< Mathayo 26 >

1 Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
Amo olelesu sia: dagoloba, Yesu da Ea fa: no bobogesu dunuma amane sia: i,
2 “Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
“Dilia dawa: ! Eso aduna aligili, Baligisu Lolo Nasu da ba: mu. Ilia da Dunu Egefe bulufalegeiga dabagala: musa: gagulaligimu.”
3 Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
Amalalu, gobele salasu dunu amola Gode Ea diasu ouligisu dunu da gobele salasu dunu Ouligisu ea dio amo Ga: iafa: se, amo ea diasuga gilisi dagoi.
4 Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
Ilia da Yesu wamowane afugili, medole legemusa: , amane ilegele sia: i,
5 Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
“Dunu huluane da amo hou higabeba: le, halale gegesa: besa: le, Lolo Nasu amo ganodini hamomu da hamedei.”
6 Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
Eso afaega, Yesu da Bedani moilaiga, lebolosi oloi dunu Saimone amo ea diasuga esalu.
7 naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
E da ha: i nanoba, uda afae da Ema misini, manoma gabusiga: gala ganagu ganodini sali, Yesu Ea dialuma da: iya sogadigi.
8 Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
Amo hou ba: beba: le, Yesu Ea ado ba: su dunu ilia da ougili amane sia: i, “Liligi ida: iwane abuli udigili ha: digibela: ?
9 Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
Amo gabusiga: hano bidi lale, amo muni lai hame gagui dunuma imunu da defea galu!”
10 Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
Be Yesu da ilia sia: dasu dawa: beba: le, amane sia: i, “Dilia abuliba: le amo udama mi hananewane sia: sala: ? E da Nama hou ida: iwane hamoi.
11 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
Dilia da hame gagui dunu eso huluane ba: mu. Be dilia da Na hobea hame ba: mu.
12 Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
E da Na bogole ulidogone salimu hou amoma asigiba: le, Na da: i hodo legema: ne, waha agoane hamoi.
13 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Na dafawane sia: sa! Osobo bagadega, soge huluanedafa amoga Na sia: ida: iwanegala dunu ilia olelesea, ilia da amo uda dawa: ma: ne, ea hou Nama waha hamoi olelemu.”
14 Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
Amalalu, Yesu Ea ado ba: su dunu afadafa amo Yudase Isaga: liode, e da ado ba: su dunu fagoyale yolesili, gobele salasu ouligisu dunu ilima doaga: i.
15 na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
E da ilima amane adole ba: i, “Na da Yesu dilima ima: ne hohonosea, dilia muni habodayane ima: bela: ?” Amalalu, ilia fage eme esala (silifa) 30 agoane idili, Yudasema i.
16 Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
Amalalu, Yudase da Yesu hohonone, ilima imunusa: logo hogolalu.
17 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
Isala: ili dunu da agi ga: gi Yisidi hame sali amo lolo nanoba, eso agega, Yesu Ea fa: no bobogesu dunu da Ema doaga: le, amane sia: i, “Ninia habidili Baligisu Lolo manusa: hahamoma: bela: ?”
18 Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
Yesu E bu adole i, “Yelusalemega asili, dilia da dunu ba: mu. Ema amane sia: ma, ‘Ninia Olelesu dunu ea ilegei eso da doaga: i dagoi. E amola ea ado ba: su dunu, ilia dia diasuga Baligisu lolo manu galebe.’”
19 Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
Amo sia: nababeba: le, ilia da Yesu Ea olelei hamoi. Ilia Baligisu Lolo Nasu manusa: hahamoi.
20 Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
Daeya doaga: loba, Yesu amola Ea fa: no bobogesu dunu fagoyale gala da ha: i manusa: esalu.
21 Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
Ha: i nananoba, Yesu E amane sia: i, “Na da dafawane sia: sa! Dunu afae ninia gilisisu ganodini da Na hohonomu.”
22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
Ilia huluane da se bagade nabi. Ilia da afae afae Yesuma amane adole boba: i, “Hina! Di da na hamomu sia: sala: ?”
