< Mathayo 23 >

1 Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake:
Then Jesus spoke to the multitudes, and to his disciples,
2 “Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Mose,
saying, The scribes and the Pharisees sit in the seat of Moses.
3 hivyo inawapasa kuwatii na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini msifuate yale wanayotenda, kwa sababu hawatendi yale wanayohubiri.
All, therefore, whatever they bid you, do and observe; but do not according to their works; for they say, and do not.
4 Wao hufunga mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata kuinua kidole ili kuisogeza.
They bind heavy burdens, and lay them on men's shoulders, and will not themselves move them with a finger.
5 “Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao.
And all their works they do to be observed by men. They make broad their phylacteries, and enlarge their fringes,
6 Wanapenda kukalia viti vya heshima katika karamu, na vile viti maalum sana katika masinagogi.
and love the first place at feasts, and the chief seats in the synagogues,
7 Hupenda kusalimiwa masokoni na kutaka watu wawaite ‘Rabi.’
and salutations in the markets, and to be called by men, Rabbi.
8 “Lakini ninyi msiitwe ‘Rabi,’ kwa sababu mnaye Bwana mmoja na ninyi nyote ni ndugu.
But be not ye called Rabbi; for one is your teacher; and ye are all brethren.
9 Nanyi msimwite mtu yeyote ‘Baba,’ hapa duniani, kwa maana mnaye Baba mmoja, naye yuko mbinguni.
And call no one your father on the earth; for one is your father, he who is in heaven.
10 Wala msiitwe ‘Mwalimu,’ kwa maana mnaye mwalimu mmoja tu, ndiye Kristo.
Nor be ye called leaders; for one is your leader, the Christ.
11 Yeye aliye mkuu kuliko ninyi nyote miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu.
But the greatest among you will be your servant.
12 Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.
And whoever shall exalt himself will be humbled; and whoever shall humble himself will be exalted.
13 “Lakini ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Kwa maana mnawafungia watu milango ya Ufalme wa Mbinguni. Ninyi wenyewe hamuingii humo, nao wale wanaotaka kuingia mnawazuia. [
But woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites I because ye shut up the kingdom of heaven against men; for ye go not in yourselves, nor suffer those who are entering to go in.
14 Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Mnakula katika nyumba za wajane, nanyi kwa kujifanya kuwa wema, mnasali sala ndefu. Kwa hiyo hukumu yenu itakuwa kuu zaidi.]
15 “Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja mwongofu, lakini baada ya kumpata, mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili kuliko ninyi! (Geenna g1067)
Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye compass sea and land to make one proselyte; and when he is made, ye make him two-fold mole a son of hell than yourselves. (Geenna g1067)
16 “Ole wenu, viongozi vipofu! Ninyi mwasema, ‘Mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini mtu akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, amefungwa kwa kiapo chake.’
Woe to you, blind guides, that say, Whoever sweareth by the temple, it is nothing; but whoever sweareth by the gold of the temple, is bound.
17 Ninyi vipofu wapumbavu! Ni kipi kilicho kikuu zaidi: ni ile dhahabu, au ni lile Hekalu linaloifanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
Fools and blind I for which is greater, the gold, or the temple that sanctifieth the gold?
18 Pia mnasema, ‘Mtu akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu akiapa kwa sadaka iliyo juu ya madhabahu, amefungwa kwa kiapo chake’
And, Whoever sweareth by the altar, it is nothing; but whoever sweareth by the gift that is upon it, is bound.
19 Ninyi vipofu! Ni kipi kikuu zaidi: ni sadaka, au ni madhabahu yanayoifanya hiyo sadaka kuwa takatifu?
Blind men! For which is greater, the gift, or the altar flint sanctifieth the gift?
20 Kwa hiyo, mtu aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hayo madhabahu na vitu vyote vilivyo juu yake.
He then who sweareth by the altar, sweareth by it, and by all that is upon it;
21 Naye mtu aapaye kwa Hekalu, huapa kwa hilo Hekalu na kwa huyo akaaye ndani yake.
and he that sweareth by the temple, sweareth by it, and by him who dwelleth in it;
22 Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketiye juu ya kiti hicho.
and he who sweareth by heaven, sweareth by the throne of God, and by him who sitteth thereon.
23 “Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu zaidi ya sheria, yaani haki, huruma na uaminifu. Iliwapasa kufanya haya makuu ya sheria bila kupuuza hayo matoleo.
Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye pay tithes of the mint, and the dill, and the cummin, and have omitted the weightier matters of the Law, justice, and mercy, and faith; these ought ye to have done, and not to leave those undone.
24 Ninyi viongozi vipofu, mnachuja kiroboto lakini mnameza ngamia!
Blind guides! who strain out a gnat, and swallow a camel.
25 “Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na kutokuwa na kiasi.
Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye make clean the outside of the cup and the platter, but within they are full of robbery and licentiousness.
26 Ewe Farisayo kipofu! Safisha ndani ya kikombe na sahani kwanza, ndipo nje itakuwa safi pia.
Blind Pharisee! cleanse first the inside of the cup, that its outside side also may become clean.
27 “Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo yanapendeza kwa nje, lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila aina ya uchafu.
Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye are like whited sepulchres, which outwardly indeed appear beautiful, but within are full of dead men's bones, and of all uncleanness.
28 Vivyo hivyo, kwa nje ninyi mnaonekana kwa watu kuwa wenye haki, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
Even so ye also outwardly appear righteous to men, but within ye are full of hypocrisy and iniquity.
29 “Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki.
Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! because ye build the sepulchres of the prophets, and adorn the tombs of the righteous,
30 Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki katika kumwaga damu ya manabii!’
and say, If we had been in the days of our fathers, we would not have been partakers with them in the blood of the prophets.
31 Hivyo mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii.
So that ye bear witness against yourselves, that ye are the sons of those who killed the prophets.
32 Haya basi, kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu!
Fill ye up then the measure of your fathers!
33 “Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanamu? (Geenna g1067)
Serpents, brood of vipers! how can ye escape the punishment of hell? (Geenna g1067)
34 Kwa sababu hii, tazameni, natuma kwenu manabii na wenye hekima na walimu. Baadhi yao mtawaua na kuwasulubisha, na wengine wao mtawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwafuatia kutoka mji mmoja hadi mji mwingine.
Therefore, behold, I send to you prophets, and wise men, and scribes; some of them ye will kill and crucify, and some of them ye will scourge in your synagogues, and persecute from city to city;
35 Hivyo ile damu ya wenye haki wote iliyomwagwa hapa duniani, tangu damu ya Abeli, ambaye alikuwa hana hatia, hadi damu ya Zekaria mwana wa Barakia, mliyemuua kati ya patakatifu na madhabahu, itawajia juu yenu.
that on you may come all the righteous blood shed upon the earth, from the blood of righteous Abel to the blood of Zechariah, son of Barachiah, whom ye slew, between the temple and the altar.
36 Amin, nawaambia, haya yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Truly do I say to you, All these things will come upon this generation.
37 “Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka!
Jerusalem, Jerusalem, that killeth the prophets, and stoneth those who are sent to her! How often would I have gathered thy children together, as a hen gathereth her chickens under her wings, and ye would not!
38 Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa.
Lo! your house is left to you desolate.
39 Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.’”
For I say to you, Ye will not see me henceforth, till ye shall say, Blessed is he that cometh in the name of the Lord.

< Mathayo 23 >