< Mathayo 22 >
1 Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
Once more Jesus spoke to them in parables.
2 “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
‘The kingdom of heaven,’ he said, ‘may be compared to a king who gave a banquet in honour of his son’s wedding.
3 Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
He sent his servants to call those who had been invited to the banquet, but they were unwilling to come.
4 “Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
A second time he sent some servants, with orders to say to those who had been invited “I have prepared my meal, my cattle and fat beasts are killed and everything is ready; come to the banquet.”
5 “Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
They, however, took no notice, but went off, one to their farm, another to their business;
6 Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
while the rest, seizing his servants, ill-treated them and killed them.
7 Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
The king, in anger, sent his troops, put those murderers to death, and set their city on fire.
8 “Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
Then he said to his servants “The banquet is prepared, but those who were invited were not worthy.
9 Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
So go to the cross-roads, and invite everyone you find to the banquet.”
10 Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
The servants went out into the roads and collected all the people whom they found, whether bad or good; and the bridal-hall was filled with guests.
11 “Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
But, when the king went in to see his guests, he noticed there a man who had not put on a wedding-robe.
12 Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
So he said to him “My friend, how is it that you came in here without a wedding-robe?” The man was speechless.
13 “Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
Then the king said to the attendants “Tie him hand and foot, and put him out into the darkness outside, where there will be weeping and grinding of teeth.”
14 “Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
For many are called, but few chosen.’
15 Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
Then the Pharisees went away and conferred together as to how they might lay a trap for Jesus in the course of conversation.
16 Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
They sent their disciples, with the Herodians, to say to him, ‘Teacher, we know that you are an honest person, and that you teach the way of God honestly, and are not afraid of anyone; for you pay no regard to a person’s position.
17 Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Tell us, then, what you think. Are we right in paying taxes to the Emperor, or not?’
18 Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
Perceiving their malice, Jesus answered, ‘Why are you testing me, you hypocrites?
19 Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
Show me the coin with which the tax is paid.’ And, when they had brought him a coin,
20 Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
he asked, ‘Whose head and title are these?’
21 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
‘The Emperor’s,’ they answered, at which he said to them, ‘Then pay to the Emperor what belongs to the Emperor, and to God what belongs to God.’
22 Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.
They wondered at his answer, and left him alone and went away.
23 Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
That same day some Sadducees came up to Jesus, maintaining that there is no resurrection. Their question was this, –
24 “Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
‘Teacher, Moses said – “should a man die without children, the man’s brother will become the husband of the widow, and raise a family for his brother.”
25 Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
Now we had living among us seven brothers; of whom the eldest married and died, and, as he had no family, left his wife for his brother.
26 Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
The same thing happened to the second and the third brothers, and indeed to all the seven.
27 Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
The woman herself died last of all.
28 Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
At the resurrection, then, whose wife will she be out of the seven, all of them having been married to her?’
29 Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
‘Your mistake,’ replied Jesus, ‘is due to your ignorance of the scriptures, and of the power of God.
30 Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
For at the resurrection there is no marrying or being married, but all who rise are as angels in heaven.
31 Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
As to the resurrection of the dead, have you not read these words of God –
32 ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
“I am the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob”? He is not the God of dead people, but of living.’
33 Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
The crowds, who had been listening to him, were greatly struck with his teaching.
34 Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
When the Pharisees heard that Jesus had silenced the Sadducees, they collected together.
35 Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
Then one of them, a Student of the Law, to test him, asked this question –
36 “Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
‘Teacher, what is the greatest commandment in the Law?’
37 Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
His answer was, ‘You must love the Lord your God with all your heart, and with all your soul, and with all your mind.
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
This is the great first commandment.
39 Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
The second, which is like it, is this – You must love your neighbour as you love yourself.
40 Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
On these two commandments hang all the Law and the prophets.’
41 Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
Before the Pharisees separated, Jesus put this question to them –
42 “Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
‘What do you think about the Christ? Whose son is he?’ ‘David’s,’ they said.
43 Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
‘How is it, then,’ Jesus replied, ‘that David, speaking under inspiration, calls him “lord,” in the passage –
44 “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
“The Lord said to my Lord: Sit at my right hand, until I put your enemies beneath your feet”?
45 Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
Since, then, David calls him “lord,” how is he David’s son?’
46 Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.
No one could say a word in answer; nor did anyone after that day venture to question him further.