23 Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
E da bu adole i, “Dunu afadafa, e amola Na gilisili hano ofodoga agi ga: gi gele iasea, amo dunu da Na hohonomu.
24 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
Dunu Egefe, Gode Sia: Dedei defele, da bogomu. Be Ea hohonosu dunu da se bagade nabimu. Amo dunu da hamedafa lalelegemu da defea galu.”
25 Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
Yesu Ea hohonosu dunu Yudase da amane sia: i, “Olelesu! Di da na hamomu sia: sala: ?” Yesu E bu adole i, “Di da sia: i dagoi!”
26 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
Ilia ha: i nanoba, Yesu da agi ga: gi lale, Godema nodone sia: ne gadole, amo agi ga: gi fifili, Ea fa: no bobogesu dunuma i. E amane sia: i, “Lale moma! Amo da Na da: i hodo.”
27 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
Amalalu, E da faigelei lale, Godema nodone sia: ne gadole, ilima i. E amane sia: i, “Dilia huluane amo waini hano moma.
28 Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
Go da Na maga: me. Gesele nasu gousa: su gaheabolo da amoga hamoi dagoi. Na maga: me sogadigimuba: le, dunu bagohame da gogolema: ne olofosu ba: mu.
29 Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
Na dilima sia: sa! Na amola dilia da osobo bagadega waini hano moma: ne, bu hame gilisimu. Gode Ea Hinadafa Hou soge ganodini fawane, ninia bu gilisili gaheabolowane manu.”
30 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
Amalalu, gesami hea: lalu, ilia Olife Goumiga asi.
31 Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
Amalalu, Yesu da ilima amane sia: i, “Wali gasia, dilia huluane da Na yolesili, hobeamu. Gode Sia: Dedei amo ganodini agoane dedei diala, ‘Gode da sibi ouligisu dunu medole legebeba: le, sibi da udigili hobeale afafamu.’
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
Be Gode da Na bu wa: legadolesisia, Na da dilima bisili Ga: lili sogega masunu.”
33 Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
Bida e bu adole i, “Dunu huluane da mugulusia, na da Di hamedafa yolesimu.”
34 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Be Yesu da Bidama amane sia: i, “Na dima dafawane sia: sa! Di da hidadea udianawane ‘Yesu na hame dawa: !’ sia: sea, fa: no gagala ga: be nabimu.”
35 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Be Bida da gasawane bu adole i, “Di bogosea, ani galu bogomu da defea. Be ‘Di na hame dawa: ,’ na da hamedafa sia: mu!” Yesu Ea fa: no bobogesu dunu huluane amola da amo defele sia: i.
36 Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
Amalalu, ilia Gedesemani sogebi amoga doaga: i. Yesu da ilima amane sia: i, “Dilia guiguda: esaloma! Na da gagoega sia: ne gadomusa: masunu!”
37 Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
Asili, E da Bida amola Sebedi ea mano aduna oule asi. Yesu da Ea dogo ganodini se bagadedafa nabi.
38 Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
E da ilima amane sia: i, “Na da bogomuwane se naba. Dilia Na fidima: ne, guiguda: mae golale sosodo ouesaloma.”
39 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
Yesu E fonobahadi asili, osoboga gala: lasa: ili, amane sia: ne gadoi, “Ada! Logo eno galea, amo se nabasu faigelei Nama ilegei, Di fadegama! Be na asigi dawa: su hanai liligi hame. Dia asigi dawa: suga hanai liligi fawane Na da hamomu.”
40 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
E da Ea fa: no bobogesu dunu udiana ilima sinidigili ba: loba, ili golai dialebe ba: i. E da Bidama amane sia: i, “Dilia abuliba: le ‘aua’ afadafa fawane ouligimu da hamedesala: ?
41 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Dawa: iwane esaloma! Dilia da dafama: ne ado ba: su amoga dafasa: besa: le ha: esaloma! Dilia a: silibu da gasa bagade, be da: i ea hou da gogaiya: i.”
