< Mathayo 25 >

1 “Wakati huo, Ufalme wa Mbinguni utakuwa kama wanawali kumi waliochukua taa zao na kwenda kumlaki bwana arusi.
Then shall the kingdom of heaven be likened unto ten virgins, which took their lamps, and went forth to meet the bridegroom.
2 Watano wao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
And five of them were foolish, and five were wise.
3 Wale wapumbavu walichukua taa zao lakini hawakuchukua mafuta ya akiba,
For the foolish, when they took their lamps, took no oil with them:
4 lakini wale wenye busara walichukua taa zao na mafuta ya akiba kwenye vyombo.
but the wise took oil in their vessels with their lamps.
5 Bwana arusi alipokawia kuja wale wanawali wote wakasinzia na kulala.
Now while the bridegroom tarried, they all slumbered and slept.
6 “Usiku wa manane pakawa na kelele: ‘Tazameni, huyu hapa bwana arusi! Tokeni nje mkamlaki!’
But at midnight there is a cry, Behold, the bridegroom! Come ye forth to meet him.
7 “Ndipo wale wanawali wote wakaamka na kuzitengeneza taa zao.
Then all those virgins arose, and trimmed their lamps.
8 Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni mafuta yenu kidogo; taa zetu zinazimika.’
And the foolish said unto the wise, Give us of your oil; for our lamps are going out.
9 “Lakini wale wenye busara wakawajibu, ‘Sivyo, hayatutoshi sisi na ninyi pia. Afadhali mwende kwa wauzao mkajinunulie mafuta yenu.’
But the wise answered, saying, Peradventure there will not be enough for us and you: go ye rather to them that sell, and buy for yourselves.
10 “Nao walipokuwa wakienda kununua mafuta, bwana arusi akafika. Wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia ndani pamoja naye kwenye karamu ya arusi na mlango ukafungwa.
And while they went away to buy, the bridegroom came; and they that were ready went in with him to the marriage feast: and the door was shut.
11 “Baadaye wale wanawali wengine nao wakaja, wakaita, ‘Bwana! Bwana! Tufungulie mlango!’
Afterward come also the other virgins, saying, Lord, Lord, open to us.
12 “Lakini yeye bwana arusi akawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, siwajui ninyi!’
But he answered and said, Verily I say unto you, I know you not.
13 “Kwa hiyo kesheni, kwa sababu hamjui siku wala saa.
Watch therefore, for ye know not the day nor the hour.
14 “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama mtu aliyetaka kusafiri, naye akawaita watumishi wake na kuweka mali yake kwenye uangalizi wao.
For [it is] as [when] a man, going into another country, called his own servants, and delivered unto them his goods.
15 Mmoja akampa talantatano, mwingine talanta mbili, na mwingine talanta moja. Kila mmoja alipewa kwa kadiri ya uwezo wake. Kisha yeye akasafiri.
And unto one he gave five talents, to another two, to another one; to each according to his several ability; and he went on his journey.
16 Yule aliyepewa talanta tano akaenda mara moja akafanya nazo biashara akapata talanta nyingine tano zaidi.
Straightway he that received the five talents went and traded with them, and made other five talents.
17 Yule aliyepewa talanta mbili akafanya vivyo hivyo, akapata nyingine mbili zaidi.
In like manner he also that [received] the two gained other two.
18 Lakini yule mtumishi aliyekuwa amepokea talanta moja, alikwenda akachimba shimo ardhini na kuificha ile fedha ya bwana wake.
But he that received the one went away and digged in the earth, and hid his lord’s money.
19 “Baada ya muda mrefu, yule bwana wa wale watumishi akarudi na kufanya hesabu nao.
Now after a long time the lord of those servants cometh, and maketh a reckoning with them.
20 Yule mtumishi aliyepokea talanta tano akaja, akaleta nyingine tano zaidi. Akasema, ‘Bwana uliweka kwenye uangalizi wangu talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta tano zaidi.’
And he that received the five talents came and brought other five talents, saying, Lord, thou deliveredst unto me five talents: lo, I have gained other five talents.
21 “Bwana wake akamwambia, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
His lord said unto him, Well done, good and faithful servant: thou hast been faithful over a few things, I will set thee over many things: enter thou into the joy of thy lord.
