< Mathayo 21 >
1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni. Ndipo Yesu akawatuma wanafunzi wake wawili,
A gdy się przybliżyli do Jeruzalemu, i przyszli do Betfagie, do góry oliwnej, tedy Jezus posłał dwóch uczniów,
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu, nanyi mtamkuta punda amefungwa hapo, na mwana-punda pamoja naye. Wafungueni na mniletee.
Mówiąc im: Idźcie do miasteczka, które jest przeciwko wam, a zaraz znajdziecie oślicę uwiązaną i oślę z nią; odwiążcież je, a przywiedźcie do mnie.
3 Kama mtu yeyote akiwasemesha lolote, mwambieni kwamba Bwana ana haja nao, naye atawaruhusu mwalete mara.”
A jeźliby wam co kto rzekł, powiedzcie, iż Pan ich potrzebuje; a zarazem puści je.
4 Haya yalitukia ili litimie lile lililonenwa na nabii, akisema:
A to się wszystko stało, aby się wypełniło, co powiedziano przez proroka, mówiącego:
5 “Mwambieni Binti Sayuni, ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mnyenyekevu, naye amepanda punda, juu ya mwana-punda, mtoto wa punda.’”
Powiedzcie córce Syońskiej: Oto król twój idzie tobie cichy, a siedzący na oślicy, i na oślęciu, synu oślicy pod jarzmem będącej.
6 Wale wanafunzi wakaenda, wakafanya kama Yesu alivyokuwa amewaagiza.
Szedłszy tedy uczniowie, a uczyniwszy tak, jako im był rozkazał Jezus,
7 Wakamleta yule punda na mwana-punda, nao wakatandika mavazi yao juu ya hao punda, naye Yesu akaketi juu yake.
Przywiedli oślicę i oślę, i włożyli na nie szaty swoje, i wsadzili go na nie.
8 Umati mkubwa wa watu ukatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakakata matawi kutoka kwenye miti, wakayatandaza barabarani.
A wielki lud słał szaty swoje na drodze, a drudzy obcinali gałązki z drzew, i słali na drodze.
9 Ule umati wa watu uliomtangulia na ule uliomfuata ukapiga kelele ukisema, “Hosana, Mwana wa Daudi!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Hosana juu mbinguni!”
A lud wprzód i pozad idący wołał, mówiąc: Hosanna synowi Dawidowemu! błogosławiony, który idzie w imieniu Pańskiem, Hosanna na wysokościach!
10 Yesu alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakauliza, “Huyu ni nani?”
A gdy on wjechał do Jeruzalemu, wzruszyło się wszystko miasto, mówiąc: Któż ten jest?
11 Ule umati wa watu ukajibu, “Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya.”
A lud mówił: Tenci jest Jezus, on prorok z Nazaretu Galilejskiego.
12 Yesu akaingia katika eneo la Hekalu na kuwafukuza wote waliokuwa wakinunua na kuuza vitu Hekaluni. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
Tedy wszedł Jezus do kościoła Bożego, i wygnał wszystkie sprzedawające i kupujące w kościele, a stoły tych, co pieniędzmi handlowali, i stołki sprzedawających gołębie poprzewracał,
13 Akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyangʼanyi.”
I rzekł im: Napisano: Dom mój dom modlitwy nazwany będzie; aleście wy uczynili z niego jaskinię zbójców.
14 Vipofu na vilema wakamwendea kule Hekaluni, naye akawaponya.
Tedy przystąpili do niego ślepi i chromi w kościele, i uzdrowił je.
15 Lakini viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walipoona mambo ya ajabu aliyofanya na kuwasikia watoto wakishangilia katika eneo la Hekalu wakisema, “Hosana Mwana wa Daudi,” walikasirika.
A obaczywszy przedniejsi kapłani i nauczeni w Piśmie cuda, które czynił, i dzieci wołające w kościele, i mówiące: Hosanna synowi Dawidowemu: rozgniewali się.
16 Wakamuuliza Yesu, “Je, unasikia hayo hawa wanayosema?” Akawajibu, “Naam; kwani hamkusoma, “‘Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa’?”
I rzekli mu: Słyszyszże, co ci mówią? A Jezus im rzekł: I owszem. Nigdyścież nie czytali, iż z ust niemowlątek i ssących wykonałeś chwałę?