42 Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
Yesu da bu asili, bu amane sia: ne gadoi, “Ada! Amo se nabasu faigelei fadegamuda hamedei galea, defea, Dia asigi dawa: su hou fawane Na da hamomu.”
43 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
Ea ado ba: su dunu udiana ilima bu sinidigili, ilia bu golai dialebe ba: i. Ilia da si fadegaiwane ha: esalumu gogolei galu.
44 Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
Amalalu, bu yolesili, asili, Yesu E da eno agoane Ea musa: sia: ne gadoi bu sia: i.
45 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Amalalu, E da Ea ado ba: su dunuma bu sinidigili, amane sia: i, “Dilia da mae nedigili, golabe amola helefisala: ? Dawa: ma: i! Ilegei eso da doaga: i dagoi! Dunu Egefe da enoga hohonoi dagoi amola wadela: i hamosu dunu da wali E gagulaligimu galebe.
46 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Wa: legadoma! Hadiga! Na hohonosu dunu manebe goea!”
47 Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
Yesu E sia: nanoba, Yudase, (Yesu Ea ado ba: su dunu fagoyale gala amo fi dunu afae) da doaga: i. Dunu bagohame, gobihei bagade amola gigi gagui, gobele salasu amola Gode Ea diasu ouligisu dunu asunasiba: le, amo dunu ilia Yudase ea baligia aligili misi.
48 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
Yesu Ea hohonosu dunu da hidadea ilima sia: i galu, “Nowa dunu na nonogobe ba: sea, amo dunu dilia afugili gagulaligima.”
49 Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
Amalalu, Yudase da Yesuma doaga: le, hahawane amane sia: i, “Olelesu! Olofoiwane esaloma!” Amalalu, e da Yesu nonogoi dagoi.
50 Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
Yesu da Yudasema amane sia: i, “Defea na: iyado! Dia hou amo hedolo hamoma!” Amalalu, gegesu gobihei amola gigi gagui dunu da Yesu gagulaligi.
51 Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
Yesu Ea oule misi dunu afadafa da ea gegesu gobihei duga: le gadole, gobele salasu Ouligisu ea hawa: hamosu dunu, amo ea ge damuni fasi.
52 Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
Amalalu, Yesu da ema amane sia: i, “Dia gobihei bu salima! Bai nowa da gobiheiga gegesea, ilia da gobiheiga faiba: le bogomu.
53 Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
Dili adi dawa: bela: ? Na da Na Ada Ema adole ba: i ganiaba, E da a: igele gegesu dunu osia: idafa Na fidima: ne asunasila: loba.
54 Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
Be amo hou agoane hamoi ganiaba, na bogomu Gode Sia: Dedei ganodini diala da hobea didili hame hamoi ba: la: loba.”
55 Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
Yesu da dunu huluanema amane adole ba: i, “Dilia abuli gasawane gegesu gobihei amola gigi gaguiwane, Na afugili lamusa: misibela: ? Na da wamolasu dunula: ? Eso huluane Na Debolo Diasuga sia: olelesa lelu. Be amo esoga, dilia da Na hame gagui.”
56 Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
Be amo hou huluane, balofede dunu ilia Gode Sia: Dedei amo ganodini sia: i da didili hamomusa: misi dagoi. Amalalu, Ea ado ba: su dunu huluane da Yesu yolesili, hobea: i dagoi.
57 Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
Ilia da Yesu afugili, gobele salasu Ouligisu dunu Ga: iafa: se, amo ea diasuga oule asi. Amoga, sema olelesu dunu amola Gode Ea diasu asigilai ouligisu dunu ilia gilisili esalebe ba: i.
58 Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
Bida e da badiliawane fa: no bobogei. E da Ga: iafa: se ea diasu gagoi amo ganodini golili sa: ili, e amola dadi gagui ouligisu dunu gilisili fi. E da fa: no mabe hou ba: musa: , esalu.
