< Mathayo 22 >
1 Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
And Jesus answering, again spoke to them in allegories, saying,
2 “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
“The kingdom of the heavens was likened to a man, a king, who made wedding feasts for his son,
3 Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
and he sent forth his servants to call those having been called to the wedding feasts, and they were not willing to come.
4 “Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
Again he sent forth other servants, saying, Say to those who have been called: Behold, I prepared my early meal, my oxen and the fatlings have been killed, and all things [are] ready, come to the wedding feasts;
5 “Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
and they, having disregarded [it], went away, one to his own field, and the other to his merchandise;
6 Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
and the rest, having laid hold on his servants, mistreated and slew [them].
7 Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
And the king having heard, was angry, and having sent forth his soldiers, he destroyed those murderers, and their city he set on fire;
8 “Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
then he says to his servants, The wedding feast indeed is ready, and those called were not worthy,
9 Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
be going, then, on to the cross-ways, and as many as you may find, call to the wedding feasts.
10 Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
And those servants, having gone forth to the ways, gathered all, as many as they found, both bad and good, and the wedding was filled with those reclining.
11 “Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
And the king having come in to view those reclining, saw there a man not clothed with wedding clothes,
12 Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
and he says to him, Friend, how did you come in here, not having wedding clothes? And he was speechless.
13 “Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
Then the king said to the servants, Having bound his feet and hands, take him up and cast forth into the outer darkness, there will be the weeping and the gnashing of the teeth;
14 “Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
for many are called, and few chosen.”
15 Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
Then the Pharisees having gone, took counsel how they might ensnare Him in words,
16 Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
and they send to Him their disciples with the Herodians, saying, “Teacher, we have known that You are true, and the way of God in truth You teach, and You are not caring for anyone, for You do not look to the face of men;
17 Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
tell us, therefore, what do You think? Is it lawful to give tribute to Caesar or not?”
18 Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
And Jesus having known their wickedness, said, “Why do you tempt Me, hypocrites?
19 Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
Show Me the tribute-coin.” And they brought to Him a denarius;
20 Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
and He says to them, “Whose [is] this image and the inscription?”
21 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
They say to Him, “Caesar’s”; then He says to them, “Render therefore the things of Caesar to Caesar, and the things of God to God”;
22 Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.
and having heard they wondered, and having left Him they went away.
23 Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
In that day there came near to Him Sadducees who are saying there is not a resurrection, and they questioned Him, saying,
24 “Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
“Teacher, Moses said if anyone may die having no children, his brother will marry his wife, and will raise up seed to his brother.
25 Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
And there were with us seven brothers, and the first having married died, and having no seed, he left his wife to his brother;
26 Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
in like manner also the second, and the third, to the seventh,
27 Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
and last of all the woman also died;
28 Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
therefore in the resurrection, of which of the seven will she be wife—for all had her?”
29 Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
And Jesus answering said to them, “You go astray, not knowing the Writings, nor the power of God;
30 Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
for in the resurrection they do not marry, nor are they given in marriage, but are as messengers of God in Heaven.
31 Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
And concerning the resurrection of the dead, did you not read that which was spoken to you by God, saying,
32 ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
I am the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob? God is not a God of dead men, but of living.”
33 Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
And having heard, the multitudes were astonished at His teaching;
34 Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
and the Pharisees, having heard that He silenced the Sadducees, were gathered together to Him;
35 Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
and one of them, a lawyer, questioned, tempting Him, and saying,
36 “Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
“Teacher, which [is] the great command in the Law?”
37 Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
And Jesus said to him, “You will love the LORD your God with all your heart, and with all your soul, and with all your understanding—
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
this is a first and great command;
39 Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
and the second [is] like to it: You will love your neighbor as yourself;
40 Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
on these—the two commands—all the Law and the Prophets hang.”
41 Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
And the Pharisees having been gathered together, Jesus questioned them,
42 “Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
saying, “What do you think concerning the Christ? Of whom is He Son?” They say to Him, “Of David.”
43 Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
He says to them, “How then does David in the Spirit call Him Lord, saying,
44 “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
The LORD said to my Lord, Sit at My right hand, Until I may make Your enemies Your footstool?
45 Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
If then David calls Him Lord, how is He his son?”
46 Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.
And no one was able to answer Him a word, nor did any dare question Him from that day [on].