17 Akawaacha, akatoka nje ya mji, akaenda hadi Bethania, akalala huko.
A opuściwszy je, wyszedł z miasta do Betanii, i tam został;
18 Asubuhi na mapema, Yesu alipokuwa akirudi mjini, alikuwa na njaa.
A rano wracając się do miasta, łaknął.
19 Akauona mtini kando ya barabara, naye akaukaribia, lakini hakupata tunda lolote ila majani. Ndipo akauambia, “Wewe usizae matunda tena kamwe!” Papo hapo ule mtini ukanyauka. (aiōn )
I ujrzawszy jedno figowe drzewo przy drodze, przyszedł do niego, i nie znalazł nic na niem, tylko same liście, i rzekł mu: Niechaj się więcej z ciebie owoc nie rodzi na wieki. I uschło zarazem one figowe drzewo. (aiōn )
20 Wanafunzi wake walipoona jambo hili, wakashangaa, wakamuuliza, “Imekuwaje mtini huu kunyauka ghafula?”
A ujrzawszy to uczniowie, dziwowali się, mówiąc: Jakoć prędko uschło to figowe drzewo!
21 Yesu akawajibu, “Amin, nawaambia, kama mkiwa na imani wala msiwe na shaka, si kwamba mtaweza kufanya tu yale yaliyofanyika kwa huu mtini, bali hata mkiuambia huu mlima, ‘Ngʼoka, ukatupwe baharini,’ litafanyika.
Tedy odpowiadając Jezus, rzekł im: Zaprawdę powiadam wam: Jeźlibyście mieli wiarę, a nie wątpilibyście, nie tylko to, co się stało z figowem drzewem, uczynicie, ale gdybyście i tej górze rzekli: Podnieś się, a rzuć się w morze, stanie się.
22 Yoyote mtakayoyaomba mkisali na mkiamini, mtayapokea.”
I wszystko, o cobyściekolwiek prosili w modlitwie wierząc, weźmiecie.
23 Yesu alipoingia Hekaluni, viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakamjia alipokuwa anafundisha na kusema, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”
A gdy on przyszedł do kościoła, przystąpili do niego, gdy uczył, przedniejsi kapłani i starsi ludu, mówiąc: Którąż mocą to czynisz? a kto ci dał tę moc?
24 Yesu akawajibu, “Nami nitawauliza swali moja. Kama mkinijibu, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
A odpowiadając Jezus, rzekł im: Spytam i ja was o jednę rzecz, którą jeźli mi powiecie, i ja wam powiem, którą mocą to czynię.
25 Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Je, ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wao kwa wao na kusema, “Tukisema ulitoka mbinguni atatuuliza, ‘Mbona basi hamkumwamini?’
Chrzest Jana skąd był? z nieba czyli z ludzi? A oni myśleli sami w sobie, mówiąc: Jeźli powiemy z nieba, rzecze nam: Czemużeście mu tedy nie uwierzyli?
26 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunawaogopa hawa watu, maana wote wanamtambua Yohana kuwa ni nabii.”
Jeźli zaś powiemy z ludzi, boimy się ludu; bo Jana wszyscy mają za proroka.
27 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Sisi hatujui.” Naye akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
A odpowiadając Jezusowi rzekli: Nie wiemy. Rzekł im i on: I ja wam nie powiem, którą mocą to czynię.
28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili. Akamwendea yule wa kwanza akamwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi kwenye shamba la mizabibu leo.’
Ale cóż się wam zda? Człowiek niektóry miał dwóch synów; a przystąpiwszy do pierwszego, rzekł: Synu! idź, rób dziś na winnicy mojej.
29 “Yule mwanawe akamjibu ‘Mimi sitakwenda.’ Baadaye akabadili mawazo yake akaenda.
Ale on odpowiadając rzekł: Nie chcę, a potem obaczywszy się, poszedł.
30 “Kisha yule baba akamwendea yule mwanawe mwingine akamwambia vilevile. Yeye akajibu, ‘Nitakwenda, bwana,’ lakini hakwenda.
A przystąpiwszy do drugiego, rzekł także; a on odpowiadając rzekł: Ja idę, panie! ale nie szedł.
31 “Ni yupi kati yao hao wawili aliyetimiza kile alichotaka baba yake?” Wakamjibu, “Ni yule wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanawatangulia kuingia katika Ufalme wa Mungu.
