< Mathayo 21 >

1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni. Ndipo Yesu akawatuma wanafunzi wake wawili,
When they had almost reached Jerusalem, having come as far as Bethphage, on the Mount of Olives, Jesus sent on two disciples.
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu, nanyi mtamkuta punda amefungwa hapo, na mwana-punda pamoja naye. Wafungueni na mniletee.
‘Go to the village facing you,’ he said, ‘and you will immediately find a donkey tethered, with a foal by her side; untie her, and lead her here for me.
3 Kama mtu yeyote akiwasemesha lolote, mwambieni kwamba Bwana ana haja nao, naye atawaruhusu mwalete mara.”
And, if anyone says anything to you, you are to say this – “The Master wants them”; and he will send them at once.’
4 Haya yalitukia ili litimie lile lililonenwa na nabii, akisema:
This happened in fulfilment of these words in the prophet –
5 “Mwambieni Binti Sayuni, ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mnyenyekevu, naye amepanda punda, juu ya mwana-punda, mtoto wa punda.’”
“Say to the people of Zion – ‘Your King is coming to you, gentle, and riding on a donkey, and on the foal of a beast of burden.’”
6 Wale wanafunzi wakaenda, wakafanya kama Yesu alivyokuwa amewaagiza.
So the disciples went and did as Jesus had directed them.
7 Wakamleta yule punda na mwana-punda, nao wakatandika mavazi yao juu ya hao punda, naye Yesu akaketi juu yake.
They led the donkey and the foal back, and, when they had put their cloaks on them, he seated himself on them.
8 Umati mkubwa wa watu ukatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakakata matawi kutoka kwenye miti, wakayatandaza barabarani.
The immense crowd of people spread their cloaks in the road, while some cut branches off the trees, and spread them on the road.
9 Ule umati wa watu uliomtangulia na ule uliomfuata ukapiga kelele ukisema, “Hosana, Mwana wa Daudi!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Hosana juu mbinguni!”
The crowds that led the way, as well as those that followed behind, kept shouting, ‘God save the Son of David! Blessed is he who comes in the name of the Lord! God save him from on high!’
10 Yesu alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakauliza, “Huyu ni nani?”
When he had entered Jerusalem, the whole city was stirred, and asked –
11 Ule umati wa watu ukajibu, “Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya.”
‘Who is this?’, to which the crowd replied – ‘This is the prophet Jesus from Nazareth in Galilee.’
12 Yesu akaingia katika eneo la Hekalu na kuwafukuza wote waliokuwa wakinunua na kuuza vitu Hekaluni. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
Jesus went into the Temple Courts, and drove out all those who were buying and selling there. He overturned the tables of the money changers, and the seats of the pigeon-dealers,
13 Akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyangʼanyi.”
and said to them, ‘Scripture says “My house will be called a house of prayer”; but you are making it a den of robbers.’
14 Vipofu na vilema wakamwendea kule Hekaluni, naye akawaponya.
While he was still in the Temple Courts, some blind and some lame people came up to him, and he cured them.
15 Lakini viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walipoona mambo ya ajabu aliyofanya na kuwasikia watoto wakishangilia katika eneo la Hekalu wakisema, “Hosana Mwana wa Daudi,” walikasirika.
But, when the chief priests and the teachers of the Law saw the wonderful things that Jesus did, and the boys who were calling out in the Temple Courts ‘God save the Son of David!’, they were indignant,
16 Wakamuuliza Yesu, “Je, unasikia hayo hawa wanayosema?” Akawajibu, “Naam; kwani hamkusoma, “‘Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa’?”
and said to him, ‘Do you hear what these boys are saying?’ ‘Yes,’ answered Jesus, ‘but did you never read the words – “Out of the mouths of babes and sucklings you have called forth perfect praise”?’
17 Akawaacha, akatoka nje ya mji, akaenda hadi Bethania, akalala huko.
Then he left them, and went out of the city to Bethany, and spent the night there.
18 Asubuhi na mapema, Yesu alipokuwa akirudi mjini, alikuwa na njaa.
The next morning, in returning to the city, Jesus became hungry;
19 Akauona mtini kando ya barabara, naye akaukaribia, lakini hakupata tunda lolote ila majani. Ndipo akauambia, “Wewe usizae matunda tena kamwe!” Papo hapo ule mtini ukanyauka. (aiōn g165)
and, noticing a solitary fig tree by the roadside, he went up to it, but found nothing on it but leaves. So he said to it, ‘Never again will fruit be gathered off you.’ And suddenly the fruit tree withered up. (aiōn g165)
20 Wanafunzi wake walipoona jambo hili, wakashangaa, wakamuuliza, “Imekuwaje mtini huu kunyauka ghafula?”
When the disciples saw this, they exclaimed in astonishment, ‘How suddenly the fig tree withered up!’
21 Yesu akawajibu, “Amin, nawaambia, kama mkiwa na imani wala msiwe na shaka, si kwamba mtaweza kufanya tu yale yaliyofanyika kwa huu mtini, bali hata mkiuambia huu mlima, ‘Ngʼoka, ukatupwe baharini,’ litafanyika.
‘I tell you,’ replied Jesus, ‘if you have faith and don’t doubt, you will not only do what has been done to the fig tree, but even if you were to say to this hill “Be lifted up and hurled into the sea!” it would be done.
22 Yoyote mtakayoyaomba mkisali na mkiamini, mtayapokea.”
And whatever you ask for in your prayers will, if you have faith, be granted you.’
23 Yesu alipoingia Hekaluni, viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakamjia alipokuwa anafundisha na kusema, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”
After Jesus had come into the Temple Courts, the chief priests and the elders of the people came up to him as he was teaching, and said, ‘What authority have you to do these things? Who gave you this authority?’
