< Mathayo 21 >
1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni. Ndipo Yesu akawatuma wanafunzi wake wawili,
And when they drew near to Jerusalem, and came to Bethphage at the Mount of Olives, Jesus sent two disciples,
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu, nanyi mtamkuta punda amefungwa hapo, na mwana-punda pamoja naye. Wafungueni na mniletee.
saying to them, Go m the village over against you, and immediately ye will find an ass tied, and a colt with her; loose and bring them to me.
3 Kama mtu yeyote akiwasemesha lolote, mwambieni kwamba Bwana ana haja nao, naye atawaruhusu mwalete mara.”
And if any one say aught to you, ye shall say, The Lord hath need of them; and he will immediately send them.
4 Haya yalitukia ili litimie lile lililonenwa na nabii, akisema:
Now this took place, that it might be fulfilled which was spoken through the prophet, saying,
5 “Mwambieni Binti Sayuni, ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mnyenyekevu, naye amepanda punda, juu ya mwana-punda, mtoto wa punda.’”
“Say to the daughter of Zion, Behold, thy king cometh to thee, meek, and riding on an ass, and on a colt the foal of a beast of burden.”
6 Wale wanafunzi wakaenda, wakafanya kama Yesu alivyokuwa amewaagiza.
And the disciples o went, and did as Jesus bade them,
7 Wakamleta yule punda na mwana-punda, nao wakatandika mavazi yao juu ya hao punda, naye Yesu akaketi juu yake.
and brought the ass and the colt, and put on them their garments, and he sat on them.
8 Umati mkubwa wa watu ukatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakakata matawi kutoka kwenye miti, wakayatandaza barabarani.
And very many of the multitude spread their garments in the road; others cut down branches from the trees, and strewed them in the road.
9 Ule umati wa watu uliomtangulia na ule uliomfuata ukapiga kelele ukisema, “Hosana, Mwana wa Daudi!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Hosana juu mbinguni!”
And the multitudes that went before him, and that followed, were crying out, saying, Hosanna to the Son of David! Blessed is he that cometh in the name of the Lord! Hosanna in the highest heavens!
10 Yesu alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakauliza, “Huyu ni nani?”
And when he came into Jerusalem, the whole city was in commotion, saying, Who is this?
11 Ule umati wa watu ukajibu, “Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya.”
And the multitudes said, This is the prophet Jesus, from Nazareth of Galilee.
12 Yesu akaingia katika eneo la Hekalu na kuwafukuza wote waliokuwa wakinunua na kuuza vitu Hekaluni. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
And Jesus went into the temple of God, and cast out all those who sold and bought in the temple, and overturned the tables of the money-changers, and the seats of those who sold the doves;
13 Akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyangʼanyi.”
and said to them, It is written, “My house shall be called a house of prayer; but ye make it a den of robbers.”
14 Vipofu na vilema wakamwendea kule Hekaluni, naye akawaponya.
And the blind and lame came to him in the temple, and he cured them.
15 Lakini viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walipoona mambo ya ajabu aliyofanya na kuwasikia watoto wakishangilia katika eneo la Hekalu wakisema, “Hosana Mwana wa Daudi,” walikasirika.
But the chief priests and the scribes, when they saw the wonderful things which he did, and the children that were crying out in the temple, and saying, Hosanna to the Son of David, were much displeased;
16 Wakamuuliza Yesu, “Je, unasikia hayo hawa wanayosema?” Akawajibu, “Naam; kwani hamkusoma, “‘Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa’?”
and said to him, Dost thou hear what these say? But Jesus saith to them, Yea; did ye never read, “From the mouth of babes and sucklings thou didst prepare praise”?
17 Akawaacha, akatoka nje ya mji, akaenda hadi Bethania, akalala huko.
And he left them, and went out of the city to Bethany, and lodged there.
18 Asubuhi na mapema, Yesu alipokuwa akirudi mjini, alikuwa na njaa.
And in the morning, as he was returning to the city, he was hungry.
19 Akauona mtini kando ya barabara, naye akaukaribia, lakini hakupata tunda lolote ila majani. Ndipo akauambia, “Wewe usizae matunda tena kamwe!” Papo hapo ule mtini ukanyauka. (aiōn )
And seeing one fig-tree by the road-side, he went up to it, and found nothing on it, but leaves only; and he saith to it, Let there be no fruit from thee hencefoward for ever. And immediately the fig-tree withered. (aiōn )
20 Wanafunzi wake walipoona jambo hili, wakashangaa, wakamuuliza, “Imekuwaje mtini huu kunyauka ghafula?”
And the disciples seeing it, marveled, saying, How suddenly did the fig-tree wither!
21 Yesu akawajibu, “Amin, nawaambia, kama mkiwa na imani wala msiwe na shaka, si kwamba mtaweza kufanya tu yale yaliyofanyika kwa huu mtini, bali hata mkiuambia huu mlima, ‘Ngʼoka, ukatupwe baharini,’ litafanyika.
Jesus answering said to them, Truly do I say to you, If ye have faith, and do not doubt, not only shall ye do what hath been done to the fig-tree, but should ye even say to this mountain, Be thou taken up and cast into the sea, it would be done.
22 Yoyote mtakayoyaomba mkisali na mkiamini, mtayapokea.”
And all things whatever ye shall ask in prayer, believing, ye will receive.
