< Mathayo 22 >
1 Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
耶稣又讲述了一个比喻:
2 “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
“天国好比一个王,为儿子摆设婚筵。
3 Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
他派仆人去请受邀之人来参加婚筵。但他们不肯来。
4 “Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
他再派另一些仆人去,对他们说:‘告诉那些受邀之人,我已经预备好了筵席,宰杀了公牛和肥畜,一切都预备妥当。来参加婚筵吧!’
5 “Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
但那些人却不理会这番邀请,掉头走开,有的去耕田,有的去做买卖,
6 Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
还有些人抓住王的仆人,凌辱他们,把他们杀了。
7 Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
王怒火中烧,派兵消灭那些凶手,焚毁他们的城。
8 “Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
然后对仆人说:‘婚筵已经预备好了,只是受邀之人不配来此。
9 Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
你们去大路口站着,邀请所有遇见之人来参加婚筵。’
10 Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
那些仆人走到街上,把所有遇见之人,无论好坏,都招聚而来,很快婚筵就满座了。
11 “Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
王进来与赴筵之人见面,发现一人没有穿着婚筵的礼服,
12 Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
于是王就对他说:‘朋友,你没有婚筵礼服,怎能进入这里?’那人无话可说。
13 “Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
于是王对侍从说:‘把他的手脚都绑起来,丢到黑暗中,在那里必有哀哭切齿。’
14 “Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
因为受邀人很多,但很少是他选择之人。”
15 Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
法利赛人离开了,聚在一起商量,怎样通过耶稣所说的话来陷害他。
16 Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
他们派了自己的门徒和希律党的门徒一同去问耶稣:“老师,我们知道你为人诚实,你所传授上帝之道皆为真理。你不允许任何人影响你,不在乎头衔或地位。
17 Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
那么请说说你的看法:纳税给凯撒,可不可以?”
18 Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
耶稣看出他们的恶意,就说:“虚伪的人,为什么试探我?
19 Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
把纳税的钱币给我看看。”他们拿了一个银币递给耶稣。
20 Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
耶稣问他们:“这上面是谁的头像,谁的名号?”
21 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
他们回答:“这是凯撒。” 他就对他们说:“凯撒的就应当归于凯撒,上帝的就应当归于上帝。”
22 Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.
这话让他们分外震惊,于是就离开他走了。
23 Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
撒都该人从来不相信复活。那天晚些时候,他们前来问耶稣:
24 “Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
“老师,摩西说如果一个已婚男人死了,没有儿女,他的弟弟就应该娶他的妻子,为哥哥留后。
25 Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
以前我们这里有兄弟七人,老大结了婚,没有孩子就死了,留下妻子给他的弟弟。嫁给老二后,老二死了,嫁给老三,老三死了,
26 Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
直到最后同样的事情又发生在老七身上。
27 Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
最后那女人也死了。
28 Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
那么复活的时候,她会是这七兄弟中哪人的妻子呢?因为他们都娶过她。”
29 Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
耶稣回答:“你们错在不明白圣经,也不知道上帝的能力。
30 Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
复活之后,人们不娶也不嫁,就像天堂的天使一样。
31 Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
关于逝者复活之事,难道你们没读过上帝所说:
32 ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
‘我是亚伯拉罕的上帝,以撒的上帝,雅各的上帝’,上帝并非死人之上帝,而是活人之上帝。”
33 Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
民众听了他所说的,对其教义感到很惊异。
34 Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
听说耶稣让撒都该人无言以对,一群法利赛人便跑来提出更多问题。
35 Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
其中有一个研究法律的专家,试探耶稣说:
36 “Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
“老师,律法中哪一条诫命最重要?”
37 Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
耶稣回答:“‘你要全心、全性、全意爱你的主,你的上帝。’
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
这是最重要的受要诫命。
39 Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
第二条与它相似,那就是:‘要爱人如己。’
40 Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
全部律法和先知之书,均以这两条诫命为根据。”
41 Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
法利赛人聚在一起之时,耶稣问他们:
42 “Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
“你们对基督的看法如何?他是谁的子孙?”他们回答:“大卫的子孙。”
43 Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
耶稣又问:“但受到感召后的大卫为何称他为主?他说
44 “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
‘主对我主说:你坐在我的右边,待我击败你所有敌人。’
45 Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
大卫既然称他为主,他怎么又是大卫的子孙呢?”
46 Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.
无人能够回答。此后再也没有人敢向他提问。