< Mathayo 20 >

1 “Kwa maana Ufalme wa Mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba aliyetoka alfajiri ili kwenda kuajiri vibarua kufanya kazi katika shamba lake la mizabibu.
“For the kingdom of heaven is like a master of a house who went out early in the morning to hire workers for his vineyard.
2 Baada ya kukubaliana na hao vibarua kuwalipa ujira wa dinarimoja kwa siku, akawapeleka kwenye shamba lake la mizabibu.
After agreeing with the workers that they would each receive a denarius for the day, he sent them into his vineyard.
3 “Mnamo saa tatu akatoka tena, akawakuta wengine wamesimama sokoni bila kazi.
About the third hour he went out and saw others standing idle in the marketplace.
4 Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu, nami nitawalipa chochote kilicho haki yenu.’
He said to them, ‘You go into my vineyard as well, and I will give you whatever is right.’
5 Kwa hiyo wakaenda. “Akatoka tena mnamo saa sita na pia saa tisa akafanya vivyo hivyo.
So they went. He went out again about the sixth hour and the ninth hour and did likewise.
6 Mnamo saa kumi na moja akatoka tena akawakuta wengine bado wamesimama bila kazi. Akawauliza, ‘Kwa nini mmesimama hapa kutwa nzima pasipo kufanya kazi?’
About the eleventh hour he went out and found others standing idle and said to them, ‘Why have you been standing here idle all day?’
7 “Wakamjibu, ‘Ni kwa sababu hakuna yeyote aliyetuajiri.’ “Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu.’
They said to him, ‘Because no one has hired us.’ He said to them, ‘You go into my vineyard as well, and you will receive whatever is right.’
8 “Ilipofika jioni, yule mwenye shamba la mizabibu akamwambia msimamizi, ‘Waite hao vibarua na uwalipe ujira wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho na kuishia na wale walioajiriwa kwanza.’
“When evening came, the owner of the vineyard said to his foreman, ‘Call the workers and pay them their wages, beginning with the last and going on to the first.’
9 “Wale vibarua walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakaja na kila mmoja wao akapokea dinari moja.
When those who had been hired about the eleventh hour came, they each received a denarius.
10 Hivyo wale walioajiriwa kwanza walipofika, walidhani watalipwa zaidi. Lakini kila mmoja wao pia alipokea dinari moja.
So when those who had been hired first came, they thought they would receive more, but they also received a denarius each.
11 Walipoipokea, wakaanza kulalamika dhidi ya yule mwenye shamba,
When they received it, they grumbled against the master of the house,
12 wakisema, ‘Hawa watu walioajiriwa mwisho wamefanya kazi kwa muda wa saa moja tu, nawe umewafanya sawa na sisi ambao tumestahimili taabu na joto lote la mchana kutwa?’
saying, ‘These last men worked for one hour, and yoʋ have made them equal to us, who have borne the burden of the day and the scorching heat.’
13 “Yule mwenye shamba akamjibu mmoja wao, ‘Rafiki, sijakudhulumu. Je, hukukubaliana nami kwa ujira wa kawaida wa dinari moja?
But he replied to one of them, ‘Friend, I am doing yoʋ no wrong. Did yoʋ not agree with me to work for a denarius?
14 Chukua ujira wako na uende. Mimi nimeamua kumlipa huyu mtu aliyeajiriwa mwisho kama nilivyokupa wewe.
Take what is yoʋrs and go. I wish to give to this last man just as I gave to yoʋ.
15 Je, sina haki yangu kufanya kile nitakacho na mali yangu mwenyewe? Au unaona wivu kwa kuwa nimekuwa mkarimu?’
Or is it not lawful for me to do what I wish with what is mine? Are yoʋ envious because I am good?’
16 “Vivyo hivyo, wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
So the last will be first, and the first will be last. For many are called, but few are chosen.”
17 Basi Yesu alipokuwa anapanda kwenda Yerusalemu, aliwachukua kando wale wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia,
As Jesus was going up to Jerusalem, he took the twelve disciples aside privately on the way and said to them,
18 “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Nao watamhukumu kifo
“Behold, we are going up to Jerusalem, and the Son of Man will be delivered up to the chief priests and scribes. They will condemn him to death
19 na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa ili wamdhihaki na kumpiga mijeledi na kumsulubisha msalabani. Naye atafufuliwa siku ya tatu!”
and hand him over to the Gentiles to be mocked, flogged, and crucified. But on the third day he will rise again.”
20 Kisha mama yao wana wa Zebedayo akamjia Yesu pamoja na wanawe, naye akapiga magoti mbele yake, akamwomba Yesu amfanyie jambo fulani.
Then the mother of the sons of Zebedee came with her sons to Jesus, and bowing down she asked him for a favor.
21 Yesu akamuuliza, “Unataka nini?” Akajibu, “Tafadhali, wajalie wanangu hawa ili mmoja aketi upande wako wa kuume, na mwingine upande wako wa kushoto katika Ufalme wako.”
So he said to her, “What do yoʋ want?” She said to him, “Declare that one of these two sons of mine may sit on yoʋr right and the other on yoʋr left in yoʋr kingdom.”
22 Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe nitakachonywea mimi?” Wakajibu, “Tunaweza.”
Jesus answered, “You do not know what you are asking. Are you able to drink the cup that I am about to drink, or to be baptized with the baptism that I am baptized with?” The two brothers said to him, “We are able.”
23 Yesu akawaambia, “Kwa kweli kikombe changu mtakinywea, lakini kuketi upande wangu wa kuume au wa kushoto si langu mimi kuwapa. Nafasi hizo ni za wale ambao wameandaliwa na Baba yangu.”
So he said to them, “You will indeed drink my cup and be baptized with the baptism that I am baptized with, but to sit on my right and on my left is not mine to give, but is for those for whom it has been prepared by my Father.”
24 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, waliwakasirikia hao ndugu wawili.
When the ten heard this, they were indignant with the two brothers.
25 Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
So Jesus called them over and said, “You know that the rulers of the Gentiles lord it over them, and their great men exercise authority over them.
26 Isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
But it shall not be so among you. Instead, whoever wants to be great among you must be your servant,
27 naye anayetaka kuwa wa kwanza miongoni mwenu hana budi kuwa mtumwa wenu:
and whoever wants to be first among you must be your slave,
28 kama vile ambavyo Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
just as the Son of Man came not to be served but to serve, and to give his life as a ransom for many.”
29 Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakiondoka Yeriko, umati mkubwa wa watu ulimfuata.
As they were leaving Jericho, a large crowd followed him.
30 Vipofu wawili walikuwa wameketi kando ya barabara. Waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapita, wakapiga kelele wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie!”
And behold, there were two blind men sitting by the road. When they heard that Jesus was passing by, they cried out, “Have mercy on us, Lord, Son of David!”
31 Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze, lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie.”
But the crowd rebuked them, telling them to be silent. Yet they cried out even more loudly, “Have mercy on us, Lord, Son of David!”
32 Yesu akasimama na kuwaita, akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
So Jesus stopped, called them over, and said, “What do you want me to do for you?”
33 Wakamjibu, “Bwana, tunataka kuona.”
They said to him, “Lord, let our eyes be opened.”
34 Yesu akawahurumia na kuwagusa macho yao. Mara macho yao yakapata kuona, nao wakamfuata.
Moved with compassion, Jesus touched their eyes, and immediately their eyes received sight, and they followed him.

< Mathayo 20 >