Któryż z tych dwóch uczynił wolę ojcowską? Rzekli mu: On pierwszy. Rzekł im Jezus: Zaprawdę powiadam wam, że was celnicy i wszetecznice uprzedzają do królestwa Bożego.
32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, lakini hamkumsadiki, lakini watoza ushuru na makahaba wakamsadiki. Nanyi hata mlipoona hayo, baadaye hamkutubu na kumsadiki.
Albowiem przyszedł do was Jan drogą sprawiedliwości, a nie uwierzyliście mu, ale celnicy i wszetecznice uwierzyli mu: a wy widząc to, przecież się nie obaczyliście, abyście mu uwierzyli.
33 “Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na mtu mmoja mwenye shamba ambaye alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akatengeneza shinikizo ndani yake na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha hilo shamba la mizabibu kwa wakulima fulani, naye akaondoka, akasafiri kwenda nchi nyingine.
Drugiego podobieństwa słuchajcie: Człowiek niektóry był gospodarzem, który nasadził winnicę, i płotem ją ogrodził, i wkopał w niej prasę, i zbudował wieżę, i najął ją winiarzom, i odjechał precz.
34 Wakati wa mavuno ulipokaribia, akawatuma watumishi wake kwa hao wapangaji ili kukusanya matunda yake.
A gdy się przybliżył czas odbierania pożytków, posłał sługi swoje do onych winiarzy, aby odebrali pożytki jej.
35 “Wale wapangaji wakawakamata wale watumishi, wakampiga mmoja, wakamuua mwingine, na yule wa tatu wakampiga mawe.
Ale winiarze pojmawszy sługi jego, jednego ubili, a drugiego zabili, a drugiego ukamionowali.
36 Kisha akawatuma kwao watumishi wengine, wengi kuliko wale wa kwanza, nao wale wapangaji wakawatendea vilevile.
Zasię posłał inszych sług, więcej niż pierwszych; i także im uczynili.
37 Mwisho wa yote, akamtuma mwanawe kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
Ale na ostatek posłał syna swego, mówiąc: Będą się wstydzić syna mego.
38 “Lakini wale wapangaji walipomwona mwanawe, wakasemezana wao kwa wao, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, ili tuchukue urithi wake.’
Lecz winiarze, ujrzawszy onego syna, rzekli między sobą: Tenci jest dziedzic; pójdźcie, zabijmy go, a otrzymamy dziedzictwo jego.
39 Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.
Tedy porwawszy go, wyrzucili go precz z winnicy i zabili.
40 “Kwa hiyo, huyo mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanyia nini hao wakulima?”
Gdy tedy pan winnicy przyjdzie, cóż uczyni onym winiarzom?
41 Wakamjibu, “Kwa huzuni kuu atawaangamiza kabisa hao wadhalimu na kulipangisha shamba lake la mizabibu kwa wakulima wengine ambao watampatia fungu lake la matunda wakati wa mavuno.”
Rzekli mu: Złe, źle potraci, a winnicę najmie inszym winiarzom, którzy mu oddawać będą pożytki czasów swoich.
42 Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika Maandiko kwamba: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni. Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni la ajabu machoni petu’?
Rzekł im Jezus: Nie czytaliścież nigdy w Pismach: Kamień, który odrzucili budujący, ten się stał głową węgielną: od Panać się to stało, i dziwne jest w oczach naszych?
43 “Kwa hiyo ninawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa watu wengine wawezao kuzaa matunda yake.
Przetoż powiadam wam: Iż od was odjęte będzie królestwo Boże, i będzie dane narodowi czyniącemu pożytki jego.
44 Yeye aangukaye juu ya jiwe hili atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
A kto by padł na ten kamień, roztrąci się, a na kogo by on upadł, zetrze go.
45 Viongozi wa Makuhani na Mafarisayo waliposikia mifano ya Yesu, walitambua kuwa alikuwa akiwasema wao.
A usłyszawszy przedniejsi kapłani i Faryzeuszowie podobieństwa jego, domyślili się, iż o nich mówił;
46 Wakatafuta njia ya kumkamata, lakini wakaogopa umati wa watu, kwa kuwa watu walimwona Yesu kuwa ni nabii.
A chcąc go pojmać, bali się ludu, ponieważ go mieli za proroka.