< Mathayo 26 >
1 Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
And it came to passe, when Iesus had finished all these sayings, he saide vnto his disciples,
2 “Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
Ye know that after two dayes is ye Passeouer, and the Sonne of man shalbe deliuered to be crucified.
3 Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
Then assembled together the chiefe Priests, and the Scribes, and the Elders of ye people into the hall of the high Priest called Caiaphas:
4 Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
And consulted together that they might take Iesus by subtiltie, and kill him.
5 Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
But they sayd, Not on the feast day, least any vprore be among the people.
6 Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
And when Iesus was in Bethania, in the house of Simon the leper,
7 naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
There came vnto him a woman, which had a boxe of very costly oyntment, and powred it on his head, as he sate at the table.
8 Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
And when his disciples sawe it, they had indignation, saying, What needed this waste?
9 Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
For this oyntment might haue bene solde for much, and bene giuen to the poore.
10 Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
And Iesus knowing it, sayde vnto them, Why trouble yee the woman? for shee hath wrought a good woorke vpon me.
11 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
For yee haue the poore alwayes with you, but me shall yee not haue alwaies.
12 Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
For in that shee powred this oyntment on my bodie, shee did it to burie me.
13 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Verely I say vnto you, wheresoeuer this Gospel shall bee preached throughout all the worlde, there shall also this that shee hath done, be spoken of for a memoriall of her.
14 Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
Then one of the twelue, called Iudas Iscariot, went vnto the chiefe Priestes,
15 na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
And said, What will ye giue me, and I will deliuer him vnto you? and they appoynted vnto him thirtie pieces of siluer.
16 Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
And from that time, he sought opportunitie to betraie him.
17 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
Nowe on the first day of the feast of vnleauened bread the disciples came to Iesus, saying vnto him, Where wilt thou that we prepare for thee to eate the Passeouer?
18 Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
And he said, Goe yee into the citie to such a man, and say to him, The master saieth, My time is at hande: I will keepe the Passeouer at thine house with my disciples.
19 Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
And the disciples did as Iesus had giuen them charge, and made readie the Passeouer.
20 Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
So when the Euen was come, hee sate downe with the twelue.
21 Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
And as they did eate, he sayde, Verely I say vnto you, that one of you shall betraie me.
22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
And they were exceeding sorowfull, and began euery one of them to say vnto him, Is it I, Master?
23 Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
And hee answered and sayde, Hee that dippeth his hande with me in the dish, hee shall betraie me.
24 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
Surely the Sonne of man goeth his way, as it is written of him: but woe be to that man, by whom the Sonne of man is betrayed: it had bene good for that man, if hee had neuer bene borne.
25 Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
Then Iudas which betraied him, answered and sayde, Is it I, Master? He sayde vnto him, Thou hast sayd it.
26 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
And as they did eate, Iesus tooke the bread, and when he had blessed, he brake it, and gaue it to the disciples, and sayd, Take, eate: this is my bodie.
27 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
Also he tooke the cuppe, and when he had giuen thankes, he gaue it them, saying, Drinke ye all of it.
28 Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
For this is my blood of the Newe Testament, that is shedde for many, for the remission of sinnes.
29 Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
I say vnto you, that I will not drinke henceforth of this fruit of the vine vntil that day, when I shall drinke it new with you in my Fathers kingdome.
30 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
And when they had sung a Psalme, they went out into the mount of Oliues.
31 Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
Then saide Iesus vnto them, All yee shall be offended by me this night: for it is written, I wil smite the shepheard, and the sheepe of the flocke shalbe scattered.
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
But after I am risen againe, I will go before you into Galile.
33 Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
But Peter aunswered, and sayde vnto him, Though that al men should be offended by thee, yet will I neuer be offended.
34 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Iesus sayde vnto him, Verely I say vnto thee, that this night, before the cocke crow, thou shalt denie me thrise.
35 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Peter saide vnto him, Though I should die with thee, I will in no case denie thee. Likewise also sayd all the disciples.
36 Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
Then went Iesus with them into a place which is called Gethsemane, and said vnto his disciples, Sit ye here, while I goe, and pray yonder.
37 Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
And hee tooke vnto him Peter, and the two sonnes of Zebedeus, and began to waxe sorowfull, and grieuously troubled.
38 Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
Then sayde Iesus vnto them, My soule is very heauie, euen vnto the death: tarie yee here, and watch with me.
39 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
So hee went a litle further, and fell on his face, and praied, saying, O my Father, if it be possible, let this cup passe from me: neuerthelesse, not as I will, but as thou wilt.
