< Mathayo 25 >

1 “Wakati huo, Ufalme wa Mbinguni utakuwa kama wanawali kumi waliochukua taa zao na kwenda kumlaki bwana arusi.
Taevariik on nagu kümme neidu, kes võtsid oma lambid kaasa ja läksid peigmehega kohtuma.
2 Watano wao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
Viis olid rumalad ja viis targad.
3 Wale wapumbavu walichukua taa zao lakini hawakuchukua mafuta ya akiba,
Rumalad neiud võtsid oma lambid, kuid ei võtnud kaasa õli,
4 lakini wale wenye busara walichukua taa zao na mafuta ya akiba kwenye vyombo.
samal ajal targad neiud võtsid kaasa nii õlinõud kui ka lambid.
5 Bwana arusi alipokawia kuja wale wanawali wote wakasinzia na kulala.
Peigmehe tulek viibis ning kõik neiud jäid uniseks ja uinusid magama.
6 “Usiku wa manane pakawa na kelele: ‘Tazameni, huyu hapa bwana arusi! Tokeni nje mkamlaki!’
Keskööl kõlas hüüd: „Vaadake, peigmees on kohal! Tulge välja temaga kohtuma!“
7 “Ndipo wale wanawali wote wakaamka na kuzitengeneza taa zao.
Kõik neiud ärkasid ja kohendasid oma lampide tahti. Rumalad neiud ütlesid tarkadele:
8 Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni mafuta yenu kidogo; taa zetu zinazimika.’
„Andke meile veidi oma õli, sest meie lambid kustuvad.“Aga targad neiud vastasid:
9 “Lakini wale wenye busara wakawajibu, ‘Sivyo, hayatutoshi sisi na ninyi pia. Afadhali mwende kwa wauzao mkajinunulie mafuta yenu.’
„Ei, sest muidu ei jaguks sellest ei teile ega meile. Minge poodnike juurde ja ostke endale õli.“
10 “Nao walipokuwa wakienda kununua mafuta, bwana arusi akafika. Wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia ndani pamoja naye kwenye karamu ya arusi na mlango ukafungwa.
Sel ajal kui nad läksid õli ostma, jõudis peigmees kohale, ja need, kes olid valmis, läksid koos temaga sisse pulmapeole, ja uks pandi lukku.
11 “Baadaye wale wanawali wengine nao wakaja, wakaita, ‘Bwana! Bwana! Tufungulie mlango!’
Teised neiud tulid hiljem. „Isand, isand!“hüüdsid nad. „Ava meile uks!“
12 “Lakini yeye bwana arusi akawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, siwajui ninyi!’
Kuid peigmees vastas: „Ma ütlen teile tõtt: ma ei tunne teid.“
13 “Kwa hiyo kesheni, kwa sababu hamjui siku wala saa.
Nii et olge valvsad, sest te ei tea päeva ega tundi.
14 “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama mtu aliyetaka kusafiri, naye akawaita watumishi wake na kuweka mali yake kwenye uangalizi wao.
See on nagu mees, kes läks ära reisile. Ta kutsus kokku oma sulased ja usaldas nende kätte oma vara.
15 Mmoja akampa talantatano, mwingine talanta mbili, na mwingine talanta moja. Kila mmoja alipewa kwa kadiri ya uwezo wake. Kisha yeye akasafiri.
Ühele sulasele andis ta viis talenti, teisele kaks ja kolmandale ühe, vastavalt nende erinevatele võimetele. Siis ta lahkus.
16 Yule aliyepewa talanta tano akaenda mara moja akafanya nazo biashara akapata talanta nyingine tano zaidi.
Viis talenti saanu läks kohe ja investeeris need ärisse ning sai juurde veel viis talenti.
17 Yule aliyepewa talanta mbili akafanya vivyo hivyo, akapata nyingine mbili zaidi.
Samamoodi sai kaks talenti saanu veel kaks juurde.
18 Lakini yule mtumishi aliyekuwa amepokea talanta moja, alikwenda akachimba shimo ardhini na kuificha ile fedha ya bwana wake.
Aga mees, kes oli saanud ühe talendi, läks ja kaevas augu ning peitis oma isanda raha ära.
19 “Baada ya muda mrefu, yule bwana wa wale watumishi akarudi na kufanya hesabu nao.
Kaua aega hiljem tuli nende sulaste isand tagasi ja õiendas nendega arved.
20 Yule mtumishi aliyepokea talanta tano akaja, akaleta nyingine tano zaidi. Akasema, ‘Bwana uliweka kwenye uangalizi wangu talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta tano zaidi.’
Viis talenti saanu tuli ja tõi kaasa veel viis talenti. „Isand, “ütles ta, „sa andsid mulle viis talenti. Vaata, ma sain viis talenti kasu.“
21 “Bwana wake akamwambia, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
Isand ütles talle: „Sa oled hästi teinud, sa oled hea ja ustav sulane. Sa tõestasid, et oled usaldusväärne väikestes asjades, nii et ma panen sind nüüd paljude asjade eest vastutama. Ole rõõmus, sest ma olen tõesti sinuga rahul!“
22 “Yule mwenye talanta mbili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, uliweka kwenye uangalizi wangu talanta mbili. Tazama nimepata hapa talanta mbili zaidi.’
