< Mathayo 21 >

1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni. Ndipo Yesu akawatuma wanafunzi wake wawili,
And when they drewe neere to Hierusalem, and were come to Bethphage, vnto the mount of the Oliues, then sent Iesus two disciples,
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu, nanyi mtamkuta punda amefungwa hapo, na mwana-punda pamoja naye. Wafungueni na mniletee.
Saying to them, Goe into the towne that is ouer against you, and anon yee shall finde an asse bounde, and a colt with her: loose them, and bring them vnto me.
3 Kama mtu yeyote akiwasemesha lolote, mwambieni kwamba Bwana ana haja nao, naye atawaruhusu mwalete mara.”
And if any man say ought vnto you, say ye, that the Lord hath neede of them, and straightway he will let them goe.
4 Haya yalitukia ili litimie lile lililonenwa na nabii, akisema:
All this was done that it might be fulfilled, which was spoken by the Prophet, saying,
5 “Mwambieni Binti Sayuni, ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mnyenyekevu, naye amepanda punda, juu ya mwana-punda, mtoto wa punda.’”
Tell ye the daughter of Sion, Beholde, thy King commeth vnto thee, meeke and sitting vpon an asse, and a colte, the foale of an asse vsed to the yoke.
6 Wale wanafunzi wakaenda, wakafanya kama Yesu alivyokuwa amewaagiza.
So the disciples went, and did as Iesus had commanded them,
7 Wakamleta yule punda na mwana-punda, nao wakatandika mavazi yao juu ya hao punda, naye Yesu akaketi juu yake.
And brought the asse and the colt, and put on them their clothes, and set him thereon.
8 Umati mkubwa wa watu ukatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakakata matawi kutoka kwenye miti, wakayatandaza barabarani.
And a great multitude spred their garments in the way: and other cut downe branches from the trees, and strawed them in the way.
9 Ule umati wa watu uliomtangulia na ule uliomfuata ukapiga kelele ukisema, “Hosana, Mwana wa Daudi!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Hosana juu mbinguni!”
Moreouer, the people that went before, and they also that followed, cried, saying, Hosanna to the Sonne of Dauid, Blessed be hee that commeth in the Name of the Lord, Hosanna thou which art in the highest heauens.
10 Yesu alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakauliza, “Huyu ni nani?”
And when he was come into Hierusalem, all the citie was mooued, saying, Who is this?
11 Ule umati wa watu ukajibu, “Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya.”
And the people said, This is Iesus that Prophet of Nazareth in Galile.
12 Yesu akaingia katika eneo la Hekalu na kuwafukuza wote waliokuwa wakinunua na kuuza vitu Hekaluni. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
And Iesus went into the Temple of God, and cast out all them that solde and bought in the Temple, and ouerthrew the tables of the money chagers, and the seates of them that sold doues,
13 Akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyangʼanyi.”
And said to them, it is written, My house shall be called the house of prayer: but ye haue made it a denne of theeues.
14 Vipofu na vilema wakamwendea kule Hekaluni, naye akawaponya.
Then the blinde, and the halt came to him in the Temple, and he healed them.
15 Lakini viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walipoona mambo ya ajabu aliyofanya na kuwasikia watoto wakishangilia katika eneo la Hekalu wakisema, “Hosana Mwana wa Daudi,” walikasirika.
But when the chiefe priestes and Scribes sawe the marueiles that hee did, and the children crying in the Temple, and saying, Hosanna to the Sonne of Dauid, they disdained,
16 Wakamuuliza Yesu, “Je, unasikia hayo hawa wanayosema?” Akawajibu, “Naam; kwani hamkusoma, “‘Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa’?”
And said vnto him, Hearest thou what these say? And Iesus said vnto them, Yea: read ye neuer, By the mouth of babes and sucklings thou hast made perfite the praise?
17 Akawaacha, akatoka nje ya mji, akaenda hadi Bethania, akalala huko.
So hee left them, and went out of the citie vnto Bethania, and lodged there.