40 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
After, hee came vnto the disciples, and founde them a sleepe, and sayde to Peter, What? coulde yee not watch with me one houre?
41 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Watch, and praie, that yee enter not into tentation: the spirit in deede is readie, but the flesh is weake.
42 Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
Againe he went away the second time, and praied, saying, O my Father, if this cuppe can not passe away from mee, but that I must drinke it, thy will be done.
43 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
And he came, and founde them a sleepe againe, for their eyes were heauie.
44 Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
So he left them and went away againe, and praied the third time, saying the same woordes.
45 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Then came he to his disciples, and said vnto them, Sleepe henceforth, and take your rest: behold, the houre is at hand, and the Sonne of man is giuen into the hands of sinners.
46 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Rise, let vs goe: beholde, hee is at hande that betraieth me.
47 Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
And while hee yet spake, loe Iudas, one of the twelue, came, and with him a great multitude with swordes and staues, from the high Priests and Elders of the people.
48 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
Now he that betraied him, had giuen them a token, saying, Whomesoeuer I shall kisse, that is he, laie holde on him.
49 Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
And forthwith he came to Iesus, and sayd, God saue thee, Master, and kissed him.
50 Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
Then Iesus sayde vnto him, Friende, wherefore art thou come? Then came they, and laide hands on Iesus, and tooke him.
51 Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
And behold, one of them which were with Iesus, stretched out his hand, and drewe his sworde, and strooke a seruaunt of the high Priest, and smote off his eare.
52 Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
Then sayde Iesus vnto him, Put vp thy sworde into his place: for all that take the sworde, shall perish with the sworde.
53 Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
Either thinkest thou, that I can not now pray to my Father, and he will giue me moe then twelue legions of Angels?
54 Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
Howe then shoulde the Scriptures bee fulfilled, which say, that it must be so?
55 Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
The same houre sayde Iesus to the multitude, Ye be come out as it were against a thiefe, with swordes and staues to take mee: I sate daily teaching in the Temple among you, and yee tooke me not.
56 Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
But all this was done, that the Scriptures of the Prophets might be fulfilled. Then all the disciples forsooke him, and fled.
57 Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
And they tooke Iesus, and led him to Caiaphas the hie Priest, where the Scribes and the Elders were assembled.
58 Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
And Peter followed him a farre off vnto the hie Priestes hall, and went in, and sate with the seruants to see the ende.
59 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
Nowe the chiefe Priestes and the Elders, and all the whole councill sought false witnesse against Iesus, to put him to death.
60 Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
But they founde none, and though many false witnesses came, yet founde they none: but at the last came two false witnesses,
61 na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
And saide, This man saide, I can destroie the Temple of God, and build it in three daies.
62 Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
Then the chiefe Priest arose, and sayde to him, Answerest thou nothing? What is the matter that these men witnesse against thee?
63 Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
But Iesus helde his peace. Then the chiefe Priest answered, and saide to him, I charge thee sweare vnto vs by the liuing God, to tell vs, If thou be that Christ the Sonne of God, or no.
64 Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
Iesus saide to him, Thou hast saide it: neuerthelesse I say vnto you, hereafter shall ye see the Sonne of man, sitting at the right hande of the power of God, and come in the cloudes of the heauen.
65 Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
Then the hie Priest rent his clothes, saying, Hee hath blasphemed, what haue wee any more neede of witnesses? beholde: nowe yee haue heard his blasphemie.
66 Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
What thinke yee? They answered, and said, He is guiltie of death.
67 Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
Then spet they in his face, and buffeted him, and other smote him with roddes,
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
Saying, Prophecie to vs, O Christ, Who is he that smote thee?
69 Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
Peter sate without in the hall, and a maide came to him, saying, Thou also wast with Iesus of Galile:
70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
But hee denied before them all, saying, I wote not what thou saiest.
71 Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
And when hee went out into the porche, another maide sawe him, and sayde vnto them that were there, This man was also with Iesus of Nazareth.
72 Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
And againe he denied with an othe, saying, I knowe not the man.
73 Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
So after a while, came vnto him they that stoode by, and sayde vnto Peter, Surely thou art also one of them: for euen thy speache bewraieth thee.
74 Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
Then began hee to curse himselfe, and to sweare, saying, I knowe not the man. And immediately the cocke crewe.
75 Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
Then Peter remembred the wordes of Iesus, which had sayde vnto him, Before the cocke crowe thou shalt denie me thrise. So he went out, and wept bitterly.