, Ye have come out as against a robber, with swords and clubs to take me; I sat daily teaching in the temple, and ye did not lay hands on me.
56 Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
But all this hath been done, that the Scriptures of the prophets may be fulfilled. Then all the disciples forsook him, and fled.
57 Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
And they who seized Jesus led him away to Caiaphas the high-priest, where the scribes and the elders were assembled.
58 Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
But Peter followed him at a distance, as far as to the court of the high-priest's palace, and went in, and sat with the officers to see the end.
59 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
And the chief priests and the whole council sought false witness against Jesus, to put him to death;
60 Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
and they found none, though many false witnesses came forward. But at last came two,
61 na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
and said, This man affirmed, I am able to destroy the temple of God, and to build it within three days.
62 Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
And the high-priest arose, and said to him, Dost thou make no answer to what these men testify against thee?
63 Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
But Jesus was silent. And the high-priest answering said to him, I adjure thee by the living God, that thou tell us whether thou art the Christ, the Son of God.
64 Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
Jesus saith to him, I am. Moreover I say to you, Henceforth ye will see the Son of man sitting on the right hand of Power, and coming on the clouds of heaven.
65 Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
Then the high-priest rent his garments, saying, He hath spoken blasphemy; what further need have we of witnesses? See! ye have now heard the blasphemy.
66 Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
What think ye? They answered and said, He should be punished with death.
67 Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
Then they spit in his face, and buffeted him; and some smote him with the palms of their hands,
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
saying, Prophesy to us, O Messiah! who it was that struck thee.
69 Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
Now Peter was sitting outside in the court. And a maid-servant came to him, saying, Thou also wast with Jesus the Galilaean.
70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
But he denied before them all, saying, I know not what thou sayest.
71 Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
And when he had gone out into the porch, another woman saw him, and said to those who were there, This man was with Jesus the Nazarene.
72 Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
And again he denied with an oath; I do not know the man.
73 Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
And shortly after, they who were standing by came and said to Peter, Surely thou too art one of them; for thy speech betrayeth thee.
74 Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
Then he began to curse and to swear, saying, I do not know the man. And immediately a cock crew.
75 Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
And Peter remembered the word of Jesus, who had said, Before a cock crows, thou wilt thrice deny me. And he went out, and wept bitterly.

< Mathayo 26 >