< Mathayo 23 >

1 Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake:
Рече тодї Ісус до народу, та до учеників своїх:
2 “Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Mose,
глаголючи: На Мойсейових сїдалищах посїдали письменники та Фарисеї.
3 hivyo inawapasa kuwatii na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini msifuate yale wanayotenda, kwa sababu hawatendi yale wanayohubiri.
Тим усе, що скажуть вам держати, держіть і робіть; по ділам же їх не робіть: говорять бо, й не роблять.
4 Wao hufunga mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata kuinua kidole ili kuisogeza.
Вяжуть бо тяжкі оберемки, що важко носити, й кладуть людям на плечі; самі ж і пальцем своїм не хочуть двигнути їх.
5 “Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao.
Усї ж дїла свої роблять, щоб бачили їх люде: ширять Филактериї свої, й побільшують поли в одежі своїй,
6 Wanapenda kukalia viti vya heshima katika karamu, na vile viti maalum sana katika masinagogi.
і люблять перші місця на бенкетах, і перші сідання по школах,
7 Hupenda kusalimiwa masokoni na kutaka watu wawaite ‘Rabi.’
і витання на торгах, і щоб звали їх люде: Учителю, учителю.
8 “Lakini ninyi msiitwe ‘Rabi,’ kwa sababu mnaye Bwana mmoja na ninyi nyote ni ndugu.
Ви ж не зовіть ся учителями, один бо ваш учитель - Христос; усї ж ви брати.
9 Nanyi msimwite mtu yeyote ‘Baba,’ hapa duniani, kwa maana mnaye Baba mmoja, naye yuko mbinguni.
І отця не звіть собі на землї, один бо Отець у вас, що на небі.
10 Wala msiitwe ‘Mwalimu,’ kwa maana mnaye mwalimu mmoja tu, ndiye Kristo.
І не звіть ся наставниками, один бо в вас наставник - Христос.
11 Yeye aliye mkuu kuliko ninyi nyote miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu.
Більший же між вами нехай буде вам слугою.
12 Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.
Хто ж нести меть ся вгору, принизить ся, а хто принизить ся, пійде вгору.
13 “Lakini ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Kwa maana mnawafungia watu milango ya Ufalme wa Mbinguni. Ninyi wenyewe hamuingii humo, nao wale wanaotaka kuingia mnawazuia. [
Горе ж вам, письменники та Фарисеї, лицеміри! що зачиняєте царство небесне перед людми; ви бо не входите, й тих, що входять, не пускаєте ввійти.
14 Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Mnakula katika nyumba za wajane, nanyi kwa kujifanya kuwa wema, mnasali sala ndefu. Kwa hiyo hukumu yenu itakuwa kuu zaidi.]
Горе вам, письменники та Фарисеї, лицеміри! що жерете доми вдовиць, й задля виду довго молитесь; тим ще тяжчий приймете осуд.
15 “Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja mwongofu, lakini baada ya kumpata, mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili kuliko ninyi! (Geenna g1067)
Горе вам, письменники та Фарисеї, лицеміри! що проходите море й землю, щоб зробити одного нововірця, і коли станеть ся, робите його сином пекла, удвоє гіршим вас. (Geenna g1067)
16 “Ole wenu, viongozi vipofu! Ninyi mwasema, ‘Mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini mtu akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, amefungwa kwa kiapo chake.’
Горе вам, проводирі слїпі, що кажете: Хто клясти меть ся церквою, нїчого; хто ж покленеть ся золотом Церковним, винуватий!
17 Ninyi vipofu wapumbavu! Ni kipi kilicho kikuu zaidi: ni ile dhahabu, au ni lile Hekalu linaloifanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
Дурні й слїпі: що бо більше: золото, чи церква, що осьвячує золото?
18 Pia mnasema, ‘Mtu akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu akiapa kwa sadaka iliyo juu ya madhabahu, amefungwa kwa kiapo chake’
І: Хто клясти меть ся жертівнею, нічого, хто ж покленеть ся даром, що на нїм, винуватий.
19 Ninyi vipofu! Ni kipi kikuu zaidi: ni sadaka, au ni madhabahu yanayoifanya hiyo sadaka kuwa takatifu?
Дурні й слїпі: що бо більше: дар, їй жертівня, що осьвячує дар?
