< Mathayo 21 >
1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage katika Mlima wa Mizeituni. Ndipo Yesu akawatuma wanafunzi wake wawili,
And when they drew near to Jerusalem, and had come to Bethphage, to the mount of Olives, then Jesus sent two disciples,
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu, nanyi mtamkuta punda amefungwa hapo, na mwana-punda pamoja naye. Wafungueni na mniletee.
saying to them: Go into the village opposite to you, and immediately you will find an ass tied, and a colt with her: loose them, and bring them to me.
3 Kama mtu yeyote akiwasemesha lolote, mwambieni kwamba Bwana ana haja nao, naye atawaruhusu mwalete mara.”
And if any one say any thing to you, you shall reply: The Lord has need of them: and he will immediately send them.
4 Haya yalitukia ili litimie lile lililonenwa na nabii, akisema:
All this was done, that the word might be fulfilled which was spoken by the prophet, saying:
5 “Mwambieni Binti Sayuni, ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mnyenyekevu, naye amepanda punda, juu ya mwana-punda, mtoto wa punda.’”
Say you to the daughter of Zion, Behold, your king comes to you, meek, and sitting upon an ass, and a colt the foal of an ass.
6 Wale wanafunzi wakaenda, wakafanya kama Yesu alivyokuwa amewaagiza.
And the disciples went and did as Jesus commanded them;
7 Wakamleta yule punda na mwana-punda, nao wakatandika mavazi yao juu ya hao punda, naye Yesu akaketi juu yake.
and brought the ass and the colt, and put their mantles on them, and caused him to sit upon them.
8 Umati mkubwa wa watu ukatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakakata matawi kutoka kwenye miti, wakayatandaza barabarani.
And a very great multitude spread their mantles in the road: and others cut branches from the trees, and spread them in the road.
9 Ule umati wa watu uliomtangulia na ule uliomfuata ukapiga kelele ukisema, “Hosana, Mwana wa Daudi!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Hosana juu mbinguni!”
And the multitudes that went before, and that followed after, cried, saying: Hosanna to the son of David. Blessed is he that comes in the name of the Lord. Hosanna in the highest.
10 Yesu alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakauliza, “Huyu ni nani?”
And when he entered Jerusalem, all the city was moved, and said: Who is this?
11 Ule umati wa watu ukajibu, “Huyu ni Yesu, yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya.”
And the multitude said: This is Jesus the prophet, that is from Nazareth of Galilee.
12 Yesu akaingia katika eneo la Hekalu na kuwafukuza wote waliokuwa wakinunua na kuuza vitu Hekaluni. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
And Jesus went into the temple of God, and drove out all that sold and bought in the temple, and overthrew the tables of the money-changers, and the seats of those who sold doves,
13 Akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyangʼanyi.”
and said to them: It is written, My house shall be called a house of prayer; but you have made it a den of robbers.
14 Vipofu na vilema wakamwendea kule Hekaluni, naye akawaponya.
And the blind and the lame came to him in the temple, and he cured them.
15 Lakini viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walipoona mambo ya ajabu aliyofanya na kuwasikia watoto wakishangilia katika eneo la Hekalu wakisema, “Hosana Mwana wa Daudi,” walikasirika.
But when the chief priests and the scribes saw the wonderful things that he did, and the children crying in the temple, and saying, Hosanna to the son of David, their anger was aroused,
16 Wakamuuliza Yesu, “Je, unasikia hayo hawa wanayosema?” Akawajibu, “Naam; kwani hamkusoma, “‘Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao umeamuru sifa’?”
and they said to him: Do you not hear what these say? And Jesus said to them: Yes; have you never read, Out of the mouth of babes and sucklings thou hast perfected praise?
17 Akawaacha, akatoka nje ya mji, akaenda hadi Bethania, akalala huko.
And he left them, and went out of the city to Bethany, and there spent the night.
18 Asubuhi na mapema, Yesu alipokuwa akirudi mjini, alikuwa na njaa.
Now in the morning, as he was returning to the city, he was hungry:
19 Akauona mtini kando ya barabara, naye akaukaribia, lakini hakupata tunda lolote ila majani. Ndipo akauambia, “Wewe usizae matunda tena kamwe!” Papo hapo ule mtini ukanyauka. (aiōn )
and seeing a fig-tree on the road, he went to it, and found nothing on it but leaves; and he said to it: Let no fruit grow on you henceforth forever. And the fig-tree immediately withered. (aiōn )
20 Wanafunzi wake walipoona jambo hili, wakashangaa, wakamuuliza, “Imekuwaje mtini huu kunyauka ghafula?”
And when the disciples saw it, they were astonished, and said: How soon has the fig-tree withered!
21 Yesu akawajibu, “Amin, nawaambia, kama mkiwa na imani wala msiwe na shaka, si kwamba mtaweza kufanya tu yale yaliyofanyika kwa huu mtini, bali hata mkiuambia huu mlima, ‘Ngʼoka, ukatupwe baharini,’ litafanyika.
Jesus answered and said to them: Verily I say to you, If you have faith, and doubt not, you shall do, not only what is done to the fig-tree, but even if you shall say to this mountain, Be taken up, and be thrown into the sea, it shall be done.
22 Yoyote mtakayoyaomba mkisali na mkiamini, mtayapokea.”
And all things that you ask for in prayer, believing, you shall receive.
23 Yesu alipoingia Hekaluni, viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakamjia alipokuwa anafundisha na kusema, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”
And after he had come into the temple, the chief priests and elders of the people came to him as he was teaching, and said: By what authority do you these things? And who gave you this authority?