18 Asubuhi na mapema, Yesu alipokuwa akirudi mjini, alikuwa na njaa.
And in the morning, as he returned into the citie, he was hungrie,
19 Akauona mtini kando ya barabara, naye akaukaribia, lakini hakupata tunda lolote ila majani. Ndipo akauambia, “Wewe usizae matunda tena kamwe!” Papo hapo ule mtini ukanyauka. (aiōn g165)
And seeing a figge tree in the way, he came to it, and found nothing thereon, but leaues onely, and said to it, Neuer fruite grow on thee henceforwards. And anon the figge tree withered. (aiōn g165)
20 Wanafunzi wake walipoona jambo hili, wakashangaa, wakamuuliza, “Imekuwaje mtini huu kunyauka ghafula?”
And when his disciples saw it, they marueiled, saying, How soone is the figge tree withered!
21 Yesu akawajibu, “Amin, nawaambia, kama mkiwa na imani wala msiwe na shaka, si kwamba mtaweza kufanya tu yale yaliyofanyika kwa huu mtini, bali hata mkiuambia huu mlima, ‘Ngʼoka, ukatupwe baharini,’ litafanyika.
And Iesus answered and said vnto them, Verely I say vnto you, if ye haue faith, and doubt not, ye shall not only doe that, which I haue done to the figge tree, but also if ye say vnto this mountaine, Take thy selfe away, and cast thy selfe into the sea, it shalbe done.
22 Yoyote mtakayoyaomba mkisali na mkiamini, mtayapokea.”
And whatsoeuer ye shall aske in prayer, if ye beleeue, ye shall receiue it.
23 Yesu alipoingia Hekaluni, viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakamjia alipokuwa anafundisha na kusema, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”
And whe he was come into the Temple, the chiefe Priestes, and the Elders of the people came vnto him, as he was teaching, and saide, By what authoritie doest thou these things? and who gaue thee this authoritie?
24 Yesu akawajibu, “Nami nitawauliza swali moja. Kama mkinijibu, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
Then Iesus answered and said vnto them, I also will aske of you a certaine thing, which if ye tell me, I likewise will tell you by what authoritie I doe these things.
25 Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Je, ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wao kwa wao na kusema, “Tukisema ulitoka mbinguni atatuuliza, ‘Mbona basi hamkumwamini?’
The baptisme of Iohn, whence was it? from heauen, or of men? Then they reasoned among themselues, saying, If we shall say, From heauen, he will say vnto vs, Why did ye not then beleeue him?
26 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunawaogopa hawa watu, maana wote wanamtambua Yohana kuwa ni nabii.”
And if we say, Of men, we feare the multitude, for all holde Iohn as a Prophet.
27 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Sisi hatujui.” Naye akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
Then they answered Iesus, and said, We can not tell. And he said vnto them, Neither tell I you by what authoritie I doe these things.
28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili. Akamwendea yule wa kwanza akamwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi kwenye shamba la mizabibu leo.’
But what thinke ye? A certaine man had two sonnes, and came to the elder, and saide, Sonne, goe and worke to day in my vineyarde.
29 “Yule mwanawe akamjibu ‘Mimi sitakwenda.’ Baadaye akabadili mawazo yake akaenda.
But he answered, and said, I will not: yet afterward he repented himselfe, and went.
30 “Kisha yule baba akamwendea yule mwanawe mwingine akamwambia vilevile. Yeye akajibu, ‘Nitakwenda, bwana,’ lakini hakwenda.
Then came he to the second, and said likewise. And he answered, and said, I will, Syr: yet he went not.
31 “Ni yupi kati yao hao wawili aliyetimiza kile alichotaka baba yake?” Wakamjibu, “Ni yule wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanawatangulia kuingia katika Ufalme wa Mungu.