20 Kwa hiyo, mtu aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hayo madhabahu na vitu vyote vilivyo juu yake.
Оце ж, хто клснеть ся жертівнею, кленсть ся нею і всїм, що зверху неї.
21 Naye mtu aapaye kwa Hekalu, huapa kwa hilo Hekalu na kwa huyo akaaye ndani yake.
І хто кленеть ся церквою, кленеть ся нею й тим, що живе в нїй.
22 Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketiye juu ya kiti hicho.
І хто кленеть ся небом, кленеть ся престолом Божим і тим, хто сидить на нїм.
23 “Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu zaidi ya sheria, yaani haki, huruma na uaminifu. Iliwapasa kufanya haya makuu ya sheria bila kupuuza hayo matoleo.
Горе вам, письменппки та Фарисеї, лицеміри! що даєте десятину з мяти, й кропу, й кмину, а залишили важнїще в законї: суд, і милость, і віру. Се повинні були робити, да й того не залишати.
24 Ninyi viongozi vipofu, mnachuja kiroboto lakini mnameza ngamia!
Проводпрі слїпі, що відціджуєте комара, верблюда ж глитаєте.
25 “Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na kutokuwa na kiasi.
Горе вам, письменники та Фарисеї, лицеміри! що очищаєте зверху чашу й блюдо, у серединї ж повні вони здирства та неправди.
26 Ewe Farisayo kipofu! Safisha ndani ya kikombe na sahani kwanza, ndipo nje itakuwa safi pia.
Фарисею слїпий, очисти перш середину чаші й блюда, щоб і верх їх став ся чистий.
27 “Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo yanapendeza kwa nje, lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila aina ya uchafu.
Горе вам, письменники та Фарисеї, лицеміри! що подобитесь гробам побіляним, що зверху являють ся гарними, в середині ж повні кісток мертвих і всякої нечисти.
28 Vivyo hivyo, kwa nje ninyi mnaonekana kwa watu kuwa wenye haki, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
Так і ви зверху являєтесь людям праведні, в серединї ж повні лицемірства та беззаконня.
29 “Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki.
Горе вам, письменники та Фарисеї, лицеміри! що будуєте гроби пророків та украшаєте памятники праведників,
30 Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki katika kumwaga damu ya manabii!’
і мовляєте: Коли б ми були за часів батьків наших, не були б спільниками їх у крові пророків.
31 Hivyo mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii.
Сим же сьвідкуєте самі на себе, що ви сини тих, що вбивали пророків.
32 Haya basi, kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu!
І ви доповнюйте міру батьків ваших.
33 “Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanamu? (Geenna g1067)
Змії, кодло гадюче, як утїчете від суду пекельного? (Geenna g1067)
34 Kwa sababu hii, tazameni, natuma kwenu manabii na wenye hekima na walimu. Baadhi yao mtawaua na kuwasulubisha, na wengine wao mtawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwafuatia kutoka mji mmoja hadi mji mwingine.
Тим же то ось я посилаю до вас пророків, і мудрцїв, і письменників, і одних з них повбиваєте та порозпинаєте, а инших бити мете по школах ваших, та гонити мете від города в город:
35 Hivyo ile damu ya wenye haki wote iliyomwagwa hapa duniani, tangu damu ya Abeli, ambaye alikuwa hana hatia, hadi damu ya Zekaria mwana wa Barakia, mliyemuua kati ya patakatifu na madhabahu, itawajia juu yenu.
щоб упала на вас уся кров праведна, пролита на землї від крові Авеля праведного до крові Захарії, сина Варахіїного, що вбили ви між церквою й жертівнею.
36 Amin, nawaambia, haya yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Істино глаголю вам: Все те прийде на кодло се.
37 “Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka!
Єрусалиме, Єрусалиме, що повбивав єси пророків, і покаменував посланих до тебе! скільки раз хотів я зібрати дітей твоїх, як курка збирав курчат своїх під крила, й не схотїли!
38 Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa.
Оце ж оставляєть ся вам дом ваш пустий.
39 Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.’”
Глаголю бо вам: Не побачите мене від нинї, аж поки скажете: Благословенyyy в імя Господнє!

< Mathayo 23 >