24 Yesu akawajibu, “Nami nitawauliza swali moja. Kama mkinijibu, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
‘I, too,’ said Jesus in reply, ‘will ask you one question; if you will give me an answer to it, then I, also, will tell you what authority I have to act as I do.
25 Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Je, ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wao kwa wao na kusema, “Tukisema ulitoka mbinguni atatuuliza, ‘Mbona basi hamkumwamini?’
It is about John’s baptism. What was its origin? Divine or human?’ But they began arguing among themselves, ‘If we say “divine,” he will say to us “Why then didn’t you believe him?”
26 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunawaogopa hawa watu, maana wote wanamtambua Yohana kuwa ni nabii.”
But if we say “human,” we are afraid of the people, for everyone regards John as a prophet.’
27 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Sisi hatujui.” Naye akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
So the answer they gave Jesus was – ‘We do not know.’ ‘Then I,’ he said, ‘refuse to tell you what authority I have to do these things.
28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili. Akamwendea yule wa kwanza akamwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi kwenye shamba la mizabibu leo.’
What do you think of this? There was a man who had two sons. He went to the elder and said “Go and work in the vineyard today my son.”
29 “Yule mwanawe akamjibu ‘Mimi sitakwenda.’ Baadaye akabadili mawazo yake akaenda.
“Yes, sir,” he answered; but he did not go.
30 “Kisha yule baba akamwendea yule mwanawe mwingine akamwambia vilevile. Yeye akajibu, ‘Nitakwenda, bwana,’ lakini hakwenda.
Then the father went to the second son, and said the same. “I will not,” he answered; but afterwards he was sorry and went.
31 “Ni yupi kati yao hao wawili aliyetimiza kile alichotaka baba yake?” Wakamjibu, “Ni yule wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanawatangulia kuingia katika Ufalme wa Mungu.
Which of the two sons did as his father wished?’ ‘The second,’ they said. ‘I tell you,’ added Jesus, ‘that tax collectors and prostitutes are going into the kingdom of God before you.
32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, lakini hamkumsadiki, lakini watoza ushuru na makahaba wakamsadiki. Nanyi hata mlipoona hayo, baadaye hamkutubu na kumsadiki.
For when John came to you, walking in the path of righteousness, you did not believe him, but tax collectors and prostitutes did; and yet you, though you saw this, even then were not sorry, nor did you believe him.
33 “Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na mtu mmoja mwenye shamba ambaye alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akatengeneza shinikizo ndani yake na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha hilo shamba la mizabibu kwa wakulima fulani, naye akaondoka, akasafiri kwenda nchi nyingine.
‘Listen to another parable. A man, who was an employer, once planted a vineyard, put a fence round it, dug a winepress in it, built a tower, and then let it out to tenants and went abroad.
34 Wakati wa mavuno ulipokaribia, akawatuma watumishi wake kwa hao wapangaji ili kukusanya matunda yake.
When the time for the grape harvest drew near, he sent his servants to the tenants, to receive his share of the produce.
35 “Wale wapangaji wakawakamata wale watumishi, wakampiga mmoja, wakamuua mwingine, na yule wa tatu wakampiga mawe.
But the tenants seized his servants, beat one, killed another, and stoned a third.
36 Kisha akawatuma kwao watumishi wengine, wengi kuliko wale wa kwanza, nao wale wapangaji wakawatendea vilevile.
A second time the owner sent some servants, a larger number than before, and the tenants treated them in the same way.
37 Mwisho wa yote, akamtuma mwanawe kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
As a last resort he sent his son to them. “They will respect my son,” he said.
38 “Lakini wale wapangaji walipomwona mwanawe, wakasemezana wao kwa wao, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, ili tuchukue urithi wake.’
But the tenants, on seeing his son, said to each other “Here is the heir! Come, let us kill him, and get his inheritance.”
39 Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.
So they seized him, and threw him outside the vineyard, and killed him.
40 “Kwa hiyo, huyo mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanyia nini hao wakulima?”
Now, when the owner of the vineyard comes, what will he do to those tenants?’
41 Wakamjibu, “Kwa huzuni kuu atawaangamiza kabisa hao wadhalimu na kulipangisha shamba lake la mizabibu kwa wakulima wengine ambao watampatia fungu lake la matunda wakati wa mavuno.”
‘Miserable wretches!’ they exclaimed, ‘he will put them to a miserable death, and he will let out the vineyard to other tenants, who will pay him his share of the produce at the proper times.’
42 Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika Maandiko kwamba: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni. Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni la ajabu machoni petu’?
Then Jesus added, ‘Have you never read in the scriptures? – “The stone which the builders despised – has now itself become the cornerstone. This cornerstone has come from the Lord, and is marvellous in our eyes.”
43 “Kwa hiyo ninawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa watu wengine wawezao kuzaa matunda yake.
That, I tell you, is why the kingdom of God will be taken from you, and given to a nation that does produce the fruit of the kingdom.
44 Yeye aangukaye juu ya jiwe hili atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
Yes, and he who falls on this stone will be dashed to pieces, while anyone on whom it falls – it will scatter him as dust.’
45 Viongozi wa Makuhani na Mafarisayo waliposikia mifano ya Yesu, walitambua kuwa alikuwa akiwasema wao.
After listening to these parables, the chief priests and the Pharisees saw that it was about them that he was speaking;
46 Wakatafuta njia ya kumkamata, lakini wakaogopa umati wa watu, kwa kuwa watu walimwona Yesu kuwa ni nabii.
yet, although eager to arrest him, they were afraid of the crowds, who regarded him as a prophet.

< Mathayo 21 >