Whether of them twaine did the will of the father? They saide vnto him, The first. Iesus saide vnto them, Verely I say vnto you, that the Publicanes and the harlots goe before you into the kingdome of God.
32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, lakini hamkumsadiki, lakini watoza ushuru na makahaba wakamsadiki. Nanyi hata mlipoona hayo, baadaye hamkutubu na kumsadiki.
For Iohn came vnto you in the way of righteousnes, and yee beleeued him not: but the Publicanes, and the harlots beleeued him, and ye, though ye sawe it, were not mooued with repentance afterward, that ye might beleeue him.
33 “Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na mtu mmoja mwenye shamba ambaye alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akatengeneza shinikizo ndani yake na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha hilo shamba la mizabibu kwa wakulima fulani, naye akaondoka, akasafiri kwenda nchi nyingine.
Heare another parable, There was a certaine housholder, which planted a vineyard, and hedged it round about, and made a winepresse therein, and built a tower, and let it out to husbandmen, and went into a strange countrey.
34 Wakati wa mavuno ulipokaribia, akawatuma watumishi wake kwa hao wapangaji ili kukusanya matunda yake.
And when the time of the fruite drewe neere, hee sent his seruants to the husbandmen to receiue the fruites thereof.
35 “Wale wapangaji wakawakamata wale watumishi, wakampiga mmoja, wakamuua mwingine, na yule wa tatu wakampiga mawe.
And ye husbandmen tooke his seruants and beat one, and killed another, and stoned another.
36 Kisha akawatuma kwao watumishi wengine, wengi kuliko wale wa kwanza, nao wale wapangaji wakawatendea vilevile.
Againe hee sent other seruants, moe then the first: and they did the like vnto them.
37 Mwisho wa yote, akamtuma mwanawe kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
But last of all he sent vnto them his owne sonne, saying, They will reuerence my sonne.
38 “Lakini wale wapangaji walipomwona mwanawe, wakasemezana wao kwa wao, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, ili tuchukue urithi wake.’
But when the husbandmen saw the sonne, they saide among themselues, This is the heire: come, let vs kill him, and let vs take his inheritance.
39 Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.
So they tooke him, and cast him out of the vineyarde, and slewe him.
40 “Kwa hiyo, huyo mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanyia nini hao wakulima?”
When therefore the Lord of the vineyarde shall come, what will hee doe to those husbandmen?
41 Wakamjibu, “Kwa huzuni kuu atawaangamiza kabisa hao wadhalimu na kulipangisha shamba lake la mizabibu kwa wakulima wengine ambao watampatia fungu lake la matunda wakati wa mavuno.”
They saide vnto him, Hee will cruelly destroy those wicked men, and will let out his vineyard vnto other husbandmen, which shall deliuer him the fruites in their seasons.
42 Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika Maandiko kwamba: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni. Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni la ajabu machoni petu’?
Iesus saide vnto them, Read ye neuer in the Scriptures, The stone which the builders refused, the same is made the head of the corner? This was the Lordes doing, and it is marueilous in our eyes.
43 “Kwa hiyo ninawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa watu wengine wawezao kuzaa matunda yake.
Therefore say I vnto you, The kingdome of God shalbe taken from you, and shalbe giuen to a nation, which shall bring foorth the fruites thereof.
44 Yeye aangukaye juu ya jiwe hili atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
And whosoeuer shall fall on this stone, he shalbe broken: but on whomsoeuer it shall fall, it will dash him a pieces.
45 Viongozi wa Makuhani na Mafarisayo waliposikia mifano ya Yesu, walitambua kuwa alikuwa akiwasema wao.
And when the chiefe Priestes and Pharises had heard his parables, they perceiued that hee spake of them.
46 Wakatafuta njia ya kumkamata, lakini wakaogopa umati wa watu, kwa kuwa watu walimwona Yesu kuwa ni nabii.
And they seeking to laye handes on him, feared the people, because they tooke him as a Prophet.

< Mathayo 21 >