Tuli ka see, kes oli saanud kaks talenti. „Isand, “ütles ta, „sa andsid mulle kaks talenti. Vaata, ma sain kaks talenti kasu.“
23 “Bwana wake akajibu, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
Isand ütles talle: „Sa oled hästi teinud, sa oled hea ja ustav sulane. Sa tõestasid, et oled usaldusväärne väikestes asjades, nii et ma panen sind nüüd paljude asjade eest vastutama. Ole rõõmus, sest ma olen tõesti sinuga rahul!“
24 “Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya mbegu.
Siis tuli ühe talendiga mees. „Isand, “ütles ta, „ma tean, et sa oled karm mees. Sa lõikad sealt, kuhu sa pole külvanud, ja kogud saaki sealt, kuhu sa pole istutanud.
25 Kwa hiyo niliogopa, nikaenda, nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa ile iliyo mali yako.’
Kuna ma kartsin sind, läksin ma ja matsin su talendi maa sisse. Vaata, sa saad tagasi selle, mis sulle kuulub.“
26 “Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna mahali nisipopanda na kukusanya mahali nisipotawanya mbegu.
Aga isand vastas talle: „Sina nurjatu ja laisk sulane! Kui sa arvad, et ma lõikan sealt, kuhu ma pole külvanud, ja kogun saaki sealt, kuhu ma pole istutanud,
27 Vyema basi, ingekupasa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, ili nirudipo, nichukue ile iliyo yangu na faida yake.
siis oleksid pidanud mu hõbeda panka hoiule andma, et ma koju tulles oleksin saanud oma raha intressiga tagasi.
28 “‘Basi mnyangʼanyeni hiyo talanta, mkampe yule mwenye talanta kumi.
Võtke talent temalt ära ja andke sellele, kellel on kümme talenti.
29 Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
Sest igaühele, kellel on, sellele antakse veel rohkem, ja igaühelt, kellel pole midagi, võetakse ära seegi, mis tal on.
30 Nanyi mtupeni huyo mtumishi asiyefaa nje, kwenye giza, mahali ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
Nüüd heitke see kasutu sulane välja pimedusse, kus on nutmine ja hammaste kiristamine.“
31 “Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake.
Aga kui inimese Poeg tuleb oma hiilguses ja kõik inglid koos temaga, siis istub ta oma suursugusele troonile.
32 Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.
Kõik tuuakse tema ette. Ta eraldab nad üksteisest, nagu karjane eraldab lambad kitsedest.
33 Atawaweka kondoo upande wake wa kuume, na mbuzi upande wake wa kushoto.
Ta paneb lambad oma paremale käele ja kitsed vasakule käele.
34 “Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njooni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu; urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
Siis ütleb kuningas neile, kes on tema paremal käel: „Tulge siia, mu Isa õnnistatud, ja pärige kuningriik, mis on teile valmistatud maailma algusest peale.
35 Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha,
Sest mul oli nälg ja te andsite mulle süüa. Mul oli janu ja te andsite mulle juua. Ma olin võõras ja te kutsusite mu sisse.
36 nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’
Ma olin alasti ja te riietasite mind. Ma olin haige ja te hoolitsesite minu eest. Ma olin vangis ja te külastasite mind.“
37 “Ndipo wale wenye haki watakapomjibu, ‘Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa tukakulisha, au ukiwa na kiu tukakunywesha?
Siis need, kes on temast paremal, vastavad: „Issand, millal me nägime sind näljasena ja toitsime sind, või janusena ja jootsime sind?
38 Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha, au ukiwa uchi tukakuvika?
Millal nägime sind võõrana ja kutsusime sind sisse või alasti ja riietasime sind?
39 Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza, au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’
Millal nägime sind haigena või vangis ja külastasime sind?“
40 “Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi mlivyomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.’
Kuningas lausub neile: „Ma ütlen teile tõtt: mida iganes te tegite ühele neist, kes on kõige tähtsusetumad, seda tegite mulle.“
41 “Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. (aiōnios g166)
Samuti pöördub ta nende poole, kes on tema vasakul käel, ja ütleb: „Minge minu juurest ära, te hukkamõistetud, igavesse tulle, mis on valmistatud kuradi ja tema inglite jaoks! (aiōnios g166)
42 Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha,
Sest mul oli nälg ja te ei andud mulle midagi süüa. Mul oli janu ja te ei andnud mulle juua.
43 nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza, na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’
Ma olin võõras ja te ei kutsunud mind sisse. Ma olin alasti ja te ei riietanud mind. Ma olin haige ja vangis ja te ei külastanud mind.“
44 “Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi, au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’
Siis vastavad ka nemad: „Issand, millal me nägime sind näljase või janusena, võõrana või alasti, haigena või vangis, ega hoolitsenud sinu eest?“
45 “Naye atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’
Siis kostab ta neile: „Ma ütlen teile tõtt: mida iganes te ei teinud ühele neist, kes on kõige tähtsusetumad, seda ei teinud te mulle.“
46 “Ndipo hawa watakapoingia kwenye adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.” (aiōnios g166)
Nad lähevad ära igavesse hukkamõistu, aga need, kes on head, lähevad igavesse ellu.“ (aiōnios g166)

< Mathayo 25 >