23 Yesu alipoingia Hekaluni, viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakamjia alipokuwa anafundisha na kusema, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”
And when he had come into the temple, the chief priests and the elders of the people came to him as he was teaching, and said, By what authority doest thou these things? And who gave thee this authority?
24 Yesu akawajibu, “Nami nitawauliza swali moja. Kama mkinijibu, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
And Jesus answering said to them, I also will ask you one question; which if ye answer me, I too will tell you by what authority I do these things.
25 Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Je, ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wao kwa wao na kusema, “Tukisema ulitoka mbinguni atatuuliza, ‘Mbona basi hamkumwamini?’
The baptism of John, whence was it? From heaven, or from men? And they reasoned among themselves, saying, If we say, From heaven, he will say to us, Why then did ye not believe him?
26 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunawaogopa hawa watu, maana wote wanamtambua Yohana kuwa ni nabii.”
But if we say, From men, we fear the multitude; for all regard John as a prophet.
27 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Sisi hatujui.” Naye akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
And they answered Jesus and said, We do not know. And he said to them, Neither do I tell you by what authority I do these things.
28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili. Akamwendea yule wa kwanza akamwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi kwenye shamba la mizabibu leo.’
But what think ye? A man had two sons: he came to the first, and said, Son, go, work today in the vineyard.
29 “Yule mwanawe akamjibu ‘Mimi sitakwenda.’ Baadaye akabadili mawazo yake akaenda.
And he answered and said, I will not. Afterward he repented, and went.
30 “Kisha yule baba akamwendea yule mwanawe mwingine akamwambia vilevile. Yeye akajibu, ‘Nitakwenda, bwana,’ lakini hakwenda.
And he came to the other and said the same. And he answered and said, I will, sir; and went not.
31 “Ni yupi kati yao hao wawili aliyetimiza kile alichotaka baba yake?” Wakamjibu, “Ni yule wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanawatangulia kuingia katika Ufalme wa Mungu.
Which of the two did the will of his father? They say, The first. Jesus saith to them, Truly do I say to you, that the publicans and the harlots go into the kingdom of God before you.
32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, lakini hamkumsadiki, lakini watoza ushuru na makahaba wakamsadiki. Nanyi hata mlipoona hayo, baadaye hamkutubu na kumsadiki.
For John came to you as a preacher of righteousness, and ye did not believe him; but the publicans and the harlots believed him; and ye, when ye had seen it, did not afterward repent, that ye might believe him.
33 “Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na mtu mmoja mwenye shamba ambaye alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akatengeneza shinikizo ndani yake na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha hilo shamba la mizabibu kwa wakulima fulani, naye akaondoka, akasafiri kwenda nchi nyingine.
Hear another parable. There was a householder, who planted a vineyard, and set a hedge about it, and dug in it a wine-press, and built a tower, and let it out to husbandmen, and went abroad.
34 Wakati wa mavuno ulipokaribia, akawatuma watumishi wake kwa hao wapangaji ili kukusanya matunda yake.
And when the season of the fruits drew near, he sent his servants to the husbandmen, that they might receive his fruits.
35 “Wale wapangaji wakawakamata wale watumishi, wakampiga mmoja, wakamuua mwingine, na yule wa tatu wakampiga mawe.
And the husbandmen took his servants, and beat one, and killed another, and stoned another.
36 Kisha akawatuma kwao watumishi wengine, wengi kuliko wale wa kwanza, nao wale wapangaji wakawatendea vilevile.
Again he sent other servants more than the first; and they dealt with them in the same manner.
37 Mwisho wa yote, akamtuma mwanawe kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
And afterward he sent to them his son, saying, They will respect my son.
38 “Lakini wale wapangaji walipomwona mwanawe, wakasemezana wao kwa wao, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, ili tuchukue urithi wake.’
But the husbandmen, when they saw the son, said among themselves, This is the heir; come, let us kill him, and get his inheritance.
39 Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.
And they took him, and cast him out of the vineyard, and killed him.
40 “Kwa hiyo, huyo mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanyia nini hao wakulima?”
When therefore the lord of the vineyard cometh, what will he do to those husbandmen?
41 Wakamjibu, “Kwa huzuni kuu atawaangamiza kabisa hao wadhalimu na kulipangisha shamba lake la mizabibu kwa wakulima wengine ambao watampatia fungu lake la matunda wakati wa mavuno.”
They say to him, He will bring those wicked men to a miserable end, and will let out his vineyard to other husbandmen, who will render him the fruits in their season.
42 Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika Maandiko kwamba: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni. Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni la ajabu machoni petu’?
Jesus saith to them, Did ye never read in the Scriptures, “The stone which the builders rejected, the same hath become the corner-stone; from the Lord did this come, and it is marvelous in our eyes?”
43 “Kwa hiyo ninawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa watu wengine wawezao kuzaa matunda yake.
Therefore I say to you, that the kingdom of God will be taken away from you, and given to a nation yielding the fruits thereof.
44 Yeye aangukaye juu ya jiwe hili atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
45 Viongozi wa Makuhani na Mafarisayo waliposikia mifano ya Yesu, walitambua kuwa alikuwa akiwasema wao.
And the chief priests and the Pharisees when they heard his parables, knew that he was speaking of them.
46 Wakatafuta njia ya kumkamata, lakini wakaogopa umati wa watu, kwa kuwa watu walimwona Yesu kuwa ni nabii.
And they sought to seize him, but feared the multitudes, because they regarded him as a prophet.