59 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
Gobele salasu dunu amola Gausolo dunu huluane da Yesu fuga: musa: , ogogosu sia: bagadewane hogoi helei.
60 Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
Ogogosu nabasu dunu bagohame da Yesu Ea hou wadela: musa: misi. Be ilia da Yesu bogoma: ne medomu logo hame ba: i. Fa: nowane, dunu aduna misini,
61 na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
ela amane sia: i, “Amo dunu E da amane sia: i, ‘Na Gode Ea diasu mugululi, eso udiana amoga fawane bu gagumu, amo hamomusa: Na da defele esala!’”
62 Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
Gobele salasu Ouligisu dunu da wa: legadole, Yesuma amane adole ba: i, “Nabibala: ? Amo diwaneya udidisu sia: nababeba: le, Di da adi sia: ma: bela: ?”
63 Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
Be Yesu E da ouiya: le esalu. Amalalu, gobele salasu Ouligisu dunu da Yesuma amane sia: i, “Defea! Di da wali Gode Ea Dioba: le moloiwane sia: ma! Di da Mesaiala: ? Di da Gode Ea Manodafala: ?”
64 Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
Yesu da ema bu adole i, “Di sia: be goa! Be Na da dilima sia: sa! Wali amola fa: no dilia da Na (Dunu Egefe), Gode Bagadedafa amo Ea lobo dafadili fibi ba: mu. Amola dilia Na muagado mumobi ganodini manebe ba: mu.”
65 Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
Amo sia: nababeba: le, gobele salasu Ouligisu da hina: abula gadelale, amane sia: i, “E da lasogole sia: i dagoi. Ninia da Ea hou ba: su dunu eno hame hogomu. Ea lasogoi sia: dilia huluane nabi dagoi.
66 Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
Dilia adi dawa: bela: ?” Dunu huluane ilia bu adole i, “E da wadela: i hamoi dagoi! Medole legemu da defea!”
67 Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
Amalalu, ilia da Yesu Ea odagia defo aduga: gala: i. Mogili, ilia Yesu lobosunane fai, mogili ilia Ea odagi loboga fai.
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
Ilia da Ema amane sia: i, “Mesaia! Di ba: la: lusu hou hamoma! Nowa ea da Di fabayale sia: ma!”
69 Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
Bida da diasu gadili gagoi ganodini esalu. Amalalu, Gobele salasu Ouligisu dunu ea hawa: hamosu a: fini da Ema doaga: le, amane sia: i, “Di amolawane da Ga: lili dunu. Yesu, ali gilisili lalu.”
70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
Be dunu huluane ilia midadi, Bida da Yesu hame dawa: sia: i. E amane sia: i, “Dia sia: be go na hamedafa dawa:”
71 Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
Bida da gagoi logo holeiga asili, a:fini eno da ea odagi ba: beba: le, eno dunuma amane sia: i, “Amo dunu da Yesu, Na: salede dunu, amo gilisili lalu.”
72 Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
Be Bida e da Yesu hame dawa: , Gode Ea Dioba: le ilegele amane sia: i, “Na da amo dunu hamedafa dawa: !”
73 Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
Fa: no, eno gadenene lelu dunu da Bidama misini, ema amane sia: i, “Dafawane! Di da Yesu Ea fi ilima gilisi dagoi. Dia sia: da ilia sia: defele nababeba: le, ninia dawa: !”
74 Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
Amalalu, Bida da gasa bagadewane gagabuli amane sia: i, “Na da Gode Ea Dioba: le dafawane sia: sa! Na da ogogosa galea, Gode da nama se iasu imunu da defea! Amo dunu Na da hamedafa dawa!” Ea sia: dagobeba: le, gagala gawali da ga: i.
75 Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
Yesu Ea musa: sia: i, “Di da hidadea ‘Yesu na hame dawa:’ udianawane sia: nanu, fa: no gagala ga: be nabimu.” Amo sia: bu dawa: beba: le, Bida da ga asili, se nabawane bagadewane dinanu

< Mathayo 26 >