< Mathayo 22 >

1 Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
Jesus spoke to them again in parables, saying,
2 “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
“The kingdom of heaven is like a certain king who prepared a marriage feast for his son.
3 Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
He sent out his servants to call those who had been invited to come to the marriage feast, but they would not come.
4 “Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
Again the king sent other servants, saying, 'Tell them who are invited, “See, I have prepared my dinner. My oxen and fattened calves have been killed, and all things are ready. Come to the marriage feast.”'
5 “Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
But they paid no attention and went away, one to his farm, another to his business.
6 Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
The others seized the king's servants, treated them shamefully, and killed them.
7 Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
The king was angry, and he sent his soldiers and they killed those murderers and burned their city.
8 “Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
Then he said to his servants, 'The wedding is ready, but those who were invited were not worthy.
9 Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
Therefore go to the highway crossings and invite as many people to the marriage feast as you can find.'
10 Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
The servants went out to the highways and gathered together all the people they found, both bad and good. So the wedding hall was filled with guests.
11 “Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
But when the king came in to look at the guests, he saw a man there who was not wearing wedding clothes.
12 Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
The king said to him, 'Friend, how did you come in here without wedding clothes?' But the man was speechless.
13 “Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
Then the king said to the servants, 'Bind this man hand and foot, and throw him into the outer darkness, where there will be weeping and the grinding of teeth.'
14 “Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
For many people are called, but few are chosen.”
15 Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
Then the Pharisees went and planned how they might entrap Jesus in his own talk.
16 Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
Then they sent to him their disciples, together with the Herodians. They said to Jesus, “Teacher, we know that you are truthful, and that you teach God's way in truth. You care for no one's opinion, and you do not show partiality between people.
17 Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
So tell us, what do you think? Is it lawful to pay taxes to Caesar or not?”
18 Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
But Jesus understood their wickedness and said, “Why are you testing me, you hypocrites?
19 Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
Show me the coin for the tax.” Then they brought a denarius to him.
20 Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
Jesus said to them, “Whose image and name are these?”
21 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
They said to him, “Caesar's.” Then Jesus said to them, “Then give to Caesar the things that are Caesar's, and to God the things that are God's.”
22 Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.
When they heard it, they marveled. Then they left him and went away.
23 Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
On that day some Sadducees, who say there is no resurrection, came to him. They asked him,
24 “Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
saying, “Teacher, Moses said, 'If a man dies, having no children, his brother must marry his wife and have children for his brother.'
25 Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
There were seven brothers. The first married and then died. Having left no children, he left his wife to his brother.
26 Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
Then the second brother did the same thing, then the third, all the way to the seventh brother.
27 Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
After them all, the woman died.
28 Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
Now in the resurrection, whose wife will she be of the seven brothers? For they all had married her.”
29 Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
But Jesus answered and said to them, “You are mistaken, because you do not know the scriptures or the power of God.
30 Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
For in the resurrection they neither marry nor are given in marriage. Instead, they are like angels in heaven.
31 Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
But concerning the resurrection of the dead, have you not read what was spoken to you by God, saying,
32 ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
'I am the God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob'? God is not the God of the dead, but of the living.”
33 Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
When the crowds heard this, they were astonished at his teaching.
34 Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
But when the Pharisees heard that Jesus had silenced the Sadducees, they gathered themselves together.
35 Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
One of them, a lawyer, asked him a question, testing him—
36 “Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
“Teacher, which is the greatest commandment in the law?”
37 Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
Jesus said to him, “'Love the Lord your God with all your heart, with all your soul, and with all your mind.'
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
This is the great and first commandment.
39 Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
And a second commandment is like it—'Love your neighbor as yourself.'
40 Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
On these two commandments depend the whole law and the prophets.”
41 Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
Now while the Pharisees were still gathered together, Jesus asked them a question.
42 “Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
He said, “What do you think about the Christ? Whose son is he?” They said to him, “The son of David.”
43 Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
Jesus said to them, “How then does David in the Spirit call him Lord, saying,
44 “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
'The Lord said to my Lord, “Sit at my right hand, until I make your enemies your footstool”'?
45 Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
If David then calls the Christ 'Lord,' how is he David's son?”
46 Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.
No one was able to answer him a word, and no man dared ask him any more questions from that day on.

< Mathayo 22 >