22 “Yule mwenye talanta mbili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, uliweka kwenye uangalizi wangu talanta mbili. Tazama nimepata hapa talanta mbili zaidi.’
And he also that [received] the two talents came and said, Lord, thou deliveredst unto me two talents: lo, I have gained other two talents.
23 “Bwana wake akajibu, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
His lord said unto him, Well done, good and faithful servant; thou hast been faithful over a few things, I will set thee over many things: enter thou into the joy of thy lord.
24 “Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya mbegu.
And he also that had received the one talent came and said, Lord, I knew thee that thou art a hard man, reaping where thou didst not sow, and gathering where thou didst not scatter:
25 Kwa hiyo niliogopa, nikaenda, nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa ile iliyo mali yako.’
and I was afraid, and went away and hid thy talent in the earth: lo, thou hast thine own.
26 “Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna mahali nisipopanda na kukusanya mahali nisipotawanya mbegu.
But his lord answered and said unto him, Thou wicked and slothful servant, thou knewest that I reap where I sowed not, and gather where I did not scatter;
27 Vyema basi, ingekupasa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, ili nirudipo, nichukue ile iliyo yangu na faida yake.
thou oughtest therefore to have put my money to the bankers, and at my coming I should have received back mine own with interest.
28 “‘Basi mnyangʼanyeni hiyo talanta, mkampe yule mwenye talanta kumi.
Take ye away therefore the talent from him, and give it unto him that hath the ten talents.
29 Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
For unto every one that hath shall be given, and he shall have abundance: but from him that hath not, even that which he hath shall be taken away.
30 Nanyi mtupeni huyo mtumishi asiyefaa nje, kwenye giza, mahali ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
And cast ye out the unprofitable servant into the outer darkness: there shall be the weeping and gnashing of teeth.
31 “Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake.
But when the Son of man shall come in his glory, and all the angels with him, then shall he sit on the throne of his glory:
32 Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.
and before him shall be gathered all the nations: and he shall separate them one from another, as the shepherd separateth the sheep from the goats:
33 Atawaweka kondoo upande wake wa kuume, na mbuzi upande wake wa kushoto.
and he shall set the sheep on his right hand, but the goats on the left.
34 “Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njooni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu; urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
Then shall the King say unto them on his right hand, Come, ye blessed of my Father, inherit the kingdom prepared for you from the foundation of the world:
35 Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha,
for I was an hungred, and ye gave me meat: I was thirsty, and ye gave me drink: I was a stranger, and ye took me in;
36 nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’
naked, and ye clothed me: I was sick, and ye visited me: I was in prison, and ye came unto me.
37 “Ndipo wale wenye haki watakapomjibu, ‘Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa tukakulisha, au ukiwa na kiu tukakunywesha?
Then shall the righteous answer him, saying, Lord, when saw we thee an hungred, and fed thee? or athirst, and gave thee drink?
38 Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha, au ukiwa uchi tukakuvika?
And when saw we thee a stranger, and took thee in? or naked, and clothed thee?
39 Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza, au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’
And when saw we thee sick, or in prison, and came unto thee?
40 “Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi mlivyomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.’
And the King shall answer and say unto them, Verily I say unto you, Inasmuch as ye did it unto one of these my brethren, [even] these least, ye did it unto me.
41 “Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. (aiōnios g166)
Then shall he say also unto them on the left hand, Depart from me, ye cursed, into the eternal fire which is prepared for the devil and his angels: (aiōnios g166)
42 Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha,
for I was an hungred, and ye gave me no meat: I was thirsty, and ye gave me no drink:
43 nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza, na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’
I was a stranger, and ye took me not in; naked, and ye clothed me not; sick, and in prison, and ye visited me not.
44 “Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi, au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’
Then shall they also answer, saying, Lord, when saw we thee an hungred, or athirst, or a stranger, or naked, or sick, or in prison, and did not minister unto thee?
45 “Naye atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’
Then shall he answer them, saying, Verily I say unto you, Inasmuch as ye did it not unto one of these least, ye did it not unto me.
46 “Ndipo hawa watakapoingia kwenye adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.” (aiōnios g166)
And these shall go away into eternal punishment: but the righteous into eternal life. (aiōnios g166)

< Mathayo 25 >