24 Yesu akawajibu, “Nami nitawauliza swali moja. Kama mkinijibu, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
Jesus answered and said to them: I also will ask you one thing, which if you will tell me, I also will tell you by what authority I do these things.
25 Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Je, ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wao kwa wao na kusema, “Tukisema ulitoka mbinguni atatuuliza, ‘Mbona basi hamkumwamini?’
The immersion of John, whence was it? from heaven, or from men? But they reasoned among themselves, and said, If we reply, From heaven, he will say to us, Why then did you not believe him?
26 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunawaogopa hawa watu, maana wote wanamtambua Yohana kuwa ni nabii.”
But if we reply, From men, we fear the multitude; for all regard John as a prophet.
27 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Sisi hatujui.” Naye akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
And they answered and said to Jesus: We know not. And he said to them: Neither do I tell you by what authority I do these things.
28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili. Akamwendea yule wa kwanza akamwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi kwenye shamba la mizabibu leo.’
But what think you? A man had two sons; and he went to the first, and said, Son, go work to-day in my vineyard.
29 “Yule mwanawe akamjibu ‘Mimi sitakwenda.’ Baadaye akabadili mawazo yake akaenda.
He answered and said, I will not. But he afterward regretted it, and went.
30 “Kisha yule baba akamwendea yule mwanawe mwingine akamwambia vilevile. Yeye akajibu, ‘Nitakwenda, bwana,’ lakini hakwenda.
And he came to the other, and spoke to him in like manner. And he answered and said, I go, sir; and went not.
31 “Ni yupi kati yao hao wawili aliyetimiza kile alichotaka baba yake?” Wakamjibu, “Ni yule wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanawatangulia kuingia katika Ufalme wa Mungu.
Which of the two did the will of his father? They said to him, The first. Jesus said to them: Verily I say to you, The publicans and the harlots go into the kingdom of God before you.
32 Kwa maana Yohana alikuja kwenu kuwaonyesha njia ya haki, lakini hamkumsadiki, lakini watoza ushuru na makahaba wakamsadiki. Nanyi hata mlipoona hayo, baadaye hamkutubu na kumsadiki.
For John came to you in the way of righteousness, and you believed him not. But the publicans and the harlots believed him. And you, when you had seen it, afterward felt no regret, that you might believe him.
33 “Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na mtu mmoja mwenye shamba ambaye alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akatengeneza shinikizo ndani yake na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha hilo shamba la mizabibu kwa wakulima fulani, naye akaondoka, akasafiri kwenda nchi nyingine.
Hear another parable: There was a master of a house who planted a vineyard, and put a hedge around it, and rigged in it a wine-press, and built a tower, and let it out to vine-dressers, and went into another country.
34 Wakati wa mavuno ulipokaribia, akawatuma watumishi wake kwa hao wapangaji ili kukusanya matunda yake.
And when the time of the fruit drew near, he sent his servants to the vine-dressers to receive the fruits of it.
35 “Wale wapangaji wakawakamata wale watumishi, wakampiga mmoja, wakamuua mwingine, na yule wa tatu wakampiga mawe.
And the vine-dressers took his servants, and scourged one, and killed another, and stoned another.
36 Kisha akawatuma kwao watumishi wengine, wengi kuliko wale wa kwanza, nao wale wapangaji wakawatendea vilevile.
Again he sent other servants more than the first: and they treated them in like manner.
37 Mwisho wa yote, akamtuma mwanawe kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
But afterward he sent to them his son, saying, They will reverence my son.
38 “Lakini wale wapangaji walipomwona mwanawe, wakasemezana wao kwa wao, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, ili tuchukue urithi wake.’
But the vine-dressers, when they saw the son, said among themselves, This is the heir; come, let us kill him, and seize upon the inheritance.
39 Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.
And they took him, and carried him out of the vineyard, and killed him.
40 “Kwa hiyo, huyo mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanyia nini hao wakulima?”
Therefore, when the owner of the vineyard comes, what will he do to those vine-dressers?
41 Wakamjibu, “Kwa huzuni kuu atawaangamiza kabisa hao wadhalimu na kulipangisha shamba lake la mizabibu kwa wakulima wengine ambao watampatia fungu lake la matunda wakati wa mavuno.”
They said to him: He will miserably destroy those wicked men, and let out his vineyard to other vine-dressers, who will give him the fruits in their season.
42 Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika Maandiko kwamba: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni. Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni la ajabu machoni petu’?
Jesus said to them: Did you never read in the Scriptures, The stone which the builders rejected has become the head of the corner?
43 “Kwa hiyo ninawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa watu wengine wawezao kuzaa matunda yake.
This was from the Lord, and it is wondrous in our eyes. For this reason, I say to you, The kingdom of God shall be taken from you, and given to a nation that will bring forth the fruits of it.
44 Yeye aangukaye juu ya jiwe hili atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
And he that falls upon this stone shall be dashed to pieces; but him on whom it shall fall, it will make like chaff for the wind.
45 Viongozi wa Makuhani na Mafarisayo waliposikia mifano ya Yesu, walitambua kuwa alikuwa akiwasema wao.
And when the chief priests and the Pharisees heard his parables, they knew that he spoke of them.
46 Wakatafuta njia ya kumkamata, lakini wakaogopa umati wa watu, kwa kuwa watu walimwona Yesu kuwa ni nabii.
And when they sought to lay hold of him, they feared the multitude, because they regarded him as a prophet.