< Mathayo 20 >
1 “Kwa maana Ufalme wa Mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba aliyetoka alfajiri ili kwenda kuajiri vibarua kufanya kazi katika shamba lake la mizabibu.
"For the kingdom of heaven is like a householder who went out at dawn to hire workmen for his vineyard.
2 Baada ya kukubaliana na hao vibarua kuwalipa ujira wa dinarimoja kwa siku, akawapeleka kwenye shamba lake la mizabibu.
"And when he had agreed with the workmen for two shillings a day, he sent them into his vineyard.
3 “Mnamo saa tatu akatoka tena, akawakuta wengine wamesimama sokoni bila kazi.
"About nine o’clock he went out and noticed some other workmen standing idle in the market-place;
4 Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu, nami nitawalipa chochote kilicho haki yenu.’
"and he said to them, "‘Do you also go into the vineyard, and whatever is just I will pay you.’
5 Kwa hiyo wakaenda. “Akatoka tena mnamo saa sita na pia saa tisa akafanya vivyo hivyo.
"So they went. Again at noon, and about three o’clock, he went out and did the same thing.
6 Mnamo saa kumi na moja akatoka tena akawakuta wengine bado wamesimama bila kazi. Akawauliza, ‘Kwa nini mmesimama hapa kutwa nzima pasipo kufanya kazi?’
"When he went out about five o’clock, he found others standing around, and said to them, "‘Why have you been standing here idle, all the day long?’
7 “Wakamjibu, ‘Ni kwa sababu hakuna yeyote aliyetuajiri.’ “Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye kazi katika shamba langu la mizabibu.’
"‘Because no one has hired us,’ they replied. "He said to them, ‘Do you also go into the vineyard.’
8 “Ilipofika jioni, yule mwenye shamba la mizabibu akamwambia msimamizi, ‘Waite hao vibarua na uwalipe ujira wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho na kuishia na wale walioajiriwa kwanza.’
"And when evening came, the Lord of the vineyard said to his steward, "‘Call the workmen and pay them their wages, beginning with the last hired and ending with the first.’
9 “Wale vibarua walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakaja na kila mmoja wao akapokea dinari moja.
"When those came who had begun at five o’clock, they received two shillings apiece;
10 Hivyo wale walioajiriwa kwanza walipofika, walidhani watalipwa zaidi. Lakini kila mmoja wao pia alipokea dinari moja.
"and when the first came they supposed that they would get more, but they also received each two shillings.
11 Walipoipokea, wakaanza kulalamika dhidi ya yule mwenye shamba,
"And as they took it they began to grumble against the master of the house.
12 wakisema, ‘Hawa watu walioajiriwa mwisho wamefanya kazi kwa muda wa saa moja tu, nawe umewafanya sawa na sisi ambao tumestahimili taabu na joto lote la mchana kutwa?’
"‘Those last men,’ they said, ‘have toiled only one hour, and you have made them equal to us who have borne the burden and the burning heat of the day.’
13 “Yule mwenye shamba akamjibu mmoja wao, ‘Rafiki, sijakudhulumu. Je, hukukubaliana nami kwa ujira wa kawaida wa dinari moja?
"In reply he said to one of them. ‘My friend, I am doing no wrong. Did you not agree with me for two shillings?
14 Chukua ujira wako na uende. Mimi nimeamua kumlipa huyu mtu aliyeajiriwa mwisho kama nilivyokupa wewe.
"Take your wage and begone! I chose to give to this last man the same as to you.
15 Je, sina haki yangu kufanya kile nitakacho na mali yangu mwenyewe? Au unaona wivu kwa kuwa nimekuwa mkarimu?’
"Have I not the right to do what I choose with my own property? Or is your eye evil because I am generous?’
16 “Vivyo hivyo, wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
"So the last shall be first, and the first, last."
17 Basi Yesu alipokuwa anapanda kwenda Yerusalemu, aliwachukua kando wale wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia,
When Jesus was about to go up to Jerusalem, he took the Twelve aside by themselves, and as they went he said to them.
18 “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Nao watamhukumu kifo
"Look! We are on the way up to Jerusalem, and the Son of man will be betrayed to the chief priests and the scribes. They will condemn him to death,
19 na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa ili wamdhihaki na kumpiga mijeledi na kumsulubisha msalabani. Naye atafufuliwa siku ya tatu!”
"and hand him over to the Gentiles to be mocked and scourged and crucified; and on the third day he will rise from the grave."
20 Kisha mama yao wana wa Zebedayo akamjia Yesu pamoja na wanawe, naye akapiga magoti mbele yake, akamwomba Yesu amfanyie jambo fulani.
Then came to him the mother of the sons of Zebedee, with her sons, kneeling down and begging a favor of him.
21 Yesu akamuuliza, “Unataka nini?” Akajibu, “Tafadhali, wajalie wanangu hawa ili mmoja aketi upande wako wa kuume, na mwingine upande wako wa kushoto katika Ufalme wako.”
"What is it you wish?" he said. She answered, "Command that these my two sons may sit upon your right hand and your left in your kingdom."
22 Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe nitakachonywea mimi?” Wakajibu, “Tunaweza.”
23 Yesu akawaambia, “Kwa kweli kikombe changu mtakinywea, lakini kuketi upande wangu wa kuume au wa kushoto si langu mimi kuwapa. Nafasi hizo ni za wale ambao wameandaliwa na Baba yangu.”
"None of you indeed shall drink," he answered, "but to sit at my right hand or at my left is not mine to grant, but belongs to those for whom it has been prepared by my Father."
24 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, waliwakasirikia hao ndugu wawili.
When the ten heard of this, they were indignant at the two brothers;
25 Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
but Jesus called them to him and said. "You know how the rulers of the Gentiles lord it over them, and their great men exercise authority over them.
26 Isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
"Not so shall it be among you. But whoever among you wishes to become great, shall be your minister,
27 naye anayetaka kuwa wa kwanza miongoni mwenu hana budi kuwa mtumwa wenu:
"and whoever wishes to be first among you, shall be your slave;
28 kama vile ambavyo Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
"just as the Son of man came not to be ministered unto, but to minister, and to give his life as a ransom for many."
29 Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakiondoka Yeriko, umati mkubwa wa watu ulimfuata.
Now as they were leaving Jericho a great crowd followed him.
30 Vipofu wawili walikuwa wameketi kando ya barabara. Waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapita, wakapiga kelele wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie!”
And two blind men, sitting by the side of the road, heard that it was Jesus who was passing by, and cried out, "Have pity on us, Master, Son of David!"
31 Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze, lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie.”
But the crowd checked them, to make them keep still. They cried out all the louder, saying, "Master, have pity on us, Son of David!"
32 Yesu akasimama na kuwaita, akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Then Jesus stopped and called to them, "What do you want me to do for you?"
33 Wakamjibu, “Bwana, tunataka kuona.”
"Master," they answered, "let our eyes be opened."
34 Yesu akawahurumia na kuwagusa macho yao. Mara macho yao yakapata kuona, nao wakamfuata.
Then Jesus, moved with compassion, touched their eyes, and they saw at once, and followed him.